Tuliowahi kupata ajali na kunusurika tukutane hapa

MBITIYAZA

JF-Expert Member
Jan 22, 2017
14,950
26,049
Mpaka leo huwa naikumbuka Jumamosi ile niliopata ajali.Kiufupi nilipanda pikipiki bahati mbaya hakuwa ameiwasha na tuko kwenye mteremko mkali,dereva nikamuuliza nini hiyo maana nilisikia ilivyokata break hakunijibu. Pikipiki ilikuwa kwenye mwendo balaa,baada ya dk kama 2 dereva akaanza kupiga kelele sister tunakufaaa pale ndio aliponitisha zaidi pikipiki ilikosa direction ikawa ninachira zigzag,barabara ni very rough imechimba kabisa mifereji ktktk kwasababu ya mvua za mwaka huu(nadhani haikuwa dalili njema kwa wizara ya madini (makinikia).

Niliangalia
mwisho wa barabara kuna miti minene imepanda kimkingamo,ilikuwa tuivae bila ubishi nikaamua kuruka nijiokoe tu,hasa nilipowakumbuka wanangu bado wadogo nikachukua maamuzi ya kuruka,the rest nilijikuta hospitali mwili wote una damu hasa usoni.

Imagine nikaja kushonwa saa7 usiki toka 8:33 nilipoanguka.Daktari aliniambia yaani wewe kuruka ndo imekuwa pona yako ile miti ulikuwa unaenda kuivaa., mawili mimi wa nyuma kuangukia mgongo na kuvunjika mgongo au kufariki maana miti ilikuwa imebabana asingeweza ikwepa.

Nashukuru sikuvunjika na ruka yangu ndo ikawa pona yangu,na nikamsaidia dreva nae aanguke mbele yangu,nae aliumia ila sio sana.

Je, wewe uliewahi kupata ajali huwa unaiongeleaje?

Poleni wote mliowahi kuajalika na kupata ulemavu na kupoteza ndugu, mimi niliponea chupuchupu ila ningeganda kusubiri miujiza walah hata ishu ya MAKINIKIA nisingeijua wala madini ya TL nisingeyasikia.

My take madereva kuweni makini
Thanks GOD
 
Dah una mbwembwe sana kijana. Mimi nilipata ajali mpaka leo nina kumbukumbu ya chuma mkono wa kushoto.
tmp_525-Screenshot_20170616-223225-552347900.jpg
tmp_525-Screenshot_20170616-223055-287438203.jpg
 
Nakumbuka miaka ya 2005 natokea babati naenda tarangire nilikuwa nimelewa sana nasukuma PUMA TD6 mvua ya hatar kuna vikona havieleweki hapo kati wanapaita kona S hahahah nikakutana na nusu mkate ka RAJU wahind flan waliokuwa na magari ya usafir babati, Jamaa akanibana kaganda katikati ya bara bara mbuuuuuula nakujakustuka naona naserereka pombe ikakata kwa muda mungu bariki tuligonga ngema ila Raju bofla kalianguka kabisa,
Ila sikomi napiga pombe na kuendesha ila tokea ile ajali nimekuwa makini sana nikilewa hata vipi wewe niweke tu kwenye staring nafika kabisa sema kushuka ndio kitendawili sasa
 
Tarehe 1/7
tabora hapa nipo napikipiki nazndesha mwenyewe mwendo wakawaida kabisa kutahamaki jiwe kubwa mbele yangu hapa na hapo aiseee nilitahamaki tu ...
Sikuelewa kilichoendelea nazinduka nipo home watu walenijalia nimeshonwa usoni nilipokuwa nimepasuka pia kuwekwa ma bandage kibao meno lawili yamekatika majeraha kibao.nastuka naqhangaa what happened wananipa uji nilishapigwa masindano ya hatari....
Ila sasa naendelea vizuri namshukulu mungu maana nilinusulika.....
Ajali sio mchezo
 
Tarehe 1/7
tabora hapa nipo napikipiki nazndesha mwenyewe mwendo wakawaida kabisa kutahamaki jiwe kubwa mbele yangu hapa na hapo aiseee nilitahamaki tu ...
Sikuelewa kilichoendelea nazinduka nipo home watu walenijalia nimeshonwa usoni nilipokuwa nimepasuka pia kuwekwa ma bandage kibao meno lawili yamekatika majeraha kibao.nastuka naqhangaa what happened wananipa uji nilishapigwa masindano ya hatari....
Ila sasa naendelea vizuri namshukulu mungu maana nilinusulika.....
Ajali sio mchezo

mie nilijisemea bora udead mazima kuliko kusikilizia yale maumiv aic,pole
l
 
Nakumbuka mwaka 2005 mwezi wa 10 nilikuwa nakatisha main road ya shy to mwz ilikuja mark two speed nakuigonga baiskeli yangu na kurushwa kwenye bonge la mtaro. Na mimi nikatoka nimesimama watu hawakuamini kama niliyegongwa nilikuwa mimi maana sikuumia hata kidogo watu wakaniambia nikachinje kuku nile peke yangu nabahati sana.
 
Nakumbuka mwaka 2005 mwezi wa 10 nilikuwa nakatisha main road ya shy to mwz ilikuja mark two speed nakuigonga baiskeli yangu na kurushwa kwenye bonge la mtaro. Na mimi nikatoka nimesimama watu hawakuamini kama niliyegongwa nilikuwa mimi maana sikuumia hata kidogo watu wakaniambia nikachinje kuku nile peke yangu nabahati sana.



hahahh mganga wako first class aic
 
2013,nlipata ajali mbili ndani ya week moja.kwanza,ilikuwa kigogo darajani,ule mteremko niko kwenye daladala fuso imetuvaa kwa nyuma.nilikuwa nyuma ya gari (dcm),nilikuja kujikuta pale mlangoni nimepiga magoti.hiyo jmos, alhamis natoka gairo naenda kondoa niko kwenye jm coach tumefika eneo moja inaitwa kelema usiku gari mbovu ikakata break mteremkoni.asee!!!watu wazima wanalia vibaya sana na sala juu.aliyekuwa kakaa mbele kakimbilia nyuma dereva kabaki na mzee mmoja hivi akimpa ujasiri,maana hapa dereva alishafungua mlango aruke.mbaya mbele kuna daraja jembamba na korongo kuubwa.nashukuru Mungu nilikuwa na utulivu wa ajabu siku ile yani nilikamata siti kwa umakini huku nikitazama kwa mbele tunakoelekea.kwa spidi ile alishindwa kulenga daraja vizuri gari ikajibamiza upande mmoja.ilitoa frem na vioo vyote upande wa dereva mpk nyuma.bahati nzuri ilisimama salama. hiyo ni saa nne usiku.r.i.p dada mmoja alikuwa mke wa tajiri mmoja wa pale kondoa,km sikosei anaitwa abdul mapesa.na majeruhi kadhaa.nilishuka kwenye gari mikono inatetemeka.
 
mwaka 2013 wa 10, nikiwa ktk bac la kopa belt lnalotoka zambia to dar, maeneo ya lwanda mkoan mbeya 2lgongwa na roli la mizgo, nashukr mungu nltoka salama salmin
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom