Tuliyaishi haya zamani yetu, sasa yamebaki kumbukumbu ya kuvutia kama si kuchekesha

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,633
697,754
1. Kupakwa dawa ya vidonda iitwayo GV
2. Kung'olewa jino kwa uzi
3. Ubwabwa kupikwa jumapili tu
4. Kidonda kuwekwa unga wa 'rangi mbili' a.k.a tetracycline
5. Kupamba kadi na pamba sebuleni
6. Ukumbi wa sherehe kupambwa kwa toilet paper
7. Kunyolewa kwa mkasi
8. Kufunga pesa kwenye leso au pindo la kanga
9. Wavulana kuvaa nguo ya ndani aina moja nchi nzima (VIP), usiombe ikakatika ukakuta imebana kifua.
10. Ku-rewind kanda kwa peni
11. Nchi nzima Kuangalia Movie ya Commando John, Double Impact, Rambo na Bruce Lee..
12. Watoto Wa Mtaa Mzima Kufahamiana sababu ya kucheza Wote Jioni Kombolela na Kibaba..
13. Kuunguzana na tunda ya Ubuyu baada ya kulisugua chini
14. Kukata ndala, eti ni kifutio
15. Kunyolewa msalaba shuleni kisa nywele ndefu
16. Kuweka Vibox box kwenye Shati la shule Mgongoni..
17. Kuweka Shati la Shule "Blue" eti liwe maridadi.
18. Ubitozi Ulikuwa ni Kusimamisha Kola Ya Shati.
19. Ukiandika Barua kwa Umpendae lazima uchore moyo na Mkuki na lazima upulizie Pafyumu ya "YU".

20. Hata kama Mlikuwa mmegombana January lakini Mtu anakwambia ngoja shule ikifungwa

Kama kuna mengine ongezea
 
Aisee umenichekesha sana. Ni kweli Mshana Jr haya mambo yalikuwepo. Nakumbuka wakubwa zangu walipokuwa primary walikuwa wanaandikia zile kalamu za wino (Fontain).

Ilikuwa marufuku kuandikia hizi Bic etc za sasa. Na madukani kulikuwa na vichupa vya wino kwa ajili ya hizo kalamu. Nilikuwa naona wino ukipungua walikuwa wanakwenda kwenye majani yenye umande wa asubuhi wananyonya na zile kalamu, hivyo umande unachanganyika na wino.
 
Zilikuwa ni kama kifuko kidogo kilicho wazi pande zote, kilichopigwa nyuzi chache kwa chini katikakati ya miguu.
Hizi kuumbuka ilikuwa lazima
maxresdefault.jpg
 
1. Kupakwa dawa ya vidonda iitwayo GV
2. Kung'olewa jino kwa uzi
3. Ubwabwa kupikwa jumapili tu
4. Kidonda kuwekwa unga wa 'rangi mbili' a.k.a tetracycline
5. Kupamba kadi na pamba sebuleni
6. Ukumbi wa sherehe kupambwa kwa toilet paper
7. Kunyolewa kwa mkasi
8. Kufunga pesa kwenye leso au pindo la kanga
9. Wavulana kuvaa nguo ya ndani aina moja nchi nzima (VIP), usiombe ikakatika ukakuta imebana kifua.
10. Ku rewind kanda kwa peni
11. Nchi nzima Kuangalia Movie ya Commando John, Double Impact, Rambo na Bruce Lee..
12. Watoto Wa Mtaa Mzima Kufahamiana sababu ya kucheza Wote Jioni Kombolela na Kibaba..
13. Kuunguzana na tunda ya Ubuyu baada ya kulisugua chini
14. Kukata ndala, eti ni kifutio
15. Kunyolewa msalaba shuleni kisa nywele ndefu
16. Kuweka Vibox box kwenye Shati la shule Mgongoni..
17. Kuweka Shati la Shule "Blue" eti liwe maridadi.
18. Ubitozi Ulikuwa ni Kusimamisha Kola Ya Shati.
19. Ukiandika Barua kwa Umpendae lazima uchore moyo na Mkuki na lazima upulizie Pafyumu ya "YU".

20. Hata kama Mlikuwa mmegombana January lakini Mtu anakwambia ngoja shule ikifungwa

Kama kuna mengine ongezea
Wapi Kanda Bongoman, Aurlus Mabele, Diblo Dibala, Defao, Awilo Longomba, Pepe Kale, Extra Musica, Wenge BCBG, Yondo Sister, Tshala Mwana, Mbilia Bel, Tabu Lei, Madilu System, Zaiko Langalanga, Mbuta Likasu,
 
Kuna mchezo ulikuwa unaitwa "tobo dunda" unachezwa kama mpira wa miguu ila hakuna magoli halafu unachaguliwa mti mmoja wa kukimbia kushika ikitokea mpira umepita katikati ya miguu yako "tobo", inapotokea unapigwa ngumi pona yako ni mbio zako kwenda kushika mti. Ulikuwa mchezo wa kishujaa sana wakati ule
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom