Tuliowahi kuchunga wakati tukiwa wadogo tukutane hapa

kALEnga kidamali

JF-Expert Member
Nov 19, 2015
542
733
Jamani wale wote ambao tumewahi kuchunga wakati tukiwa wadogo kabla hatuja anza shule na hata baada ya kuanza shule yaani ukirudi shule unachunga na zile siku za wikiendi basi wewe ni kwenda porini/malishoni kuchunga mifugo kama vile ng'ombe, mbuzi na kondoo tukutane hapa kuelezea uzoefu wetu pamoja vituko, mikasa na masahibu ya huko porini/malishoni ulipokuwa unachunga.

Mimi nilikuwa nikipenda sana kutokana na zile raha za kupata kila aina za matunda huko maporini pia kulikuwa na kuwinda wanyama wadogowadogo kama vile digidigi, pimbi, sungura pamoja na kanga na kware yaani ilikuwa wewe mchungaji unaporudi unapokelewa kwa heshima Kubwa ukirudi hasa ukiwa na mnyama uliyewinda huko machungoni, yaani ilikuwa kijana anayechunga anajaliwa na kuheshimiwa nyumbani mda wote kabla ya kutoka na baada ya kurudi machungoni anapewa chakula kizuri cha kushiba bila kusahau maziwa ya kutosha hata kama chakula ni kidogo basi atakula mchungaji kwanza wengine mtasubiri baadae wasiowachungaji walitamani kuwa wachungaji kutokana na mchungaji anavyojaliwa pale nyumbani kwetu.

Kingine nilichokuwa nakipenda ni kutembea na jeshi la mbwa wakali waliofundishwa kuwinda huku kila mbwa akiwa kapewa jina lakie kama vile chui, simba, nyati, mbogo, mwitu, jeshi, polisi, n.k

Hawa mbwa kwanza wakati wa kwenda machungoni ilikuwa ni mwiko kuwapa chakula(asiwe mvivu kuwinda) yaani mbwa akiwa na njaa akifika porini dakika kumi nyingi digidigi kadakwa hapo utasikia mbwa akitoa mlio wa sauti kuashiria mimi niende kuna jambo limetokea kwani wakikamata mnyama yeyote hawamli hadi mimi niende nikamchukue kama ni kumalizia kumchinja nifanye mimi na hapo mbwa watafurahi sana kwani kichwa ,miguu,matumbo ya ndani ndio mlo wao yaani nilikuwa nawapikia supu moja matata mno, baada ya kuja huku dsm nimeshangaa kuona supu lile ndio linaitwa kongoro.

Aisee ninayo mengi, hebu share na wewe yako.
 
Sitasahau siku moja nilisikia mbwa wakitoa milio fulani hivi pembeni ya kichaka kimoja nikaenda fasta kwa bashaha zote nikajua kuna mnofu umedakwa, ile kufika asalaaaaleee! Nikakuta mbwa mmoja anamalizia kukata roho kagongwa na nyoka aina ya koboko Kubwa hilo, zile mbio nilizotoka nazo hapo ilikuwa ni hatari yaani niliondoa ng'ombe haraka na kulihama lile pori na sikuwahi rudi tena lile pori. Niliambiwa koboko akikugonga nusu saa haifiki usha fika akhera sasa nikawa nimejawa hofu hatari.
 
Nakumbuka mengi coz am cowboy. Ntakuja na story kamili but kwa kuanzia

1. Kupewa maziwa mengi kabla ya kutoa mifugo na baada ya kumrudisha
2. Tulikuwa tunashindana nani atakaeenda ndani zaidi ya Pori
3. Kuwinda ndege na sungura
4. Kuogelea kwenye lambo la kunyweshea mifugo ,hapo panakuwaga na Mademu wanaochungaga nyumban
5. Hamna kitu raha kama mbuzi kuzaa mapacha kwenye zamu yako ,unawabeba vitoto vya mbuzi kifuani hadi nyumbani
 
Kama ulikuwa hudandii ng'ombe kama farasi basi hujachunga.

Kama ni mkubwa sana unavizia akiwa anakula majani unatumia kichwa chake kama ngazi,kosea timing akanyage kidole cha mguu unaouacha chini,niliishatolewa kucha kwa mkasa aina hii.

Kosea mambo yote ila my friend usijevaa koti lenye kofia juu ukapita karibu na ng'ombe atakuzingua vibaya sana(sio hawa ngombe wenu wa maziwa).

Kuna mang'ombe ilikuwa ukizubaa tu yanaenda kwenye mashamba ya watu.

Kingine ngombe nayeye ana tabia kama ya mbwa,akijutisha ukajaa,anakuoshea, ila ukimkazia anatulia.
 
kama ulikuwa hudandii ng'ombe kama farasi basi hujachunga.
kama ni mkubwa sana unavizia akiwa anakula majani unatumia kichwa chake kama ngazi,kosea timing akanyage kidole cha mguu unaouacha chini,niliishatolewa kucha kwa mkasa aina hii.

kosea mambo yote ila my friend usijevaa koti lenye kofia juu ukapita karibu na ng'ombe atakuzingua vibaya sana(sio hawa ngombe wenu wa maziwa).

kuna mang'ombe ilikuwa ukizubaa tu yanaenda kwenye mashamba ya watu.

kingine ngombe nayeye ana tabia kama ya mbwa,akijutisha ukajaa,anakuoshea.ila ukimkazia anatulia.
We jamaa kama mimi mda wa kuludi nadandia kama star wa kichina.
 
kama ulikuwa hudandii ng'ombe kama farasi basi hujachunga.
kama ni mkubwa sana unavizia akiwa anakula majani unatumia kichwa chake kama ngazi,kosea timing akanyage kidole cha mguu unaouacha chini,niliishatolewa kucha kwa mkasa aina hii.

kosea mambo yote ila my friend usijevaa koti lenye kofia juu ukapita karibu na ng'ombe atakuzingua vibaya sana(sio hawa ngombe wenu wa maziwa).

kuna mang'ombe ilikuwa ukizubaa tu yanaenda kwenye mashamba ya watu.

kingine ngombe nayeye ana tabia kama ya mbwa,akijutisha ukajaa,anakuoshea.ila ukimkazia anatulia.
sasa ng'ombe na yale mapembe akutishe halafu unakazaje sasa?
 
Sitasahau siku moja nilisikia mbwa wakitoa milio fulani hivi pembeni ya kichaka kimoja nikaenda fasta kwa bashaha zote nikajua kuna mnofu umedakwa, ile kufika asalaaaaleee! Nikakuta mbwa mmoja anamalizia kukata roho kagongwa na nyoka aina ya koboko Kubwa hilo, zile mbio nilizotoka nazo hapo ilikuwa ni hatari yaani niliondoa ng'ombe haraka na kulihama lile pori na sikuwahi rudi tena lile pori.... Niliambiwa koboko akikugonga nusu saa haifiki usha fika akhera sasa nikawa nimejawa hofu hatari
Koboko hatari sana mkuu.Shukuru Mungu hakukudhuru.
 
Back
Top Bottom