Tuliowai kupata Supplemental kwenye final exam za UE/IE tukutane hapa

Supp haina huruma aise nilipokua chuo tokea nianze mpaka namaliza nilipata SUPP moja ya Economics ilikua ivi

tulikua na madame m moja anatufundisha Economics alikua mpole, sio muongeaji, mtaratibu, anafundisha vizuri, yani wakati wa kipindi chake ukijisikia huendi ukitaka unaenda yani haangaiki na mtu, kitim tim kilianza pepar ya test alituletea test ya economics rahis economics ya Advance 5&6 tulipata 90, 96, 84 zilikua za kutosha yani Coz work nilikua nayo ya 34 out of 40 sasa kimbembe ilikua final exam tulijua tena final mteremko yani economics tukaipuuzia tukajua ni inakuja rahisi kama ya test, dhuu!! Siku ya final ya economics nafungua mtihani duu sijawah jua kama kwenye economics kuna topics zile mtihan ulikua una maswali 5 kila swali 20mrks, nilijubu swali moja tu nilikua na huakina nalo, matokeo yanatoka na supp ya economics dhaa nilipata uzuni nikalipa 20,000 ya kurudia supp nilisoma kila kitu Nikachomoa iyo supp..
Mpaka sasa sipuuziagi kitu kila kitu nakichukulia uzito haya mambo ya mzaa sio mazuri aise.
kwa walio wahi kupata supp kama mm ya kwako ilikuaje??? Na ilikua ya nini???
Hivi sis wenye vidiploma tunacoment wapi?
 
Duh hatar sana... Modules 12 si mchezo...mm chuon kwetu pia modules nyingi ni 6 na kuna baadh ya semister unakuta una modules 5
Asee watu mmesoma kwa raha yaan semister 1 masomo 6?? Sie semister ikiwa na masomo machache ni 9 tena hio semister inakuwa ya bata hatari bt mostly semister ilikuwa na modules 12 mpka 13 so kwa mwaka ni modules 24 &26 kwhyo kukuta watu wana sup zaidi ya 10 ilokuwa kawaida sana... shkamoo wana DIT alumn
 
Yaan ambao hamjawah pata sup hongeren sup zinatesa aisee...mwaka wa mwisho semister ya mwisho UE financial management sup hyo ikabid nirud hapo nshaenda mkoan yaan roho iliniuma stak kukumbuka...nashukuru Mungu nilichomoka
 
nadhani haujamwelewa anachomaanisha.

yaani mtihani wa UE una marks 100. maswali 5@20 marks.

yeye alikuwa anajua moja tu la marks 20.

tukisema alipata hilo tu lote ana 20

20 x 0.6 = 12

jumlisha na CW 34

34+12= 46

na hapo inawezekana hilo swali la marks 20 hakupata lote
Ultimate au nakosea
Nime kusoma mkuu
 
first year niliteleza tu,,, second year nikapata sup ya principle na technique za wlm third year nikapata brobation somo la yule principle wa Mweka kwa sasa lastly nikavaa joho na saizi nipo kitaani nakomaa
 
Haaaaa wazee Wa COET
wale wa UDSM COET sitamsahau Prof Chambega second year ile shule ilijua kuninyoosha hakuna pakushika miti yoote inateleza first year gpa ya 4 second year gpa 2.8 na sup juu nilinyooka aisee....Chambega popote ulipo mzee wa Electrical analysis shkaoooo
 
Back
Top Bottom