St. Paka Mweusi
JF-Expert Member
- Sep 3, 2010
- 7,637
- 4,521
Chanjo ya kienyeji..Chajo ya Aina gani
Chanjo ya kienyeji..Chajo ya Aina gani
Hebu na wewe tunga moja tuStori zote hizo ni za kutunga, hamna yenye ukweli hata moja.
Kamera yangu nikiwa form 2 hadi form 3Mkuu simu yenyewe itoke wapi?? Ni katika kukumbuka tu visa na mikasa ya utotoni!
Enzi hizo kamera zilikuwa Konica au Yashica na picha ilikuwa mpk siku za sikukuu.Wapiga picha hawakuzidi wawili kata yetu!View attachment 1007652
Sent using Jamii Forums mobile app
Na mimi nipe pole...!!! Juzi kati nilienda kumtembelea anko, kijijini. Basi bwana, si unajua mambo ya shamba, kulikuwa na togwa ya kutosha. Anko alikuwa ameitengeneza togwa hiyo mida ya asubuhi. Kipidi hicho, sisi tulipenda shamba na wapwa zangu wengine. Tuliondoka 11.00 alfajiri na saa 5 ya asubuhi hiyo ndiyo tukarudi huku kijua kinawaka haswa. Kufika tu nyumbani, tukaikuta togwa. Basi kuiona togwa tu ! Nikainywa togwa kama sina akili nzuri ukizingatia nilikuwa nimetoka kwenye "jembe" na kijua kinawaka haswa.Pole mkuu umepitia magumu kiasi
Ya kawaida ndiyo maana Tanzania kubwa, siyo wanaishi mjini.mleta mada inaonekana wewe ni mpori mpori sana.... yaonekana sehemu kubwa ya maisha yako ume-spend porini.
Na siyo wote wanaishi mijini wanaishi vizuri pamaja na majumba ya kifahari, wengi wanalala nje, kwenye mabanda ya kukaangia chips.Maisha mazuri ni general term na personal perception. Kuna mtu anaishi maisha ya kiporipori anaenjoy zaidi kuliko mtu anayeishi maghorofani sijui na ukisasa.So, wewe ukiona unafurahia maisha ya usasa upo sahihi, na mwingine akiona raha kufurahia uporipori yupo sahihi pia!
Life is all meant to enjoy buddy!
Sent using Jamii Forums mobile app
Ya Chui hujamaliza vyema,eeehe baada ya kumuona ukapiga na mkuki ama?malizia basi
😂😂😂😂Mobutu Seseko wazabanga au mobutu Babu yako?thubutuu,umenikumbusha hadithi ya Mobutu alipokuwa na miaka 10 hivi alikutana na chui porini akiwa na mjomba wake,akamrushia mshale yule chui na kumuua.hii huwa naamini ni kamba
Mobutu Seseko wazabanga au mobutu Babu yako?
Duuuh ukute mtoa Uzi nae alimpiga mkuki chui akafaa😂😂😂ndio
hayo mate ya nyoka yalikupa maumivu? maana unasema yalisababisha uwe kama umeungua...Miaka inavyozidi kwenda wanyama wakali wanazidi kukimbia mbali na makazi ya watu hivyo kuwaona inazidi kuwa adimu.
Simba
Nakumbuka mwaka 1998 nikiwa na wawindaji wenzangu 6 (nilikuwa mdogo kuliko wote) tulikuwa kambi poli moja Tabora vijijini. Tulikuwa tumewasha moto huku twapiga story. Hii ilikuwa ni baada ya kumuua nyati mmoja mkubwa, sasa kwa sababu ilikuwa jioni tulishindwa kumgawa na kusafirisha kurudi kijijini, so tuliamua kukaa kibanda cha nyasi kusubiri kukuche. Usiku tulilala kwa zamu ili kuzuia fisi wasiharibu kitoweo chetu.Usiku huo ilikuwa ni mwendo wa stori na kuchoma nyama!! Majira ya kama saa 3 hivi tulighutushwa na kelele za mwenzetu aliyekuwa kalala kibandani, kumbe Simba limemkamata mguu pajani na kuanza kuondoka nae, aisee tulimfukuza huku tunamtupia vijinga vya moto mpk akamuachia jamaa. Mpk leo yupo na alama ya meno ya simba pajani!
Chui
Yes, same kijiji, siku hiyo ulikuwa usiku wa mbalamwezi. Nikiwa nimelala usingizi mara nikasikia kelele za yowe la mwanamke. Haraka niliamka, nikachukua mkuki wangu na kutoka nje huku nikiwa na tahadhari. Kumbe kelele zilikuwa jirani tu, nilinyata kufuata yowe lile! Hatua chache tu karibu na ile nyumba nilikutana uso kwa uso na chui!! Aisee sio kwa jasho lile lililonitoka! Chui alikua keshaua mbuzi wapatao watano!
Nyoka!
Hii ndo ilikuwa balaa. Tulikuwa tukitoka shamba na mama angu jioni kama saa 11 hivi. Nakumbuka I was std 6. Mama alikuwa na kuni kichwani na aliniacha nyuma like mita 120-150 hivi na nilikuwa na gunia la mihogo kichwani na panga mkononi!
Ghafla bin vuu!akaibuka nyoka mkubwa kwa kasi, akasimama mbele yangu na kupuliza mate fuuuuu!
Nilitupa gunia huku nikijikinga kwa panga usoni! Kilichofuata ni mbio kali sanaaa ambazo sidhani kama hata Usain Bolt angenikamata! Sikumbuki ndala zangu aina ya Sky way zilidondokea wapi na muda gani! Mate yalinipata mgongoni kiasi na nilibabuka ka nimeungua na moto mkali!!
Weka kisa chako tukumbukie when life was real life!!
View attachment 1007643View attachment 1007644
Sent using Jamii Forums mobile app
vipi ulirudia tena huo mchezo.Mungu ni mwema hukuwa kipofu.Pole sanaNikiwa mdogo kama umri wa miaka 7-10 watoto pale kijijini tulikuwa na michezo ya kuweka matope kwenye vichuguu halafu mnateleza na makalio . Vichuguu vingine vinakuwaga na mashimo ,Siku moja asubuhi tukiwa tunafunga mbuzi kama kawaida tukaanza mchezo wa kuteleza na tako toka kwenye kichuguu.
Sasa nilipopanda kwenye kichuguu nikakaa karibu na shimo kumbe kobra ndo anatoka shimoni ,kugeuka nyuma tukakutana face to face akanitemea mate machoni . Gafla nikawa naona giza halafu macho yanawasha kama nimemwagiwa pilipili kwenye macho,nikawa sioni wenzagu walinipeleka nyumbani .Kufika nyumbani mama aliniwekea mafuta (Samli ) kwenye macho yaani kupaka kwenye machoni .Nililala kuanzia saa tano asubuhi nimekuja kuamka saa kumi jioni macho yako mekundu yanaona kwa shida ,ila mda ulivyokuwa unaenda macho yakarudi kwenye hali yale ya kawaida kila kitu kikawa poa