kimsboy
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 8,991
- 17,888
Tuliowahi kupitia jandoni, tohara, mafunzo na changamoto zake tukumbushane enzi zako unakumbuka nini?
Mimi ni mmoja wa vijana tulipotia jandoni nakumbuka enzi hizo Kilimanjaro hususan sisi Wachaga tulikua na utamaduni huu sana wa vijana kwenda jandoni
Utaratibu ulikua ni kila kijana akipata tohara basi ule mwezi mmoja au zaidi anaokua yupo ndani basi anafundishwa mambo kadhaa kuhusu yeye na kujitambua, elimu ya uzazi, heshima na utiifu.
Kwa Wachaga majando yalijengwa migombani au maporini, ambapo migombani, majani ya migomba maturubai na matawi ya miti yalitumika kutengeneza jando la vijana na chini walilalia majani ya migomba yalotandazwa chini na ikiwa wanahitaji godoro wanaweza wakaweka na godoro juu
Huu utamaduni bado upo
Maandalizi yalikua kama ifuatavyo:---
NAENDELEA
Maandalizi ya ujenzi wa jando yalifanyika siku moja kabla ya vijana hawajapata hiyo tohara
Kisha wakishajenga jando, sasa wataitwa wataalam wa tohara ambapo Mzee wa hiyo kazi atakuja au hata daktari atakuja atawafanyia vijana tohara na akishakamilisha basi huko nje shangwe na vigelegele husikika ambapo Wazazi wanafurahia mwanao kupata tohara na kuona sasa kijana wao sasa kakua
Na mara nyingi sana ilikua ni vijana kuanzia miaka 8 mpaka 18
Na rika zuri ilikua ni wale waliotimiza miaka 10 hadi 18 hapa ndo walikua wanapewa mafunzo vizuri kabisa
Na ilikua ni kila jando wanafanyiwa vijana zaidi ya wawili na mara nyingi wanakua ni vijana wawili ambapo kitendo cha kufanyiwa tohara pamoja kinahesabika kuwa ni undugu wa damu mshaunganisha na hapo ni urafiki na udugu hadi kifo inakua tayari ni mtu na patner wake (ukhoo) kwa kichaga
Huyu anakua ni ndugu yangu kabisa maana kitendo cha kufabyiwa tohara pamoja naye inaonekana ni kana kwamba mmechanganya damu na tayari huo ni urafiki w maisha kwa shida na raha
Nitarudi kuendelea kuelezea sasa wanachofundishwa ninini haswa,vyakula, kukabidhiwa fimbo,siku ya jungu, kuoga mtoni,kuchoma jando etc na siku ya kutoka,na pia suala la wanawake kutoruhusiwa kwenda kwenye majando ya wanaume
Mimi ni mmoja wa vijana tulipotia jandoni nakumbuka enzi hizo Kilimanjaro hususan sisi Wachaga tulikua na utamaduni huu sana wa vijana kwenda jandoni
Utaratibu ulikua ni kila kijana akipata tohara basi ule mwezi mmoja au zaidi anaokua yupo ndani basi anafundishwa mambo kadhaa kuhusu yeye na kujitambua, elimu ya uzazi, heshima na utiifu.
Kwa Wachaga majando yalijengwa migombani au maporini, ambapo migombani, majani ya migomba maturubai na matawi ya miti yalitumika kutengeneza jando la vijana na chini walilalia majani ya migomba yalotandazwa chini na ikiwa wanahitaji godoro wanaweza wakaweka na godoro juu
Huu utamaduni bado upo
Maandalizi yalikua kama ifuatavyo:---
NAENDELEA
Maandalizi ya ujenzi wa jando yalifanyika siku moja kabla ya vijana hawajapata hiyo tohara
Kisha wakishajenga jando, sasa wataitwa wataalam wa tohara ambapo Mzee wa hiyo kazi atakuja au hata daktari atakuja atawafanyia vijana tohara na akishakamilisha basi huko nje shangwe na vigelegele husikika ambapo Wazazi wanafurahia mwanao kupata tohara na kuona sasa kijana wao sasa kakua
Na mara nyingi sana ilikua ni vijana kuanzia miaka 8 mpaka 18
Na rika zuri ilikua ni wale waliotimiza miaka 10 hadi 18 hapa ndo walikua wanapewa mafunzo vizuri kabisa
Na ilikua ni kila jando wanafanyiwa vijana zaidi ya wawili na mara nyingi wanakua ni vijana wawili ambapo kitendo cha kufanyiwa tohara pamoja kinahesabika kuwa ni undugu wa damu mshaunganisha na hapo ni urafiki na udugu hadi kifo inakua tayari ni mtu na patner wake (ukhoo) kwa kichaga
Huyu anakua ni ndugu yangu kabisa maana kitendo cha kufabyiwa tohara pamoja naye inaonekana ni kana kwamba mmechanganya damu na tayari huo ni urafiki w maisha kwa shida na raha
Nitarudi kuendelea kuelezea sasa wanachofundishwa ninini haswa,vyakula, kukabidhiwa fimbo,siku ya jungu, kuoga mtoni,kuchoma jando etc na siku ya kutoka,na pia suala la wanawake kutoruhusiwa kwenda kwenye majando ya wanaume