Tuliza Moyo Habiba - (Ombi)

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Tuliza moyo habiba, moyo wako na upoe,
Upunguzie shuruba, hofu yote iondoe,
Penzi letu sio haba, huzuni yako itoe,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Tuliza moyo habiba, ni mbali tumetokea,
Tumeyaona ya huba, ya penzi lilokolea,
Na mengine yenye miba, maumivu kuletea,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Tuliza moyo habiba, ya zamani yamepita,
Uchungu tusije beba, mbeleni tukaja juta,
Tusikijaze kibaba, kwa yale yanayopita,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Tuliza moyo habiba, wenye kusema waseme,
Wanajifanya swahiba, sumu yao waiteme,
Yarabi twalia toba, hawa ni mapaka shume,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Tuliza moyo habiba, penzi letu likolee,
Wa mbinguni yeye Baba, dua zetu apokee,
Atujaze mara saba, penzi letu lendelee,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Tuliza moyo habiba, la moyoni nimesema,
Busu langu liwe tiba, likutakialo mema,
Moyoni ninakubeba, u mawazoni daima,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)
 
Tuliza moyo habiba, moyo wako na upoe,
Upunguzie shuruba, hofu yote iondoe,
Penzi letu sio haba, huzuni yako itoe,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Tuliza moyo habiba, ni mbali tumetokea,
Tumeyaona ya huba, ya penzi lilokolea,
Na mengine yenye miba, maumivu kuletea,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Tuliza moyo habiba, ya zamani yamepita,
Uchungu tusije beba, mbeleni tukaja juta,
Tusikijaze kibaba, kwa yale yanayopita,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Tuliza moyo habiba, wenye kusema waseme,
Wanajifanya swahiba, sumu yao waiteme,
Yarabi twalia toba, hawa ni mapaka shume,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Tuliza moyo habiba, penzi letu likolee,
Wa mbinguni yeye Baba, dua zetu apokee,
Atujaze mara saba, penzi letu lendelee,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Tuliza moyo habiba, la moyoni nimesema,
Busu langu liwe tiba, likutakialo mema,
Moyoni ninakubeba, u mawazoni daima,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)



MwaKjj hongera kwa tungo hii, kuna mdada hapa JF, nijui status yake wala yako katika mahusiano ya kimapenzi, ila naona kama mngefaana sana na ingependeza kama huu utungo ungeudedicate wake.
 
Nina wazo. Kutokana na baadhi ya wana jf kuonyesha kipaji cha kuandika mashairi, kwa nini tusianzishe kamtindo ka kuchagua mada halafu kila mpenda kuandika shairi anaandika shairi lake kuhusu hiyo mada? Nafikiri hii style itachangamsha zaidi utundu wa mashairi, zaidi ya kumsubiri mkjj atoke halafu ndio ajibiwe.

Pengine tunaweza kutengeneza kitabu cha jf mashairi na kupeleka huko mashuleni kitumike. Who knows?

Ni wazo tu!
 
MwaKjj hongera kwa tungo hii, kuna mdada hapa JF, nijui status yake wala yako katika mahusiano ya kimapenzi, ila naona kama mngefaana sana na ingependeza kama huu utungo ungeudedicate wake.

Yeah.. I dedicate this one to her..! (I really don't know which one..)
 
Yeah.. I dedicate this one to her..! (I really don't know which one..)

ya hands are full, stop pushin ya way in like a bull,
just like me you do, silently i act cool,
no more school to you, in court the ball is with you,
mkjj you rule, but careful as you eat ya gruel.

SteveD. (Echo from the trench)
 
habiba wangu jamani, mbona wanitesa wangu moyo
wajua ninavyo kutamani, mbona waumiza yangu roho
kipenzi changu cha thamani, mbona wanyanyasa pangu koo
habiba wangu wa amani, nini nimekutenda wangu polo?

habiba rudi kwangu jamani, haki napatwa na masimanzi
chonde chonde tafadhali, lako tamu penzi bado nalihitaji
usiku wapita mwenzio silali, nakuwaza wangu manzi
habiba wangu asali, nini nifanye tafadhali?

kumbuka mengi twafanya, tuwapo pamoja mahala
nguruko pale tulichofanya, miili yetu tulitoa kafara
utamu wetu ulichanganya, chini ulitaka galagala
habiba wangu wa chanya, nini chakutia hasara?

usiku wa harusi ya dadayo, kawe rumba tulicheza
kisha tukafuatilia yafuatayo, pata chumba hatukuweza
tukaishia kwenye uzio, ngoma yetu tamu tukacheza
habiba wangu wa enzio, nini nifanye wangu pweza?

kuendelea siwezi tena, naomba nifikirie kwa undani
mwenzio nashindwa hema, naomba nijie kitandani
hakika vizuri nitakutenda, naomba ikuingie kichwani
habiba wangu nakupenda, nini wataka wangu wa ubani?
 
habiba wangu jamani, mbona wanitesa wangu moyo
wajua ninavyo kutamani, mbona waumiza yangu roho
kipenzi changu cha thamani, mbona wanyanyasa pangu koo
habiba wangu wa amani, nini nimekutenda wangu polo?

habiba rudi kwangu jamani, haki napatwa na masimanzi
chonde chonde tafadhali, lako tamu penzi bado nalihitaji
usiku wapita mwenzio silali, nakuwaza wangu manzi
habiba wangu asali, nini nifanye tafadhali?

kumbuka mengi twafanya, tuwapo pamoja mahala
nguruko pale tulichofanya, miili yetu tulitoa kafara
utamu wetu ulichanganya, chini ulitaka galagala
habiba wangu wa chanya, nini chakutia hasara?

usiku wa harusi ya dadayo, kawe rumba tulicheza
kisha tukafuatilia yafuatayo, pata chumba hatukuweza
tukaishia kwenye uzio, ngoma yetu tamu tukacheza
habiba wangu wa enzio, nini nifanye wangu pweza?

kuendelea siwezi tena, naomba nifikirie kwa undani
mwenzio nashindwa hema, naomba nijie kitandani
hakika vizuri nitakutenda, naomba ikuingie kichwani
habiba wangu nakupenda, nini wataka wangu wa ubani?



Mkuu,


Umetulia mwanakwetu.
 
Tuliza moyo habiba, moyo wako na upoe,
Upunguzie shuruba, hofu yote iondoe,
Penzi letu sio haba, huzuni yako itoe,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!....

Tuliza moyo habiba,.......
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)

Tuliza moyo habiba, mwenziyo amekuomba
Siye twajua ka kwiba, na sasa anajikomba
Pia amuomba Toba, ahisi ume m-bamba!
Bi Habiba mi nasema, uliza kwani kunani?

Anaanza kwa upole, ahisi ushagundua
Uhuni wake wa kale, adhani umejulia
Mabusu hayo chelele, ni nini anafichia?
Bi Habiba mi nasema, uliza kwani kunani?

Anajihisi mwenziyo, ila ashindwa tamka
Achunguza wako moyo, na yepi uta tamka
Anayahepa machoyo, ya kwake yeshamtoka!
Bi Habiba mi nasema, uliza kwani kunani?

Habiba mwana fulani, fungua macho wa kwetu
Uliza yule ni nani, nimsemaye Sikitu
muangalie machoni, asije kuficha kitu
Bi Habiba mi nasema, uliza kwani kunani?
 
Tuliza moyo habiba, moyo wako na upoe,
Upunguzie shuruba, hofu yote iondoe,
Penzi letu sio haba, huzuni yako itoe,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Tuliza moyo habiba, ni mbali tumetokea,
Tumeyaona ya huba, ya penzi lilokolea,
Na mengine yenye miba, maumivu kuletea,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Tuliza moyo habiba, ya zamani yamepita,
Uchungu tusije beba, mbeleni tukaja juta,
Tusikijaze kibaba, kwa yale yanayopita,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Tuliza moyo habiba, wenye kusema waseme,
Wanajifanya swahiba, sumu yao waiteme,
Yarabi twalia toba, hawa ni mapaka shume,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Tuliza moyo habiba, penzi letu likolee,
Wa mbinguni yeye Baba, dua zetu apokee,
Atujaze mara saba, penzi letu lendelee,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Tuliza moyo habiba, la moyoni nimesema,
Busu langu liwe tiba, likutakialo mema,
Moyoni ninakubeba, u mawazoni daima,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)


Mahabuba nimeshindwa, moyo wangu kutuliza
mazito nalemewa, iweje leo waniuliza
uchungu nahemewa, na yako miujiza
moyo hauwezi tulia, na penzi lisiloshibisha

Mbali tumetokea, iweje leo ukumbuke
kwa yale yaliyotokea, lazima ugutuke
hofu imenienea, natafuta mahala niruke
moyo hauwezi tulia, na penzi lisiloshibisha

penzi lazima lishibishe, iwe kwako iwe kwangu
nani akueleweshe, matendo yako uchungu kwangu
kidonda usinitoneshe, ubichi bado kwangu
moyo hauwezi tulia, na penzi lisiloshibisha

kurudi kwako asilani, hata kwa maneno matamu
nisijeonekana hayawani, penzi limepoteza hatamu
penzi limepata miwani, penzi pofu sina hamu
moyo hauwezi tulia, na penzi lisiloshibisha


 
Du kumbe Mwanakijiji ni hatari kwa mashairi ya mapenzi, siku hizi wanasema umebobea
 
Wakijiji umelonga,acha nami ninene
Shairilo limekonga,limelizidi sebene
Kidogo nataka chonga,Naomba dakika nne
Kwa Habiba umegonga,Ninaye mwaka wa nne

Wajificha huko shamba,Habiba wamwacha town
wakijiji nakuomba,Mwache apate amani
Huku alipo atamba,Ananipenda Amani
Kwa Habiba umegonga,ninaye mwaka wa nne

Habiba alikupenda,na wewe ukamtenda
Ukamwacha njia panda,ukaamua kuhanda
Ameamua kuenda,sasa watoka udenda
Kwa Habiba umegonga,ninaye mwaka wa nne

Pendo lake Habiba,ni tamu siwezi sema
Kama chakula nishashiba,mpaka nashindwa kuhema
Pendo lake kwangu tiba,Mola atupe |Uzima
Kwa Habiba umegonga,Ninaye mwaka wa nne

Uchungu ninaupata,Kwa mateso uliompa
Chalinze mpaka Msata,Shambani ukamtupa
Ulimfanya Kuruta,kwa kazi ulizompa
Sasa kwangu amefika,Na kamwe sitamtupa

Kadi tamati wa tama,Mimi mwisho nimefika
Habiba ni wangu mama,Moyo wangu kaushika
wakiji kachunge ndama,Niache mimi na 'mama'
Kwa Habiba umegonga,ninaye mwaka wa nne
 
habiba habebi,haibi hububu,
wala hatubu kwa uongo kukuhubu,
hana haiba na mpenda misiba,
heri yako wewe ushapata mahaba.


mimi sijawahi kupendwa baba,
kupata habiba mwenye kwangu huba,
nimekulia upweke na huzuni nimeshiba,
tuache hadithi zake mahabuba.

miaka 18, nitafute tuonane,
kisha tuelewane kisha tuoane,
tukaishi saanane tukifa tuzikane,

nakukumbusha popote ulipo,
chambi chambicho kificho,
chambi ukipata chambilecho,
chambilecho ni kifo ukiwa nacho
,
 
Tuliza moyo habiba, moyo wako na upoe,
Upunguzie shuruba, hofu yote iondoe,
Penzi letu sio haba, huzuni yako itoe,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Tuliza moyo habiba, ni mbali tumetokea,
Tumeyaona ya huba, ya penzi lilokolea,
Na mengine yenye miba, maumivu kuletea,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Tuliza moyo habiba, ya zamani yamepita,
Uchungu tusije beba, mbeleni tukaja juta,
Tusikijaze kibaba, kwa yale yanayopita,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Tuliza moyo habiba, wenye kusema waseme,
Wanajifanya swahiba, sumu yao waiteme,
Yarabi twalia toba, hawa ni mapaka shume,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Tuliza moyo habiba, penzi letu likolee,
Wa mbinguni yeye Baba, dua zetu apokee,
Atujaze mara saba, penzi letu lendelee,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Tuliza moyo habiba, la moyoni nimesema,
Busu langu liwe tiba, likutakialo mema,
Moyoni ninakubeba, u mawazoni daima,
Tuliza moyo habiba, Penzi letu limeshiba!

Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)

MHE shairi lako zuri sema tunarudi kulekule you will develop what you practise, ebu soma michango yetu utagundua wabongo tunapenda mapenzi kuliko jambo lolote. ndio maana nchi inauzwa tukiwa tunawaza mapenzi... tutungie shairi la kuponda mafisadi bwana.. hizi za mapenzi waachie akina mr blue na banana zoro
 
MHE shairi lako zuri sema tunarudi kulekule you will develop what you practise, ebu soma michango yetu utagundua wabongo tunapenda mapenzi kuliko jambo lolote. ndio maana nchi inauzwa tukiwa tunawaza mapenzi... tutungie shairi la kuponda mafisadi bwana.. hizi za mapenzi waachie akina mr blue na banana zoro


Naunga Mikono na miguu yote
 
Back
Top Bottom