Tulipokuwa primary,unakumbuka?

Mnakumbuka masomo tu michezo?
1.BABA NA MAMA.
2.AMSINI PUTUKA.
3.KUCHONGANISHWA ILI MPIGANE (KUPUNJA)
4.KUJIFICHA.
5.JUONGEA KINYUMENYUME.
Yaani ni mingi mpaka basi.
 
Mkuu Kasana umenikumbusha mbali sana maana ishu ya tebo ilikuwa soo hasa pale wale walimu wanoko waliokuwa wanavuka hataile tebo ya 12 na kwenda mpaka ya ishirini, maana tebo ya saba, tisa ni noma sasa huko kwenye 13, 17, 19 je?. Oyaa mnakumbuka sayansi kimu, ile ya kutengeneza maakuli skuli halafu mnapata maksi. Pia kun ishu moja huwa inaniboa nikikumbuka mpaka leo; NAMBA Yaani mtu unawahi shule kinoma ili uwe namba moja. Mnakumbuka tobo bao, usiombe hiyo ichezwe darasani wakati nje mvua inanyesha! Mnakumbuka mtihani wa mwisho wa darasa la saba, pale ambapo mnaanza say na hisabati baada ya hapo mnaenda kucheza mpaka mnajisahau mnakuja kuitwa mtihaniiiiiiiiii!!! mnaenda tena mkimaliza the same. HALAFU MWISHO KABISA MNAVUNJA PENI, KALAMU N.K


Nyambala, bhule bhule?
Umenikumbusha mbali sana na suala la kuhesabu namba asubuhi. Nakumbuka watoto wa walimu waliokuwa wanaishi karibu karibu na shule walikuwa wakija kuwahi namba huku wakiwa na miswaki midomoni, ama wakiwa wamenawa mguu mmoja (passport), halafu wakimaliza kuhesabu namba wanarudi home kwenda kumalizia maandalizi yao.
Halafu wewe uliacha maandishi pale shuleni kuwa "Akumbukwe Nyambala" mara baada ya kuhitimu darasa la saba, uwongo? Yapo mpaka leo, uende ukafute!
(Just a joke)
 
Nikiwa darasa la tano, nilimuandikia barua hii dada Agness, alikuwa mrembo si utani (sijui alipo kwa sasa).

"Kwako dada mpendwa, salamu nyingi sana zikufikie hapo ulipo. Utakapo kujua hali yangu, mimi ni mzima wa afya, hofu ni kwako uliye mbali na upeo wa macho yangu (wakati tupo darasa moja, yeye alikuwa anakaa mbele yangu).
Dhumuni la barua hii ni kukuambia kuwa nakupenda sana, yaani huwa silali kwa kukuwaza wewe. Napenda uwe mpenzi wangu.
Wako mpenzi.......Idimi
(jina langu nalihifadhi kwa sababu za kisiasa)"

Sasa Agnes kumbe ile barua ikawa imemkera sana (nadhani alikuwa bado mtoto kuweza kutambua mambo haya). Si akaifikisha kwa mwalimu Chale (alikuwa mwalimu wa zamu) bila mimi kujua. Ikagongwa kengele,wote tukatoka madarasani. Nilikuwa sijashitukia dili muda huo. Nikaitwa mbele ya hadhara, barua ikasomwa pamoja na sahihi yangu ya majigambo pale chini.
Mnihurumie kwa yaliyonipata, chekeni kwanza kabla sijamalizia!
 
Nikiwa darasa la tano, nilimuandikia barua hii dada Agness, alikuwa mrembo si utani (sijui alipo kwa sasa).

(jina langu nalihifadhi kwa sababu za kisiasa)"

Sasa Agnes kumbe ile barua ikawa imemkera sana (nadhani alikuwa bado mtoto kuweza kutambua mambo haya). Si akaifikisha kwa mwalimu Chale (alikuwa mwalimu wa zamu) bila mimi kujua. Ikagongwa kengele,wote tukatoka madarasani. Nilikuwa sijashitukia dili muda huo. Nikaitwa mbele ya hadhara, barua ikasomwa pamoja na sahihi yangu ya majigambo pale chini.
Mnihurumie kwa yaliyonipata, chekeni kwanza kabla sijamalizia!

Umenikumbusha mbaaaaaaaaali na barua za mapenzi
Tatizo langu lilikuwa kwamba nikiandika barua ya mapenzi sipati mtu wa kumpa (middlegirl/broker), na yule binti niliyekuwa namtaka kusoma ilikuwa shida kidogo. Basi nikawa namfukuza wakati wa mwagano hadi namshika na kumsomea barua niliyomwandikia...kaaazi kweli kweli......mana kabla sijakubaliwa yule binti akawa ame improve kusoma, technically I became a tutor!!!
 
Nikiwa darasa la tano, nilimuandikia barua hii dada Agness, alikuwa mrembo si utani (sijui alipo kwa sasa).

(jina langu nalihifadhi kwa sababu za kisiasa)"

Sasa Agnes kumbe ile barua ikawa imemkera sana (nadhani alikuwa bado mtoto kuweza kutambua mambo haya). Si akaifikisha kwa mwalimu Chale (alikuwa mwalimu wa zamu) bila mimi kujua. Ikagongwa kengele,wote tukatoka madarasani. Nilikuwa sijashitukia dili muda huo. Nikaitwa mbele ya hadhara, barua ikasomwa pamoja na sahihi yangu ya majigambo pale chini.
Mnihurumie kwa yaliyonipata, chekeni kwanza kabla sijamalizia!

Umenikumbusha mbaaaaaaaaali na barua za mapenzi
Tatizo langu lilikuwa kwamba nikiandika barua ya mapenzi sipati mtu wa kumpa (middlegirl/broker), na yule binti niliyekuwa namtaka kusoma ilikuwa shida kidogo. Basi nikawa namfukuza wakati wa mwagano hadi namshika na kumsomea barua niliyomwandikia...kaaazi kweli kweli......mana kabla sijakubaliwa yule binti akawa ame improve kusoma, technically I became a tutor!!!

Ha ha ha hii issue ya kutakana shuleni ilikuwa kiboko. Nakumbuka nilivyokuwa darasa 7, kuna siku mmoja nilimwazima (nilimpatia) binti mmoja, tuliyekuwa tunasoma nae, mkanda wa video wa Home Alone (part 1). Basi yule binti aliporudisha ule mkanda, akapachika, ndani ya kasha, kipande cha karatasi kilichoaandikwa "Nakupenda. Mbona unaninyanyasa mtoto wa watu." Dah ebwanee nasemaje....hiyo line inanikuna mpaka leo hii. Huwaga nasisimuka kila nikiikumbuka yaani.
 
Ha ha ha hii issue ya kutakana shuleni ilikuwa kiboko. Nakumbuka nilivyokuwa darasa 7, kuna siku mmoja nilimwazima (nilimpatia) binti mmoja, tuliyekuwa tunasoma nae, mkanda wa video wa Home Alone (part 1). Basi yule binti aliporudisha ule mkanda, akapachika, ndani ya kasha, kipande cha karatasi kilichoaandikwa "Nakupenda. Mbona unaninyanyasa mtoto wa watu." Dah ebwanee nasemaje....hiyo line inanikuna mpaka leo hii. Huwaga nasisimuka kila nikiikumbuka yaani.

heheheh, wewe babu ulisoma wakati wa raha basi, wakati wadada tayari wameshageuka kuwa ndio wasakaji.

Enzi zetu ilikuwa noma!! kama umemkosa shule lazima ukakatanaye kuni bila hata ya kutumwa na wazazi wako. Ukijuwa katumwa sokoni na wewe chap chap unamuuliza maza wako kama anamahitaji yeyote sokoni.

Ila kunasiku nilitenda dhambi,,,,nilikatongoza ka classmate kangu kalivyokuwa kanatoka sokoni kununua karanga za tui. Duh, kwanza kalianza kuchora-chora chini, somo lilipo kolea kakaanza kutafuna karanga za tui moja hadi nyingine. Masikini sijui alisema nini kwa wazazi aliporudi bila karanga!!!
 
Washikaji, hiyo yote tisa, Mnakumbuka tulikuwa tunaenda shule peku peku, halafu baridi la Asubuhi si mchezo. wakati mwingine njiani kulikuwa na nyasi kibao kabla mazingira yetu hayajaharibiwa, basi ukitembea inabidi upige mahesabu maana umande ulikuwa wa baridi ukizingatia hata viatu hujavaa.

Halafu ingine ni ile nyumbani hakuna pasi, au kwa sababu ya michezo mingi unachelewa kunyoosha nguo, sasa kulikuwa na technolojia ya asili. unakunja vizuri uniform zako unazitandika chini ya shuka halafu unazilalia juu, Asubuhi ukiamka si mchezo panga zimesimama kiroho mbaya.
 
Washikaji, hiyo yote tisa, Mnakumbuka tulikuwa tunaenda shule peku peku, halafu baridi la Asubuhi si mchezo. wakati mwingine njiani kulikuwa na nyasi kibao kabla mazingira yetu hayajaharibiwa, basi ukitembea inabidi upige mahesabu maana umande ulikuwa wa baridi ukizingatia hata viatu hujavaa.

Halafu ingine ni ile nyumbani hakuna pasi, au kwa sababu ya michezo mingi unachelewa kunyoosha nguo, sasa kulikuwa na technolojia ya asili. unakunja vizuri uniform zako unazitandika chini ya shuka halafu unazilalia juu, Asubuhi ukiamka si mchezo panga zimesimama kiroho mbaya.

Hii kiboko!
Ndg Sahara, hii mbinu imeniacha hoi sana. Nadhani hii ilikuwa kabla ya asi za mkaa ama sio?
 
hapa ni burudani tupu,nimecheka sana

IDIMI hizo zilikuwa za wasichana wengi,

HOME familia yetu ilikuwa 'very extended' tulikuwa kama saba hivi tunaosoma shule ya msingi, si unajua mtoto wa mjomba, shangazi n.k
Kwa kawaida tulikuwa tunapair moja moja ya uniform, unaanza nayo hiyo darasa la kwanza hadi la tano, labda itokee hapo katikati mwenzako kamaliza shule utabahatika kukusanya mabaki yake.

Ilikuwa kazi asubuhi unapoamka na kukuta ama shati au kiatu au kaputura/sketi saa nyingine madaftari mwenzako kakufichia. hapo ilikuwa noma....
 
Mnakumbuka pale ambapo shule inafungua jtatu halafu a day before ndiyo unaanza kutafuta uniform, daftari n.k?
 
Hivi mnakumbuka kwamba wanafunzi wengi ilikuwa wanaenda shule pekupeku?? na wakti wa mapumziko kwenye mpira jamaa watakataa usicheze mpaka uvue "mdundo" viatu vyako........enzi hizo safari buti na viatu flani hivi vya bora vyeusi kwa mbele vipana tulikuwa tunaviita "vita," na raba flani hivi za canvas watoto wanafua na kupaka chaki ili viendelee kuwa vyeupe ndio vilikuwa vinatamba. Kenya wenzetu bado wana safari buti sisi mmmmmmmmmh, tena sidhani hata Bora shoe company ime survive wimbi hili la "ukimwi" wa maendeleo!!!.
 
Mkuu IDIMI umeniacha hoi sana juu ya kupiga machata "AKUMBUKWE........." Anyways mnayakumbuka mafuta ya kupaka yaani RAYS na SHANTI? kungfu shoes na asante salim (soili lainiiiii!!!!!)
 
Hivi mnakumbuka kwamba wanafunzi wengi ilikuwa wanaenda shule pekupeku?? na wakti wa mapumziko kwenye mpira jamaa watakataa usicheze mpaka uvue "mdundo" viatu vyako........enzi hizo safari buti na viatu flani hivi vya bora vyeusi kwa mbele vipana tulikuwa tunaviita "vita," na raba flani hivi za canvas watoto wanafua na kupaka chaki ili viendelee kuwa vyeupe ndio vilikuwa vinatamba. Kenya wenzetu bado wana safari buti sisi mmmmmmmmmh, tena sidhani hata Bora shoe company ime survive wimbi hili la "ukimwi" wa maendeleo!!!.

YNIM
Du aisee hizi safari buti zilikuwa safi sana. Nakumbuka zilikuwa haziishagi. Pamoja na kuzipigia madochi sana kwenye soccer. basi unakuta enzi zile mzazi anakuchunia kukununulia viatu vingine mpaka ulivyokuwa navyo viishe au mguu ukue. Sasa kwa wale wakina andunje kama mimi, tulijikuta tunavaa safari buti mmoja kuanzia darasa la 5 mpaka la 7. Nakumbuka za kwangu ilibidi nizichanje wembe, vinginevyo ningeingia level ya unjuka nimevitinga. Mguu uligoma kukua kabisa!
 
YNIM
Du aisee hizi safari buti zilikuwa safi sana. Nakumbuka zilikuwa haziishagi. Pamoja na kuzipigia madochi sana kwenye soccer. basi unakuta enzi zile mzazi anakuchunia kukununulia viatu vingine mpaka ulivyokuwa navyo viishe au mguu ukue. Sasa kwa wale wakina andunje kama mimi, tulijikuta tunavaa safari buti mmoja kuanzia darasa la 5 mpaka la 7. Nakumbuka za kwangu ilibidi nizichanje wembe, vinginevyo ningeingia level ya unjuka nimevitinga. Mguu uligoma kukua kabisa!

Haha mzee umenivunja mbavu na hii staili ya kuvichanja wembe viatu ili ununuliwe vipya.

wazee mbona hamjagusia enzi hizo ukitaka kuanza darasa la kwanza lazima uuvushe mkono kwenye kichwa ushike sikio la upande wa pili, ukishindwa tu,ujue wewe unarudia vidudu. hahaha!
 
wazee mbona hamjagusia enzi hizo ukitaka kuanza darasa la kwanza lazima uuvushe mkono kwenye kichwa ushike sikio la upande wa pili, ukishindwa tu,ujue wewe unarudia vidudu. hahaha!

Gamba la nyoka, hili umenikumbusha mkuu, mimi nilikuwa mwathilika mkuu, miaka miwili kila nikienda mkono haufiki narudishwa home, mara ya tatu sikukubali. niligoma kurudi nyumbani mpaka kikaeleweka. ulikuwa mtindo mbaya kweli ule. halafu mnakumbuka pia kuwa tulikuwa hatuvai chupi? hiyo hiyo kaptula ndiyo chupi hiyo hiyo. saa ukisahau kufunga vifungo ndo umeadhirika shule nzima watajua.
 
Hii kiboko!
Ndg Sahara, hii mbinu imeniacha hoi sana. Nadhani hii ilikuwa kabla ya asi za mkaa ama sio?


IDIMI, naweza kukuhakikishia kuwa hii method ilikuwa kali sana kwa sababu kwanz ahuhitaji kuhangaika na pasi ya mkaa, pili ni kuwa nguo zinakuwa na panga kali ile mbaya, kumbuka ishu ilikuwa upanga kuonekana apo!
 
Duh, kweli tunatoka mbali.

Nyambala,
Hivi yale mafuta uliyotaja hapo juu "Rays" na "Shanti" bado yapo? Nimecheka sana.
Jamani msisahau kuwa enzi za Waziri mkuu Sokoine watu tulivaa mashati yenye rangi za mawingu! Sijajua yalikuw yanazalishwa wapi, ila nina uhakika ilikuwa ni Tanzania hapa hapa..

Nani alikuwa Kaka Mkuu kama mimi hapa JF? Naoma tubadilishane uzoefu. Mimi nilikuwa kaka mkuu nikiwa darasa la sita.
 
Nani alikuwa Kaka Mkuu kama mimi hapa JF? Naoma tubadilishane uzoefu. Mimi nilikuwa kaka mkuu nikiwa darasa la sita.
Duh mzee kumbe umewahi kuwa mnene, mimi nilikuwa Monita, tena monita mwenyewe monita wa Msitari,darasa letu lilikuwa na Mistari minne kila msitari na monita wake, sasa mimi msitari wangu ulikuwa na wasichana wazuri kweli(kwa mujibu wetu wakati huo). sasa kuna kabinti kamoja nilikuwa nakazimia kichizi, kenyewe kalikuwa kanakaa siti ya mbele karibu na ubao,mimi nilikuwa nakaa nyuma kabisa
sasa unakuta wakati mwingine nakuwa nataka tu nikaonepo sura yake, basi hapo nitakapigisha magoti mbele kwa kisingizio kwamba kanaongea darasani ili japo tu nipate wasaa wa kukaona sura yake nzuri.dah nikikumbuka mzee nachoka ile mbaya.
 
I like this thread very much kwa sababu inanikumbusha mbali sana yaani nikianza kuzisoma hizi post nacheka sana.

Mimi nimekuwa monitor kuanzia darasa la tano, darasa la sita nikawa kilanja na umonitor ukaendelea. Darsa la saba nikawa Dada Mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom