Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Kuna baadhi yetu tumekuwa na wasiwasi sana na huu uwekezaji wa fedha za wanachama wa mifumo ya hifadhi ya jamii mkubwa kati yao ukiwa ni wa NSSF. NSSF siyo mfuko pekee lakini ndio mfuko ambao unatumiwa sana kuwekeza kwenye miradi mingi na mkataba mkubwa ambao wengi watakuwa wanaufahamu ni wa ujenzi wa daraja la KIgamboni. CAG katika ripoti yake anadokeza vitu vichache ambavyo vinapaswa kuangiliwa na wanachama na watu wote wanaofuatilia mambo haya:
My Take:
Je wanachama wa NSSF na mifuko mingine ya jamii wanapaswa kujali jinsi mifuko hii inavyowekeza?
7.7 Usimamizi wa Uwekezaji Katika Mifuko ya Pensheni Usimamiaji wa uwekezaji ni usimamizi wa kitaalam wa dhamana mbalimbali (hisa, na dhamana nyingine) na mali (kwa mfano, mali zisizohamishika) ili kufikia malengo ya uwekezaji kwa ajili ya faida ya wawekezaji. Hii inaweza kuhusisha upembuzi wa mali, hisa, utekelezaji na ufuatiliaji wa mipango inayoendelea kwenye uwekezaji. Hata hivyo, katika hili, mapungufu kadhaa yameonekana wakati wa ukaguzi wa uwekezaji unaofanywa na kusimamiwa na mifuko ya hifadhi ya Jamii kama ilivyoelezwa hapa chini:
(i) Uwekezaji Katika Chuo Kikuu cha Dodoma
Ukaguzi wa uwekezaji wa NSSF katika Chuo Kikuu cha Dodoma ulibaini mapungufu kadha wa kadha. Ukaguzi ulibaini kuwa Mfuko haukusaini mkataba wa mradi kwa ajili ya ujenzi wa awamu ya pili ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM). Mfuko ulitumia jumla ya Shilingi bilioni 234 katika mradi huu lakini ulisaini mkataba wa awamu ya kwanza wa Shilingi bilioni 35.2 tu. Majengo kwa ajili ya awamu ya kwanza yalikamilika na kuwekwa katika matumizi mwezi Septemba, 2008.
Mpaka wakati wa ukaguzi, Mfuko haujaweza kukusanya malipo ya pango kutoka Serikalini na hadi sasa limbikizo la riba limefikia thamani ya Shilingi bilioni 14. Zaidi ya hayo, kiasi kilichotumika kufadhili mradi awamu ya kwanza kimekuwa kikitambuliwa kama mkopo na sehemu ya riba kuwa mtaji kinyume na masharti ya mkataba ambayo yanasema mradi ambao ni aina ya kubuni, kujenga, kumiliki na kuhamisha (Design Build, Own and Transfer), ambapo Mfuko utapokea kodi iliyokokotolewa kwa gharama za uwekezaji na riba ambayo ni 15% kwa kipindi cha miaka 10. Mifuko mingine ambayo imewekeza katika Chuo Kikuu cha Dodoma katika mikataba kama hiyo ni kama inavyoonyeshwa katika jedwali hapa chini:
My Take:
Je wanachama wa NSSF na mifuko mingine ya jamii wanapaswa kujali jinsi mifuko hii inavyowekeza?