Tuliowahi kupata pesa na kufilisika/kufulia, tujikumbushe hapa

666 chata

JF-Expert Member
Mar 14, 2013
1,688
3,815
Nikiwa nimemaliza chuo sina hili wala lile, niko kitaa nikijipanga, nikachangiwa na ndugu zangu mtaji wa milion 4 point something huko, niende nikafanye biashara ya mchele toka Moro vijijini kuleta mijini na kusambaza kwa bei ya jumla.

Biashara mwanzo ilienda vizuri, mwisho wateja wangu wa siku zote wakawa wakopaji wangu wakubwa, malipo yakawa ya kuzungushana, nikawa mkali kidogo ila kwa bahati mbaya pesa ikawa ndogo kwenye mzunguko wangu, sinunui tena zile kilo nilizoanza nazo kwa wakati, mambo yakawa tofauti kidogo, nikaenda weee.

Mwisho wa siku nikachanganyiwa mchele kipuuzi kabisa na mtu ambae nilikua namuamini, nikajikuta nipo na mchele wa vitumbua na jamaa yule kakimbia, hapo ndio ukawa mwisho wangu, nilifilisika kama kuku, ndugu zangu hawakunielewa tena, nilipata stress kama tani 7 hivi.

Wakati tena nikapataga milion 3 kwa enzi zile haikua haba aisee, nikawa naishi vizuri tu, hizo elf 10 kwangu zilikua buku, sina cha kujibania kwa kweli, kuja kustuka nimenunua friji na tv tu vya geto tena ka friji kale kadogoo kabisaa, hela yotee imeisha katika njia zisizoeleweka, nilichanganyikiwa tena, sina nidhamu ya fedha.

Mwisho nikarudi zangu kusoma tena chuo ndio nikaja kutoboa kwa njia zingine kabisa kwa kutumia kazi niliyosomea.

Je, wewe unakumbuka vipi? Nini kilikupata?
 
Nilipewaga dola 100 zamani sana na danga limoja hivi aiseee kwa kipindi kile ilikuwa hela nzuri nikaja nikaila bila kuelewa imepita wap

Nikaja kupewa tena mil 1 na hilo hilo danga zamani kidogo nayo haikufanya la maana

Nikaja nikapata danga lingine likanipa m2 nazo nimefanyia kazi haikuzaaa

Tangu wakati huo miaka imepita sitaki tena hela za madanga, nimeolewa na ninatafuta hela kihalali.

Msiwashangae kina Wema hela za kudanga hata upewe bil 1 huwa zinayeyuka.
 
Niliwahi kuzichanga huko nyuma, nikafungua grocery! Kwa kuwa nami nilikuwa mwanachama, mwanzoni nilikuwa na wateja wazuri na waaminifu. Baada ya muda mikopo ikaanza. Mteja akikopa na deni likiwa kubwa, anahama kijiwe.

Nakumbuka mara ya mwisho nilifungia crate tupu kwani hata chupa walishakopa zikiwa na pombe ndani. My Take: Biashara ya pombe kama na wewe mmiliki ni mnywaji, usinywee pale, ni hatari kwa usalama wa grocery yako.
 
Niliwahi kuzichanga huko nyuma, nikafungua grocery! Kwa kuwa nami nilikuwa mwanachama, mwanzoni nilikuwa na wateja wazuri na waaminifu. Baada ya muda mikopo ikaanza. Mteja akikopa na deni likiwa kubwa, anahama kijiwe. Nakumbuka mara ya mwisho nilifungia crate tupu kwani hata chupa walishakopa zikiwa na pombe ndani. My Take: Biashara ya pombe kama na wewe mmiliki ni mnywaji, usinywee pale, ni hatari kwa usalama wa grocery yako.
Hahahahaahahah mkuu umenichekesha sanaaa.
 
184 Reactions
Reply
Back
Top Bottom