Njemba Soro.
JF-Expert Member
- Oct 5, 2013
- 3,246
- 5,756
Salaam.
Huku mitaani kuna vichaa na kuna wanaoigiza ukichaa. Hapa ni matukio kadhaa niliwahi kukutana nayo dhidi ya vichaa.
1. Hili lilitokea soko la Mbuyuni Moshi. Asubuhi na mapema nimeshusha mzigo wa malimao debe tano, zile debe nne nikauza kwa bei ya jumla halafu moja nikapanga sehemu nikawa nauza kwa mafungu. Mara akatokea mshikaji anajifanya dishi limeyumba, ana mfuko wa rambo akachukua malimao mafungu saba halafu akanipiga kibao huku ananitolea macho. Nilimpiga ngumi za uso kama tano, jamaa dishi likaa sawa akaacha rambo akaondoka kwa kasi ya ajabu. Baadaye tukagundua anajifanya chizi akichukua vitu anapeleka kwenye hotel fulani hivi anauza.
2. Mwenge Dar es Salaam.... nilishuka kwenye daladala ya Mbagala nikawa nawahi ya Tegeta kipindi hicho foleni ni kubwa sana na magari ni machache. Wakati nagombea gari nikahisi mkono mfukoni nikaudakia hukuhuku mfukoni halafu nikamvuta jamaa pembeni. Akaanza kuniigizia kama vile dishi limeyumba, bila kumuuliza chochote nilimpiga ngumi mbili tu jamaa akazimia, wale wapigadebe wa Mwenge wakaja kumsaidia nikaondoka. Kesho yake napita pale namuona jamaa ni mzima kabisa kumbe siyo kichaa.
3. Watu wa Mbuyuni Moshi, kuna jamaa miaka ya 2006 alikuwa anavaa vyuma mwili mzima hadi kwenye nywele, hivi yupo bado? Yule ndio kichaa aliyewahi kuninyang'anya Tsh. 2000 halafu akaondoka kibabe
Huku mitaani kuna vichaa na kuna wanaoigiza ukichaa. Hapa ni matukio kadhaa niliwahi kukutana nayo dhidi ya vichaa.
1. Hili lilitokea soko la Mbuyuni Moshi. Asubuhi na mapema nimeshusha mzigo wa malimao debe tano, zile debe nne nikauza kwa bei ya jumla halafu moja nikapanga sehemu nikawa nauza kwa mafungu. Mara akatokea mshikaji anajifanya dishi limeyumba, ana mfuko wa rambo akachukua malimao mafungu saba halafu akanipiga kibao huku ananitolea macho. Nilimpiga ngumi za uso kama tano, jamaa dishi likaa sawa akaacha rambo akaondoka kwa kasi ya ajabu. Baadaye tukagundua anajifanya chizi akichukua vitu anapeleka kwenye hotel fulani hivi anauza.
2. Mwenge Dar es Salaam.... nilishuka kwenye daladala ya Mbagala nikawa nawahi ya Tegeta kipindi hicho foleni ni kubwa sana na magari ni machache. Wakati nagombea gari nikahisi mkono mfukoni nikaudakia hukuhuku mfukoni halafu nikamvuta jamaa pembeni. Akaanza kuniigizia kama vile dishi limeyumba, bila kumuuliza chochote nilimpiga ngumi mbili tu jamaa akazimia, wale wapigadebe wa Mwenge wakaja kumsaidia nikaondoka. Kesho yake napita pale namuona jamaa ni mzima kabisa kumbe siyo kichaa.
3. Watu wa Mbuyuni Moshi, kuna jamaa miaka ya 2006 alikuwa anavaa vyuma mwili mzima hadi kwenye nywele, hivi yupo bado? Yule ndio kichaa aliyewahi kuninyang'anya Tsh. 2000 halafu akaondoka kibabe