Tulipokuwa primary,unakumbuka?

Hahahahahaaaaa, duh wakuu mmenikumbusha mbali sana, tulikuwa tukiwahi namba na endapo una mshkaji wako kachelewa unamuwekea jiwe au dumu la maji kwenye mstari ikiwa ni ishara kuwa kuna mtu, hlf Jumatatu na Alhamis ilikuwa ni ukaguzi, kuna mwalimu alikuwa na ruler ya mbao kwenye ukaguzi yeye alikuwa anapenda kutazama kucha tu, akikukuta na kucha ndefu unakula ruler za vidoleni sita! Hlf uniform ilikuwa ni viatu vyeusi au brown tu! Hahahaaaaa, ikifika wakati wa kuingia darasani baada ya assembly kuna band inapiga kama gwaride la jeshi vile! Hlf watoto wa kihindi na kiarabu ndo walikuwa matajiri zetu mida ya break, anakununulia mihogo ya kukaanga na visheti ili umpe ulinzi kwa wababe wa shule au umpange kwenye timu ya darasa! Duh it was sooo funny, I really miss those great great moments, hlf kuna mwalimu mkuu alinunua gari yake Land rover alikuwa akipaki chini ya mwembe karibu na assembly, hataki mtu aiguse, ukiigusa tu unakwenda kusafisha vyoo ambavyo vilikuwa vichafu balaa, alikuwa akiitwa Mwalimu Sitta, hiyo ilikuwa ni experience ya Lake Primary huko Mwanza! Miaka ya 86- 92!
Du! You have made my day amazing!
 
Hahahahahaaaaa, duh wakuu mmenikumbusha mbali sana, tulikuwa tukiwahi namba na endapo una mshkaji wako kachelewa unamuwekea jiwe au dumu la maji kwenye mstari ikiwa ni ishara kuwa kuna mtu, hlf Jumatatu na Alhamis ilikuwa ni ukaguzi, kuna mwalimu alikuwa na ruler ya mbao kwenye ukaguzi yeye alikuwa anapenda kutazama kucha tu, akikukuta na kucha ndefu unakula ruler za vidoleni sita! Hlf uniform ilikuwa ni viatu vyeusi au brown tu! Hahahaaaaa, ikifika wakati wa kuingia darasani baada ya assembly kuna band inapiga kama gwaride la jeshi vile! Hlf watoto wa kihindi na kiarabu ndo walikuwa matajiri zetu mida ya break, anakununulia mihogo ya kukaanga na visheti ili umpe ulinzi kwa wababe wa shule au umpange kwenye timu ya darasa! Duh it was sooo funny, I really miss those great great moments, hlf kuna mwalimu mkuu alinunua gari yake Land rover alikuwa akipaki chini ya mwembe karibu na assembly, hataki mtu aiguse, ukiigusa tu unakwenda kusafisha vyoo ambavyo vilikuwa vichafu balaa, alikuwa akiitwa Mwalimu Sitta, hiyo ilikuwa ni experience ya Lake Primary huko Mwanza! Miaka ya 86- 92!

Ninyi mlikuwa mjini na maendeleo yalikuwepo. Kwetu miaka hiyo 1984-1990 kijijini kuvaa kiatu ni neema ya ajabu, wengi tulitinga shule pekupeku hadi darasa la sita ndio wengi wanapata kutia kiatu mguuni. Hata hivyo ilikuwa lazima kuhakikisha visigino vyako havina nyufa, vinginevyo fito kila siku halali yako...habari ya mwalimu kununua gari enzi hizo inaashiria 'ujasiriamali' wa hali ya juu maana hata leo walimu wa shule ya msingi ni wachache wanaweza kumudu kununua na kuhudumia gari!
 
Mkuu nakukumbusha tu japo Mimi ni wa enzi za mwinyi kwenye English alikuwa Neema ,Musa and Baraka namkumbuka Neema kwa kuibiwa kikapu sokoni tukiwa darasa la sita pia nakumbuka Baraka alipomshauri baba yake waanzishe mradi wa ufugaji wa Kuku ili jogoo wakiwika wamwamushe awahi shule
 
aisee ni unakumbuka "CHOPEKO NA MNOFU"?? HESABU ZA KIKWETU nilikua noma sana aisee kulikua hakuna swali linalonishinda,ila naona mtaani kitabu kilichotupa msingi wa kujua kusoma wengi wetu enzi hizo "SOMA KWA HATUA" nakumbuka enzi hizo mwalimu wa darasa la kwanza lazima awe bibi,sio siku izi mwalimu hajui ata uchungu wa mtoto upo vipi bana!!!! nimekumbuka mbali sana wacha tu nilie.mimi
 
Hakika ya kale ni dhaabu, ki ukweli ukiusoma uzi huu lazima ulengwe na machozi pia lazima ucheke sana kwa furah, vilevile lazima upatwe na hisia kali za kuyatamani yaliyopita. Kwa kizazi cha leo hawawezi kujua lulu ya yaliyo andikwa hapa ila wale wa zamani wanajua. Mambo yanavyoenda sasa hivi katika sekta ya elimu ni tofautu sana. Zamani tulifundishwa mambo ya kizalendo, mtu kujitambua, heshima na kujua kuwa unadeni katika jamii na taifa, lakini leo vitabu vimevurugwa hadi kero. My God ! Watoto wetu nani atawaonesha njia?
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom