BilioneaPATIGOO
JF-Expert Member
- Jun 23, 2012
- 12,321
- 11,315
Alikua shetani lucifer huyo ..2015 Natoka makaburini kumzika Baba Yangu Mzazi. Nipo nyuma ya nyumba nimejiinamia nikilia kwa kumpoteza Baba. Mlio wa kunijulisha kuwa kuna Sms Inaingia nikausikia. Lakini kwa kuwa sikujisikia kusoma kutokana na kilio nikaona nitausoma baadae. Baada ya kulia kwa muda mrefu sana baadae nikanyamaza na kuona kuwa napaswa kuwa mwanaume. Ndipo nilipoamua kuufungua Ujumbe. "IT'S OVER". kwanza niliganda kwa Muda Nikijiuliza nilichomkosea. Nikaamua kumpigia kuuliza tatizo na kosa langu. "Hujui kuachwa? Lilikuwa swali kisha akakata simu. Mpaka leo silijui kosa langu