Tuliowahi kuchukua mikopo tukafanya ndivyo sivyo

Nilichojifunza mimi,usikope ili kununua kiwanja au kujenga nyumba ambayo haizalishi bali kopa na wekeza kwenye kitu kitakachokuwa kinazalisha ili mkopo ujilipe wenyewe
Shida ipo hapo kwenye kuweza kubuni kitu ambacho kitazslisha pesa ili deni lijilipe lenyewe unaweza anzisha shughuli ikafa ukiwa hujapata hata mia. Si rahisi kupata mkopo wa kujenga na kumaliza nyumba hapohapo na kuanza kupata mpunga kutokana viwango vyetu vya mishahara. Hata hivyo yote kwa yote ni kujaribu ukipata changamoto unajifunzia mumohumo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Baada ya kuchoka mishahara ya wahindi niliamua kujiajiri, nikawa nafanya biashara ndogondogo maisha yanaenda, nilikuwa nachukia Mikopo Sana, baada kuingia Kwenye biashara hukuhuku nikaona bora niingie Kwenye vikundi vya wanawake pamoja na Vicoba, nilikuwa na Vicoba vitatu na vikundi vinne vyote nilikuwa na vihudumia naweka tu Pesa sikopi.

Baada ya story za Mikopo za wanachama wenzangu Sasa na Mimi nikaona acha nikope bank nifungue biashara yangu moja ya uwakika nikakopa mil 10 marejesho miaka mitatu, Pesa yote niliingiza Kwenye mzunguko wa biashara mwaka wa kwanza marejesho yalienda Safi Kabisa mwaka wa pili matatizo yakaanza biashara zikafa nikabaki na shamba la korosho na msimu Kama mnavyojua mwaka kwa mwaka. ikawa ikifika tarehe ya rejesho nakopa Kwenye kikundi napeleka bank ikafika wakati vikoba vyote vitatu na vikundi mpaka wanachama wananidai Huku rejesho bado halijaisha la bank.

Nikavuna korosho nikasema Pesa Itanisaidia kupunguza madeni, mwanaume niliyekuwa naye akanishauri usilipe Pesa yote madeni zungushia biashara Huku unalipa madeni kidokidogo. Pesa nikampa mpenzi tuzungushe biashara akanidhulumu ikafika wakati sina hata mia mfukoni marafiki wote wamenikimbia bank nadaiwa, kila kona na madeni Sina kazi Sina biashara nilala ndani Kisa madeni ya watu ya riba mitaan sitaki kukumbuka nilisota nakusota. Ndugu Zangu ikabidi wajichangishe kulipa Mkopo WA bank iliyobaki maana ilibaki miez michache niliiweka dhamana viwanja vyangu viwili. Wakaona bora wanisaidie kuliko vipigwe mnada wakati nilibakisha kidogo.

Hii Mikopo mingine ya vikundi, vikoba na mitaani watu walinidai mpaka walikaa kimya na kuchoka maana Sina kitu Niko mweupeeeee. Baada ya kuumalizika Mkopo WA bank nikauza kiwanja kimoja nikalipa lipa madeni ya mitaani nikabakiza Pesa kidogo nikaaza na moja biashara

Sasa hivi sitaki kusikia Mikopo, vikoba Wala vikundi maana kwa wanawake wengi humo Ndio Huwa Chanzo cha matatizo na wahanga ni wengi maana humo watu wana ushawishi wa ajabu, Kama Sina najua Sina ila Sina Deni na mtu kuliko huna alafu udaiwe utatamani ufe kwa muda. Mikopo inaumiza .
Ufe kwa mda alafu baadae ufufuke au?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Financial literacy ni jambo muhimu sana. Mikopo ni mitamu asikwambie mtu, ila kulipa ni kuchungu kupita maelezo.

Kuna mambo mengi sana ya kuangalia ili usije kulia. Ni mkopo wa kiasi gani? Unarudisha kwa muda gani? Riba yake ni kiasi gani? Ni riba ya aina gani?

Vijana wengi sana wanaumizwa ni mikopo hasa hasa ya magari. Unakuta kijana kachukua mkopo 12m, interest 24% per annum. Mkopo wa miaka 3. Wengi hawapigi hesabu kujua ni kiasi gani watalipa mwishoni, kila mwezi etc. Mkopo kama huu, mwishoni mtu atalipa jumla karibu 20ml, by that time ki Alteza kimeshakufa na kimemtia gharama za kutosha.

Mkopo unahitaji umakini mkubwa, usijekuta unalia.
Ila mikopo mingi ukiangalia sana mwisho wa siku unaezakuta riba ni zaidi ya ile inayosemekana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mm sijawahi kukopa na sitokuja kukopa unajua sababu gani mm ni loan officer wa miaka miwili nadai mpaka mdaiwa akiniona anahisi amemuona Israel mtoa roho yani mda wa ku recovery madeni nadai mpaka najihis kujiogopa yani Kama unatakaa kupungua mwili kwa stress njoo nikukopeshe alafu usilipe unizungushe.

Sent using Jamii Forums mobile app
Anayetaka kukonda bila mazoezi inabidi aje kwako kukopa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nilikopa mwaka jana NMB Mi. 9 kwa miaka mitano. Nikachukua pikipiki mbili. Moja ya bodaboda na nyingine ya kwangu kutembelea. Mil.4 nikachukua kiwanja na shamba kwa ajili ya kilimo. Laki 5 nikalimisha shmaba na kupanda mahindi na laki tano nikafanyia mambo yangu menginene. Mshahara nikabaki 247,000

Matokeo yake;

i)Bodaboda ilidumu miezi sita ikaibiwa.
ii) mahindi sikupata hata nusu gunia,kwa sababu ya ukame.
iii)mipango yangu ilikuwa mwaka huu nioe kama mambo yangeenda vizur kinyume chake nimeshindwa,mchumba wangu alipoona hali imekuwa tete akaanza visa kumbe kashaanza mahusiano na mwanaume mwingine,nikabaki mimi kama mimi.
iv)Baada ya bodi ya mkopo kuanza kukata 15% nikaanza kuchukua 197,000/= kwa mwezi
v) kwa sasa siwezi saidia chochote kwa mama na ndugu zangu kibaya zaidi mdogo wangu kachaguliwa chuo cha afya diploma ada mil.2. 5 sijaweza kumpa hata mia.

Sina bahati kabisa
pole sana hii ya bodi 15% imeongeza maumivu
 
Mm sijawahi kukopa na sitokuja kukopa unajua sababu gani mm ni loan officer wa miaka miwili nadai mpaka mdaiwa akiniona anahisi amemuona Israel mtoa roho yani mda wa ku recovery madeni nadai mpaka najihis kujiogopa yani Kama unatakaa kupungua mwili kwa stress njoo nikukopeshe alafu usilipe unizungushe.

Sent using Jamii Forums mobile app
daah umetisha broo
 
Daaah!!mi wakati naanza kazi nilikopa 5mil,nilitoa hela yote kwenye account,nikanunua pikipiki ya kutembelea na iliyobaki niliweka gheto ktk bukta flan zile timberland si unajua zinakuaga na mifuko mingi!!bhas bhana mi nakula ugimbi nikiishiwa narudi gheto nazama ndani nachomoa mzigo nasepa naenda kula vyombo!sitosahau Kuna siku naingiza mkono kwenye mfuko imebaki 30,ikabidi niichomoe ile nguo kwenye msumali nikapekua mifuko yote na kukung'uta hamna kitu!!ikabidi nikatoka njee nikaingiza pikipiki ndani nikalala zangu!!
Ah ah umenichekesha Sana mkuu ukajua umeibiwa nn?
 
Mikopo inaumiza sana. Tangu nimalize mikopo, sina deni now sidaiwi na mtu, basi nalala usingizi mnono kama mtoto mchanga. Nilishawahi kukopa milioni kumi nikaongezea na za kwangu nikanunua gari ya biashara. Ndani ya mwezi mmoja gari ikala mzinga. Niliteseka sana kulipa deni na kuishi kigumu gumu. Nimeshaapa siku mtu akinona najaza fomu kuchukua mkopo kwenye taasisi ya fedha, basi mtu huyo anichinje kwa msumeno!
 
Huu mkasa nilishautoaga humu, sio mbaya nikirudia. Okay nitaelezea in first person view.

Mwaka 2011, nilikuwa nimeacha kazi serikalini, nikaamua kuanza biashara ndogo ndogo kwani zililipa kuliko mshahara wa kazini. Hapa nilikuwa na girlfriend ambae nilimtambulisha nyumbani na kwao pia walinijua. Mimi na huyu gf wangu tulifungua kampuni moja, nitaaiita Xcorp. Gf wangu yeye alikuwa muajiriwa wa serikali(mwanasheria), kwahiyo alikuwa vizuri in terms of lifestyle. Basi tukaamua kuexpand business, tuliplan kujenga kumbi nne ambazo zitakuwa za kisasa... Tuliplan kuweka swimming pool, malls humo humo. Ilitakiwa 1bil. Tukasema we can make it. Wakati naendelea na vibiashara vidogo vidogo vya kwenda China, rafiki yangu wa kike akanitambulisha kwa rafiki yake. Nae alikuwa mdada. Huyu dada nitamuita Grace. Grace alionekana ni mtu mwenyewe mafanikio sana. Aliishi Masaki nyumba ina swimming pool, na counter, pia alikuwa akitumia magari ya bei; BMW X5, Hilux new model, Brevis, Mark X na Range Rover. Kwa kweli enzi hizo Mark X na Brevis zilikuwa za kuhesabu barabarani. Huyu dada akaniambia yeye ni mfanyakazi wa kampuni ya mtandao mkubwa hapa Tz. Basi akaniambia wanaproject lakini inaitaji investors. Hii project ilikuwa kama ndoto ya mchana kwani ndani ya mwaka mmoja ningepata 1B.

Nikamueleza gf, akanielewa. Basi mwanzo tukawekeza 40m tu. Kweli ndani ya wiki mbili tulipata faida ya 40m!!! So tukarudishiwa 80m!!! Aisee nikapiga picha, ile biashara ya China bora niiache kwanza mikiki mikiki ya bandarini na mzigo hapa Tz unakaa miezi miwili plus kuja kuisha na faida ni kama 40% tu. Basi Grace akanichombeza ningeongeza hela ya kuwekeza to 400m. Ningepata 800m faida na ningekaribia goal ya 1b. Nikauza viwanja vyote, magari yote(nilikuwa nayo 8) sikubakiza hata moja, mtaji wa China wote nikakusanya. Nikawa na kama 230m. Nikamuomba Gf aniongezee, akagoma, akaingiza maswala ya kwamba mimi natembea na Grace(hii story nyingine) ila sio kweli. Baadae Gf akaniambia kwanini usiombe mkopo kwa nyumba yako. Duh nikasema poa. Gf ndio alikuwa na connection na watu wa benki basi tukaomba mkopo kwa kutumia kampuni yetu, nikaweka nyumba dhamana. Hapa ndipo natamani ningerudisha siku nyuma.

Wiki ambayo mkopo ulikuwa unatakiwa utoke sikupigiwa wala nini. Nikakaa kimya. Wiki ya pili nikaenda ile benki. Wakaniambia mbona ulikuja kuchukua na ukasign kabisa. Duh nikaenda kuangalia, signature sio yangu, na hela kweli zimeingia, lakini ajabu zimeingia kwenye account ya Gf. Nikampigia hapo hapo. Nilimuwakia sana. Akaniambia hela alishampa Grace 400m. Mkopo tulipata 156m, ilibidi turudishe 200m in 1 year. Dadeki nikaona huu utani. Nikamfata Gf home tulifokeana sana(advice usioe/usiolewe na mwanasheria kama hujui ubishi) nikatulia. Akaingiza mambo ya mimi kutoka na Grace, mara haniamini. Ajabu ni kwamba asilimia kubwa ya vitu at risk ni vyangu yeye kwenye biashara ya China alinipaga kama 30m tu. Kwasababu nilimpenda nikakausha. Grace wiki ya kwanza tuliongea freshi tu, ila baada ya wiki akapotea.

Duh wasiwasi ukanijia. Ila nikasema tusubiri ule muda aliosema hela zitarudi. Muda ukapita Grace hatujui alipo. Gf akanigeuzia kibao mimi. Mara mimi ndio nilimtambulisha kwake. Basi nikamfata yule dada aliyenitambulisha. Akaniambia yeye hayupo karibu nae. Aisee nilitamani kuua mtu. Yeye mwenyewe kweli alivyoniunganisha nae sikumueleza yaliyoendelea. Kwanza alikuwa hajui kama nafanya biashara na Grace. Kwenda kwake Grace nakuta kahama na nyumba ilikuwa ya kupanga sio yake. Magari ya kukodi, yeye alikuwa na BMW X5 tu. Nikaenda kampuni ya simu aliosema ni mfanyakazi, hajulikani!!! Nilikaa chini kwenye floor. Miezi ikapita.

Gf alivyoona nimeishiwa, akawa distant, mara hapokei simu. Matusi kwa wingi, baada ya muda akaniacha. Life lilikuwa gumu. Mwezi uliobidi turudishe mkopo ukaingia, sina mia. Ndugu ndio wananitumia hela ya kula. Siku mbili zinaweza pita nyumbani giza, sina hela ya LUKU. Mboga nzuri ilikuwa dagaa mchele. Grace hajulikani halipo. Basi nikaanza kumkazia Gf, kumtishia kuwa alifoji signature yangu. Basi akawa na uwoga nae akaanza kunisaidia kumtafuta Grace. Akafanikiwa, alimuweka Grace ndani kama wiki nzima kabla hajapata mdhamana. Nikaja kujua ukweli, kumbe Grace ni tapeli hata zile hela za mwanzo zilirudi kwasababu aliwachimba wengine. Kiukweli life lake ni show tu ya kuwateka watu. Basi tukambana, akatupa documents za nyumba yake moja. Akasema ndio alichonacho, BMW lake kuna victim mwingine alishalichukua na bado ana mdai Grace 40m. Therefore nae akagangania documents za nyumba. Tukaongea na polisi, maana Mimi nadai 400m mwenzangu 40m bora nipewe Mimi. Polisi wakasema twende court, mwenyewe sina hata mia. Na yule mdai mwingine yupo vizuri kifedha, as you all know bila hela mahakamani... Acha nisimalizie. Nikaongea na mdai, nikamwambia tuuze nyumba nitamlipa 40m alafu nitachukua iliyobaki. Akakubali ila yeye abaki na documents.

Mzaa. Nyumba haina hati, kwanza value 260m ya kwangu ilikuwa 516m. Kwasababu sina kitu nikakubaliana na hali halisi. Nyumba ya Grace ilikuwa haijamalizika, matengenezo kama 40m, ilikuwa golofa. Nyumba haikuuzika mwaka mzima. Baada ya muda wa kupiga stop order, benki wakapiga mnada nyumba yangu nikahamia ghetto. Nikaanza kupaona kuzimu aisee. Nikasema nisue benki maana walicheza mchezo na Gf, na hela sina za kupambana nao. Nikaona nikimtubua Gf nitajiharibia mwenyewe. Basi Grace tukaachana nae kwani na yeye kapigika mbaya.

Huu mwaka wa 5 tangu nyumba yangu iuzwe. Nakaa jumba amabalo mvua ikinyesha maji yanaingia godoro linaloa. Sina gari wala baiskeli. Nikiona mtu ana starlet namuona Mungu. Msosi nasaidiwa na ndugu. Bado nipo kwenye harakati za kutafuta mteja wa nyumba ya Grace hata kwa 150m nauza nianze upya.


Back to third person view. Gf ana life jingine na kidume mwingine, life is good. Ila Gf yupo hatarini, kwani soon TAKUKURU will be after her. Huu mkasa umemtokea ndugu yangu wa karibu sana. Siku anatimuliwa na polisi kwake alilala mpaka kwenye mchanga analia. Na nyumba yake mpaka leo wateja wanakuja na kuchomoa, haijauzwa. Mpaka watu wa benki wanaleta waganga wafanye manyanga. Nyumba imekaa haina watu mpaka walinzi wa benki wanapangisha vyumba vya ndani. Huyu ndugu yangu kakimbiwa na watu wengi wa karibu kwasababu wanajua kaishiwa. Anyway lesson learnt, Mimi namuomba Mungu aniepushe na haya. Bora niishi na salary au biashara ndogo kuliko kukopa. Ukikopa unakuwa mtumwa.

-callmeGhost
Huyo dem wa jamaa ndo hafai kabisa,alikuwa na kihelehele gani paka aforge signature bank na kumpa mkopo wote grace??.

Inawezekana walishilikiana,dah inauma sana hii.
 
Mikopo ni noma, hasa ile unapo anza anza kazi. Kuna jamaa yangu amebaki na ufunguo wa gari tu (alichonga copy), gari alishauza na bado anadaiwa na bank. Bahati nzuri alikua staff wa bank hiyo aliyokopa. Anajuta bora angenunua hata kiwanja....
Daah ushahidi km aliwah kumiliki gari lol
 
Back
Top Bottom