Econometrician
JF-Expert Member
- Oct 25, 2013
- 15,792
- 28,434
Baby lock, mafundi magari ni sawa na mafundi electronics wanapiga hela za bure kutokana na watu wengi kutokuwa na ABC za vitu husika.Mara ya kwanza kumiliki gari baada ya miezi miwili hivi mlango wa nyuma kwa abiria ukawa haufunguki kwa ndani, basi siku nimeenda kufanya service ya gari, nikamwambia ilo tatizo fundi, nikaona anatabasamu tuu alafu akasema ngoja ampigie fundi wa umeme, fundi kaja kachokonoa kiana mara mlango ukawa fresh, wakanitoa upepo kidogo. Daaahh nilipokuja kugundua shida ilibidi nicheke tuu.