Tume mpya ya uchaguzi yaundwa Zanzibar

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Dec 26, 2006
4,184
671
Karume ateua Tume ya Uchaguzi Zanzibar

*Ni ya wajumbe mchanganyiko wa itikadi

Na Ali Suleiman, Zanzibar

RAIS Amani Abeid Karume, ametangaza Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) mpya na kumteua Bw. Khatib Mwinchande Khatib, kuwa Mwenyekiti wa Tume hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa za Ikulu iliyotolewa jana, wajumbe wa Tume hiyo wakiwamo wawili kutoka CUF ambao ni Bw. Ayoub Bakari Hamad na Wakili wa Kujitegemea, Bw. Nassor Khamis Mohamed.

Wengine ni Bw. Said Bakari Jecha, ambaye aliwahi kuwa mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Jaji Omar Othman Makungu, Bw. Abrahman Rashid Mohamed na Bibi Mwanabakari Maalim Ahmed, ambaye ni mjumbe pekee mwanamke katika Tume hiyo.

Uteuzi huo umekuja baada ya Tume ya awali iliyokuwa chini ya Mwenyekiti wake, Bw. Masauni Yussuf Masauni kumaliza muda wake.

Katika Tume iliyopita, ni mjumbe mmoja pekee aliyerudi ambaye ni Mwenyekiti, Bw. Mwinchande.

Tume hiyo inakabiliwa na changamoto kubwa ikiwamo kufanya maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 na Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

Pia tume hiyo wakati ikiwasilisha taarifa yake kwa Rais ilisema yapo marekebisho yanayohitaji kufanyiwa kazi kwa lengo la kuboresha uchaguzi mkuu kuwa huru na wa haki zaidi.


naam jee tume hii itakuwa ni jibu la wazanzibari? jee tume hii itaweza kutuvusha tusirejeee tulipotoka au kufikia walipofika ndugu zetu wakenya?
 
Changa la macho hilo... hakuna jipya another Kiviutu in making....
 
Tume huru sio hoja sana kwa siasa za Zenji.
Swali linakuja kwamba: Je sirikali ya muungano itaendelea kutuma askari kwa wingi na mamluki wengine kwenda visiwani kupiga kura? Iwapo suala hili litajibiwa basi tutakuwa na maoni tofauti kuhusu hiyo tume.
Vinginevyo naungana na Masatu kwamba hili suala ni kiini mazingaombwe.
Tutarudi kule kule kwa Kivuitu
 
Changa la macho hilo... hakuna jipya another Kiviutu in making....

Hapa jipya lipo, waliochaguliwa wanachukua nafasi ya tume iliyomaliza muda wake. Aidha wajumbe wote ni watu waadilifu ndio maana wamechaguliwa. Kwa upande mwingine Mh.Karume anamaliza muda wake hivyo sidhani ka atakuwa anamteua mtu ili kuja kupata fadhila zake. Aidha siasa za Zenj ni tofauti sana na siasa za Kenya.

Malalamiko makubwa katika Tume iliyomaliza muda wake ni usahihi wa Daftali la kudumu la wapiga kura. Maadamu mwenyekiti amerudi tena, hapana shaka ataweza kuondoa kasoro zilizotokea katika daftali hilo muhimu.
 
Hapa jipya lipo, waliochaguliwa wanachukua nafasi ya tume iliyomaliza muda wake. Aidha wajumbe wote ni watu waadilifu ndio maana wamechaguliwa. Kwa upande mwingine Mh.Karume anamaliza muda wake hivyo sidhani ka atakuwa anamteua mtu ili kuja kupata fadhila zake. Aidha siasa za Zenj ni tofauti sana na siasa za Kenya.

Malalamiko makubwa katika Tume iliyomaliza muda wake ni usahihi wa Daftali la kudumu la wapiga kura. Maadamu mwenyekiti amerudi tena, hapana shaka ataweza kuondoa kasoro zilizotokea katika daftali hilo muhimu.

Sawa mtu wa Zenji, na tusubirie muda ufike tuone mapya ya tume hii. Long live Zanzibar, log live Tanzania.
 
Hapa jipya lipo, waliochaguliwa wanachukua nafasi ya tume iliyomaliza muda wake. Aidha wajumbe wote ni watu waadilifu ndio maana wamechaguliwa. Kwa upande mwingine Mh.Karume anamaliza muda wake hivyo sidhani ka atakuwa anamteua mtu ili kuja kupata fadhila zake. Aidha siasa za Zenj ni tofauti sana na siasa za Kenya.

Malalamiko makubwa katika Tume iliyomaliza muda wake ni usahihi wa Daftali la kudumu la wapiga kura. Maadamu mwenyekiti amerudi tena, hapana shaka ataweza kuondoa kasoro zilizotokea katika daftali hilo muhimu.

Mawazo kama yako ndio yatafanya nchi yetu iingie kwenye janga kama Kenya.

Tatizo kwa Zenji ni kuanzia tume ya uchaguzi, daftari la wapiga kura, uhuru wa ku kampeni bila bugudha nk.

Karume angesubiri kidogo na kushirikisha wadau wengine kuteua tume huru. Hii ya sasa ni mazingaombwe yale yale ya Afrika.
Kuna sehemu Masanja ameandika, adui wa maendeleo ya Waafrika ni Waafrika wenyewe.

Miaka na miaka tunashindwa kutatua jambo kama hili ambalo liko wazi.

Kama mtu hana mawazo mabaya kwanini aogope tume ambayo iko huru kwenye macho ya kila mtu?
 
Jukumu la kuteua Tume lipo chini ya rais,hivyo ni wajibu wake kuteua tume kwa wakati wake. Hilo la kusubiri sijui una maana gani? Tena awashirikishe wadau wengine...! wadau gani hawo? Jaribu kufafanua hapo.

Zenj inakwenda kwenye mwaka wa 15 tokea chaguzi ya kwanza ya vyama vingi. Katika muda wote huo imekuwa ikijifunza mengi na imeweza kufahamu mengi katika chaguzi hizo. Wanamageuzi wa kweli wanaweza kudhibitisha hilo.

Uhuru wa Tume, Uhuru wa Kampeni na uhuru wa kupiga kura ni mpana sana sasa kulinganisha na mwaka 1995. Sasa kama unaona kuna mapungufu, ni vema ukayataja ili yaweze kujadiliwa na sio kurukia kwenye kuhukumu tu.

Tatizo la wengi ni kutojua jinsi ya kujadili hoja, badala yake hukimbilia kwenye kuhukumu tu.
 
Jukumu la kuteua Tume lipo chini ya rais,hivyo ni wajibu wake kuteua tume kwa wakati wake. Hilo la kusubiri sijui una maana gani? Tena awashirikishe wadau wengine...! wadau gani hawo? Jaribu kufafanua hapo.

Zenj inakwenda kwenye mwaka wa 15 tokea chaguzi ya kwanza ya vyama vingi. Katika muda wote huo imekuwa ikijifunza mengi na imeweza kufahamu mengi katika chaguzi hizo. Wanamageuzi wa kweli wanaweza kudhibitisha hilo.

Uhuru wa Tume, Uhuru wa Kampeni na uhuru wa kupiga kura ni mpana sana sasa kulinganisha na mwaka 1995. Sasa kama unaona kuna mapungufu, ni vema ukayataja ili yaweze kujadiliwa na sio kurukia kwenye kuhukumu tu.

Tatizo la wengi ni kutojua jinsi ya kujadili hoja, badala yake hukimbilia kwenye kuhukumu tu.

Naona unaongea upupu tupu, hakuna ambacho Zenji mmejifunza kuhusu matatizo ya uchaguzi.

Mna bahati kwamba mna wajomba zenu bara, mkiiba kura wanakuja kuwasaidieni ili msichinjane kama Kenya.

mmeiletea aibu Tanzania kwa kutoa wakimbizi shauri ya ujinga wenu, leo unataka kuongea nini hapa?

Maisha ya binadamu yana thamani na lazima kila juhudi ichukuliwe ili kuhakikisha hata mnyonge anaishi. Lakini sidhani mmejifunza, mwaka 2010 mtaua wengine kama mlivyofanya 1995, 2000 na 2005.

Palipo na nia kila kitu kinawezekana. Katiba inatungwa na watu na kama
Wazanzibri mnataka kutatua matatizo yenu mnaweza kabisa kwa kuitumia katiba hiyo hiyo kukaa pamoja na kuyatatua.

Lakini kila nikiangalia sioni kabisa kwamba mnataka kujifunza, badala yake ni ujinga ule ule tu. Nchi toka 1964 mpaka leo ni umaskini tu wa kunuka bado mnajiona mna haki ya kuongoza hata kwa nguvu.

Acheni ujinga wenu na ngojera zenu hapa, wadanganyeni hao Wadanganyika lakini tunaelewa hakuna la maana mnalofanya hapa zaidi ya kutetea matumbo yenu na ndio maana mnaleta upupu huu.

Inabidi Watanzania kuanza kuchukia kwani sitaki hata Mtanzania mmoja afe kwasababu ya watu ambao ki ukweli hawastahili hata kuongiza kata. Wamepewa nafasi za kuongoza na wamezitumia vibaya.

Acheni Wazanzibari wajiamulie kwa njia ya haki wanataka kuongozwa na nani.

Baada ya kuona yaliyotokea Kenya, sasa nimechukia kweli kweli.
 
RAIS Amani Abeid Karume, ametangaza Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) mpya na kumteua Bw. Khatib Mwinchande Khatib, kuwa Mwenyekiti wa Tume hiyo.

Ha ha ha ha ha ha ha ha!!!!! Mwinyichande mwenyekiti ya tume??? msinivunje mbavu mie!!! Huyu bwana na CCM ni kama samaki na bahari, yaani haelewi somo. Nadhani sasa chama cha kafu inabidi kiingize katika ilani yao ya uchaguzi suala la muafaka kama moja ya sera yao. Kwamba wanaingia katika uchaguzi ili kuendeleza vikao vya muafaka baada ya uchaguzi. Hapa ni mwendo mdundo, muafaka mtindo mmoja mpaka kunako 2050!!!!
 
Kibunango,
Wasiwasi wa wengi wetu hapa ni kwamba tunataka tume ambayo itasema "HAPANA" kwa askari kupigishwa kura Zanzibar kwa namna yoyote ile. Tunataka tume ambayo itatuhakikishia kwamba daftari la kudumu la wapiga kura "HALIBAKWI" na kuwabagua baadhi ya watu, ambapo ikifika siku ya kupiga kura majina yao hayaonekani, kisa tu wanatoka chama fulani ama eneo fulani.
Sasa ukizingatia haya, je tume hii ina 'reputation' hiyo tajwa? Je aliyefanya haya chini ya tume staafu si ni huyu huyu mwenyekiti aliyebakizwa? Hatarudia yale yale?
Tunahofia isije watu wakakimbia na maboksi ya kura vichakani halafu hawachukuliwi hatua!
Wasiwasi wa wengi wetu uko hapo!
 
Kibunango,
Wasiwasi wa wengi wetu hapa ni kwamba tunataka tume ambayo itasema "HAPANA" kwa askari kupigishwa kura Zanzibar kwa namna yoyote ile. Tunataka tume ambayo itatuhakikishia kwamba daftari la kudumu la wapiga kura "HALIBAKWI" na kuwabagua baadhi ya watu, ambapo ikifika siku ya kupiga kura majina yao hayaonekani, kisa tu wanatoka chama fulani ama eneo fulani.
Sasa ukizingatia haya, je tume hii ina 'reputation' hiyo tajwa? Je aliyefanya haya chini ya tume staafu si ni huyu huyu mwenyekiti aliyebakizwa? Hatarudia yale yale?Tunahofia isije watu wakakimbia na maboksi ya kura vichakani halafu hawachukuliwi hatua!
Wasiwasi wa wengi wetu uko hapo!

Idimi you are raising an interesting fact here. This chairperson is part of CCM blood veins. This should send a strong warning to CUF. Watch out CUF, watch out CUF!!!!!
 
nnapenda niweke masahihisho kuwa mwenyekiti aliepita alikuwa ni mzee masauni na huyu wa sasa ni mwinyi chande huyu alikuwa ni kamishna kipindi kile.


na sijasikia CUF kusema lolote hadi sasa huenda hawana mashaka na uteuzi huo.
 
Hii ni tume nyingine ya kisanii, subirini mtayaona.Mwenyekiti wa tume mwalimu wa darasani,halafu ni kada wa CCM!Wajumbe wenyewe ni mbili kwa tatu!
 
Hii ni tume nyingine ya kisanii, subirini mtayaona.Mwenyekiti wa tume mwalimu wa darasani,halafu ni kada wa CCM!Wajumbe wenyewe ni mbili kwa tatu!

Na zogo lenyewe ltaanzia hapa haswaa! Kwa sababu iwapo wajumbe wa CUF watashindwa kukubaliana na wenzao wa sisiemu, si wataamua kupiga kura ili yaishe? Na ndio hapa wale watatu watakapowazidi wale wawili wa "si yu efu".
 
Naona unaongea upupu tupu, hakuna ambacho Zenji mmejifunza kuhusu matatizo ya uchaguzi.

Mna bahati kwamba mna wajomba zenu bara, mkiiba kura wanakuja kuwasaidieni ili msichinjane kama Kenya.
Kaka mbona unalia? Jibu maswala niliyokuuliza na sio kulia lia hapa.

Kwa taarifa yako Mapendekezo yaliyotolewa na Tume iliyomaliza muda wake ambayo kwa undani ni kutokana na malalamiko n kasoro zilizojitokeza katika chaguzi zilizopita ni kama yafuatayo....
  • Mapendekezo haya ni chini ya Tume ya Rais ya pamoja ya utekelezaji Muafaka wa CCM na CUF.

  • Aidha timu ya wataalamu walioshiriki katika kutoa ushauri inaundwa na Bw. Ron Gould kutoka Canada na Profesa Chris Peter kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na wataalumu wengine toka ndani na nje ya Tanzania


Nafasi ya naibu mkurugenzi wa uchaguzi na wasaidizi wakurugenzi wa uchaguzi imeondolewa na sasa imependekezwa kuwa na muundo wa divisheni sita.

Divisheni ya kwanza ni ofisi ndogo ya uchaguzi Pemba itakayosimamia shughuli za kiutawala, fedha na shughuli nyengine zote za uchaguzi, ikiwemo kumshauri Mkurugenzi wa Tume hiyo.

Divisheni ya pili ni ya uchaguzi ambayo itakuwa ikimshauri Mkurugenzi kuandaa utekelezaji wa taratibu za uandikishaji wapiga kura, uteuzi wa wagombea, kampeni za uchaguzi, upigaji kura, kuhesabu na kutangazwa kwa matokeo.

Divisheni ya tatu ni ya utawala na uendeshaji itakayosimamia shughuli za mafunzo kwa wafanyakazi, uajiri na haki za wafanyakazi kwa kuzingatia kanuni za utumishi.

Divisheni ya nne ni ya habari na uhusiano itakayokuwa na majukumu ya kujenga uhusiano kati ya vyombo vya habari na Tume na utoaji wa elimu kwa wananchi.

Divisheni ya tano ni ya fedha, ukaguzi na bajeti itakayokuwa na majukumu ya kuandaa bajeti ya fedha na malipo yanayofanyika kuhakikisha yanakidhi mahitaji yote ya upatikanaji na utumiaji wa fedha.

Divisheni ya sita ni ya sheria itakayofanyakazi ya kumshauri Mkurugenzi wa Uchaguzi masuala yote ya sheria za uchaguzi na kuwa Mwakilishi wa Tume ya Uchaguzi mahakamani wakati inapohitajika kutoa au kujibu hoja kuhusu masuala yote ya uchaguzi yanayotokana na Katiba ya Zanzibar, Sheria ya Uchaguzi na Kanuni zinazotungwa.

Mapendekezo mengine...

Kuwepo na ofisi katika kila wilaya ili kuendeleza zoezi la uandikishaji wapiga kura watakaokuwa wamefikisha umri unaotakiwa kisheria.

Kuangalia watu waliohama katika maeneo na kuingia katika maeneo mengine, ili kuhakikisha wanashiriki katika uchaguzi bila matatizo yoyote.


Sasa kama bado una dukuduku soma hapo juu vizuri, kama hukufahamu uliza swali na sio kulia lia hapa.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom