Tuliowahi kuwashuhudia wachawi na kuzungumza nao LIVE tukutane hapa...

Fohadi

JF-Expert Member
Jul 24, 2020
770
2,406
Mwaka 2006 hadi 2011 ni kipindi ambacho kama familia hatukuwahi kuwa na furaha ya kudumu. Dada yetu ambae ndie first born wa familia alikuwa anaumwa ugonjwa ambao haukuwa wa kawaida. Familia ilijitahidi kumtafutia tiba, pesa nyingi zilitumika na pengine matatizo ya dada ndiyo yaliyofanya familia yetu ikawa nyuma kimaendeleo kwani gharama nyingi sana sana zilitumika.

Katika kuhangaika huku na huku, familia ilifanikiwa kukutana na 'mtaalamu' mmoja wa jadi. Na katika harakati zake za kimatibabu, ilibidi kwa kutumia ujuzi wake aweze kuwaita wachawi ili wapate kuzungumza na baadhi ya member wa familia ili kujua tatizo ni nini na kwanini wameiandama sana familia yetu. Siku ya siku ikafika, kikao kikapangwa kufanyika usiku eneo la nje kidogo na nyumbani.

Nakumbuka kipindi hicho mzee alikuwa amesafiri nje ya mkoa. Hivyo mimi nikiwa kama mtoto wa kwanza wa kiume katika familia pamoja na Mama ndio tuliotakiwa kushiriki kwenye hicho kikao. Sikuwa na hofu wala kidogo maana kwa miaka 4 tayari mauza uza ya nguvu za giza nilikuwa 'nimeyazoea'. Na kweli, usiku ulifika, nikiwa mimi, mama yangu, mtalaamu wa jadi na watu wengine wawili tulikuwa tayari kwa kikao kile dhidi ya wachawi wale ambao wangeingia mda wowote. Tulipakwa dawa fulani usoni na kusubiri kikao.

Mtaalamu alianza kufanya yake na kuanza kuwaita wale wachawi na mara ghafla tukiwa tumekaa ndani ya hiyo nyumba ambapo kikao kilipangwa kufanyikia, waliingia watu watatu wakiwa kama walivyozaliwa wakiwa wamejipaka dawa nyeupe usoni.

Nakumbuka alikuwa Mwanamme mmoja mzee mnene ambae ndie alikuwa kiongozi wao na wanawake wawili wenye umri wa kama miaka 40's. Wale jamaa walikuwa wakali sana kwanini wameitwa. Mama yangu alikuwa anatetemeka kupita kiasi. Mmoja kati ya wale watu tuliokuwa nao alikuwa analia na wale wachawi walimkanya anyamaze mara moja.

Hakika ulikuwa ni usiku wa kutisha sana, wachawi waliokuja walikuwa watatu na walidai kuwa mshirika mwenzao ambae ndie mtesi wa familia yetu alikuwepo pale nje amekuja ila hakutaka kuingia ndani. Kikao kilichukua kama dakika 20 hivi na wale jamaa wakaomba kuondoka, hawana muda wa kupoteza wanawahi kuendelea na ratiba zao zingine usiku ule.

Sitasahau usiku ule, dunia imejaa watu makatili sana. Hatuna budi kumshukuru Mungu kama familia zetu zina furaha na amani. Binafsi namshukuru sana Mungu kwani mambo mengi leo yamebaki historia.​
 
Poleni sana

Hujatuambia sista yako alipona au ilikuwaje
Asante sana Mkuu...Yule ndiye alikuwa mtaalamu wa mwisho kumtibu sista.

Namshukuru sana Mungu. Ni miaka 10 sasa imepita sister yuko fresh na alipona tatizo lake..Angalau sasa 99% ya zile nyakati ngumu sana katika familia zimebaki historia. Sio mimi wala ndugu zangu ambao wanapenda kukumbuka changamoto za kipindi kile.
 
Zamani nikiwa mdogo niliwahi kuwaona wachawi. Kuna vijiji vya ndani ndani huko Tanganyika vina wachawi mno aisee!

Ndio maana huwa sibishi sana nikielezwa kuhusu wachawi maana naamini wapo!
 
Umeandika ujinga wa kitoto sana, hata kama uchawi upo ila huo wa kujipaka masizi ni FUTUHI tu.
Ndiyo mkuu, naheshimu mtazamo wako na pengine nimeandika ujinga sana sana..Lakini nitakuwa mjinga sana kama nikiwa na akili zangu timamu nimeandika hii story hapa ili kufurahisha jukwaa tena nikiihusisha na familia yangu.

Kwako wewe itaonekana ni ujinga, sikulaumu maana labda hujawahi kuupitia upande wapili wa shilingi. Ila trust me, hii nguvu ya giza inawatesa wengi sana sana sana. Kitu pekee ninachoweza kukushauri ni kuzidi kuijenga imani yako juu ya Mungu.
 
Sasa walisemaje..umeongea vitu visivyo na mashiko... vyote hivyo tunajua kuwa wachawi wapo uchi
 
sasa walisemaje..umeongea vitu visivyo na mashiko... vyote hivyo tunajua kuwa wachawi wapo uchi
Mkuu..Pengine yale waliyosema nikiyaweka hapa ndio yataonekana hayana mashiko zaidi na hutaamini... Na yote kwasababu hujawahi kuuishi huu upande..Tujenge nchi mkuu.
 
Zamani nikiwa mdogo niliwahi kuwaona wachawi. Kuna vijiji vya ndani ndani huko Tanganyika vina wachawi mno aisee!

Ndio maana huwa sibishi sana nikielezwa kuhusu wachawi maana naamini wapo!
Mkuu...kabla ya 2006 nilikuwa naona mambo yote kama muvi za kinaijeria.. Ila baada ya yale yaliyotokea nimekuwa sibishi nikisikia story za watu.

Uchawi upo sana sana, ila kikubwa ni kutokuuweka akilini na kuutegemea au kuufanya ndio chanzo cha kila tatizo.

Watu wengi kulingana na historia zao wamekuwa affected sana na ushirikina psychologically kiasi kwamba chochote wanachokiona wanakihusanisha na uchawi. Mfano mtu anaweza ona kuku anamuangalia tayari anasema kuna mkono wa mtu au mwingine tu anajenga ukuta unaanguka analaumu ni uchawi.

Mtu anaweza wahukumu hawa watu bila kujua kuwa tayari wamekuwa affected na historia zao. So, ukishindwa kujicontrol ndo unaishia kuwa addicted kitu ambaco ni kibaya zaidi. Hili tatizo lipo ila Mungu ndie mwenye nguvu zaidi katika kulitatua.
 
๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น๐Ÿ‘บ๐Ÿ‘น
 
9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom