Tulitakiwa tukemee kitendo cha Kassim Majaliwa kuingilia Muhimili wa Bunge..

Interest

JF-Expert Member
Apr 11, 2015
3,432
7,055
Sijui kwanini tulishangilia pale Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipomwambia Naibu Rais wa Bunge la Africa, St. Masele, asiitike wito wa Spika wa Bunge, Job Ndugai na aendelee na majukumu yake.

Lile lilikuwa ni kosa na kutoheshimu uhuru wa muhimili mwingine. Kosa kubwa mno!

Yes, kuna udhaifu mkubwa sana kwa Bunge letu la sasa na namna Ndugai anavyoliendesha, lakini tusiruhusu precedence mbaya kama ambayo PM alitaka kuiweka.

Nampongeza Mhe. Masele kwa kuonesha nidhamu na kuitika wito wa Spika, Job Ndugai. Nimemuona akitinga bungeni asubuhi ya leo >>
 
Back
Top Bottom