Tuliowahi kudhulumiwa na Mtandao wa Tigo Tanzania tukutane hapa

NGolo Kante

Member
Feb 28, 2017
80
131
Mnamo Jumanne ya Tarehe 11 mwezi huu (Februari 2020) nilinunua kifurushi cha Internet kwa njia ya Tigo Pesa. Ndugu zangu wana JamiiForums yakapita masaa 24 bila ya kupewa kifurushi wala kupewa taarifa yoyote.

Nilichukua hatua ya kuwapigia Huduma kwa Wateja, nikajibiwa kifurushi changu kitawezeshwa baada ya masaa 24. Kwa hakika nilidanganywa.

Nikawa nikiwapigia simu kila baada ya masaa 24 lakini hakuna nilichosaidiwa zaidi ya kuambiwa nisubiri masaa 24 mengine na hadi leo hakuna nilichorudishiwa si fedha wala si kifurushi.

Huu mtandao umekubuhu kwa huduma mbovu lakini cha kushangaza sasa wamehamia hadi kuiba fedha za wateja.
 
Tigo wezi sana, walivyokua wananipa hasara kila nikiweka salio yaan ukichelewa kujiunga unakuta wamekata hata 100 bila sababu za msingi. So inabd ununue vocha nyingine ili kujazia kujiunga lile bando ulikua unataka.
Mimi wamenichosha sana Huduma kwa Wateja ovyo kabisa
 
Wiki iliyopita niliweka salio nikawa nataka kujiunga kifurushi cha intaneti cha sh 2000 1gb kipindi hicho ilikuwa, Kila nilipojaribu kujiunga niliambiwa salio halitoshi nikiangalia limo nikaona nijiunge kifurushi cha chini yake sh 1000 ilikuwa mb 300 wakati huo, kujaribu ikakubali. Kuanza kuperuzi youtube hakikumaliza hata dk 3 kikaisha. siyapendi Tigo majizi sana.

Siku hiyo walikuwa wanaiba kwa njia mbili
1. Ku encourage watu kujiunga kifurushi cha siku badala ya wiki ili kuvuna pesa nyingi kwa siku.

2. Kutoa mb pungufu ya kiwango ulichonunua. Mbin hii nimeiona hata kwenye vifurushi vipya vya sasa walivyotoa wanaotumia kuibia watu. Jana nilijiunga kile cha gb 3 sh 2000 sikufanya chochote nikaanza download video kuja kujumlisha saizi ya nyimbo nilizodownload hazikufika gb 3 ziliishia gb 1.4 kama sikosei
 
Niliambiwa kuna tatizo la kimtandao baada ya kujiunga bando la 2000 na kuwasha data kwamba wangenitaarifu mtandao ukikaa sawa.

Lakini sikuona hiyo sms hadi siku ya nne nilipoamua kujiunga tena na mtandao ulikuwa umerudi na maisha yakaendelea kwa hiyo elfu mbili ilienda kavu
Tunaweza vp kuwashtaki hawa watu au serikali inamikakati gani kudhibiti hii

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwaka jana mwezi wa 11 nilinunua kifurushi cha tigo 5000 kwa njia ya tigo-pesa mpaka leo sijapata hiyo huduma nimepga huduma kwa wateja mpaka leo naambiwa 24hrs
 
Jana nimemtukana mtu wa customer care. Laini yangu ni mpya, nilihamisha salio kutoka mpesa kila nikijaribu kununua kifurushi naambiwa transaction declined. You are not registered with this service, tangu wiki iliyopita.... kile kitoto kikanijibu ' tigo pesa yako iko vizuri, haina tatizo lolote...una tatizo lingine nikusaidie'? Angekuwa jirani nahisi ningemchapa makofi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwaka 2013 nilikuwa natumia line hii 071X008580. Kuna deni nilikuwa nadaiwa kama Tshs.35,000/-, Nikamtumia mdai wangu kiasi hicho mida ya saa tano usiku, Sikupata meseji yeyote ya uthibitisho, kuwa ujumbe wangu umefika kwa mlengwa japokuwa salio langu lilikuwa limekatwa tayari, na nilipojaribu kupiga call centre niliambiwa kuna tatizo la network mafundi wanajaribu kulitatua, nitapata mrejesho baadaya ya masaa 24.

Ilinibidi nizisubirie hizo saa, japokuwa mdai wangu alionyesha kama kutoniamini kwa kile nilichomwambia...baada ya masaa hayo kupita sikupokea ujumbe wowote..Nilifuatilia takribani mwezi bila ya majibu yenye uhakika..zaidi ya tatizo letu la kiufundi likitatulia utaona ujumbe huo mfupi.

Nizungumzavyo mpaka leo sikupokea ujumbe wowote na hela yangu ilikatwa. ilipita mwaka sikuwa na imani tena na hii kampuni...Mpaka leo siitaki hata kuisikia...Majuzi nilipiga hiyo namba yangu ikapokelewa na bidada mmoja nasikia yupo mbeya.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom