Tume huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya: Uchaguzi Mkuu 2020 uahirishwe, iundwe serikali ya mseto (ya Muda)

Trust None

JF-Expert Member
Feb 12, 2018
1,260
4,415
Wapinzani wanajifariji tu lakini kwa Katiba ya sasa na Tume ya uchaguzi iliyopo pamoja na hali ya kisiasa iliyopo hivi sasa, hawawezi kupata viti hata robo ya vile walivyopata mwaka 2015 achilia mbali uraisi hawawezi kuuunusa kabisa.

Nashauri uongozi uliopo sasa hivi ujiuzuru mwezi Octoba 2020 halafu iundwe Serikali ya Mpito itakayohusisha vyama vyote vyenye uwakilishi Bungeni ili Serikali hiyo iwe na jukumu kuu la kuhakikisha inasimamia mchakato wa uundwaji wa katiba mpya na taasisi zake.

Hilo likiwezekana, nashauri ile RASIMU YA KWANZA YA WARIOBA ndiyo ifanyiwe kazi, ni nzuri na inayozingatia uzalendo tofauti na rasimu ya pili iliyochakachuliwa kwa maslahi ya wachache.

Kusema ukweli tungekuwa na katiba huru yenye kutambua taasisi huru, kusingekuwa na tabia ya mhimili mmoja kujichimbia chini zaidi huku mihimili mingine ikisifia tu kama ilivyotokea huko Ufaransa miaka ya 1600 pale King Louis xiv aliposema, "I Am The State And My Words Are Law"
 
Bila watu wachache kuamua kuingia msituni kwa ajiri ya kupigania maslahi ya wengi dhidi ya haka ka kikundi kanakoitwa ccm hilo unalolitaka haliwezekani
 
Bila watu wachache kuamua kuingia msituni kwa ajiri ya kupigania maslahi ya wengi dhidi ya haka ka kikundi kanakoitwa ccm hilo unalolitaka haliwezekani
Nani aingie msituni afe, kumbuka una familia ya kulisha sio umati wakufurahisa
 
Plq1llqlq1q
Nani atakayeitetea hiyo Rasimu ya Warioba kwa sasa?!
Kama nchi hii ingekuwa na raia wengi basi hao ndo ilibidi waitetee.ila kwa kuwa nchi Ina watu wengi zaidi kuliko raia na hao watu wapo pale kuangalia maslahi ya matumbo yao ambayo ni ya muda mfupi na yasiyo sustainable basi acha twende hivi hivi
 
Back
Top Bottom