Tulioumizwa viwanja Jiji & Kamishna Mkoa Dodoma 2024 tukutane hapa!

Yesu Anakuja

JF-Expert Member
Apr 10, 2019
12,675
25,924
Wife yupo Dodoma huko serikalini, nafanya shughuli zangu DSM, tangu enzi za magufuli kuhamisha watumishi nikasema ninunue viwanja kadhaa, ashukuriwe Mungu vingine nilijenga na nilipata wapangaji wazuri, in the process kujenga vingine nikaja gundua kumbe ni viwanja hewa, vina double allocation. Kumbe pale jiji kuna vibaka wa ardhi hatari kuliko majambazi ya kutumia silaha haya tunayoyaogopa, Dodoma ni sehemu hatari sana kununua ardhi, tumepigwa tukio moja baya sana na wafanyakazi ardhi jiji, na kamishna wa ardhi Mkoa yule mfupi hana uwezo wowote kutatua mgogoro na ushahidi unaonyesha anashirikiana na Jiji hadi Mathew kamishna mkuu wapo pamoja. ni kama ile ya traffic police, anachukua rushwa halafu anaanza kuigawa kwa DTO, kwa RTO hadi kwa Mkuu wa traffic taifa.

naongea kwa uchungu kwa sababu nimekuja kugundua, walioniumiza sio raia, ni maafisa wa ardhi jiji kwa kushirikiana na kamishna wa ardhi Mkoa wa Dodoma. miezi 6 iliyopita nilienda Dodoma kufuatilia na nilionana naye,majibu aliyonijibu yalionyesha moja kwa moja yeye ndiye adui yangu. sijawahi kuona mfanyaazi wa serikali mwenye kiburi kama yule kijana. na sijaelewa anatoa wapi kiburi. kuna kipindi alikuja Waziri Jerry slaa nikaamini angesafisha wale watu, tutapata haki zetu, lakini alipoondoka tu mtu niliyemweka Dodoma afuatilie ananiambia kila kitu kimerudi kama mwanzo. hivi wafanyakazi wa ardhi mtamwogopa lini Mungu?

Kwanza kabisa, Sina hata haja ya kuomba Waziri wa ardhi afanye assessment ya wafanyakazi hao na kumwondosha kamishna wa mkoa Dodoma, kwa sababu najua hatafanya hivyo, hao viongozi wote wakichaguliwa, huwa wanawatumia haohaoo kutafutiwa viwanja na maeneo ya kupora. ni vitendea kazi vya mawaziri na viongozi. ndio maana wana kiburi na wanajua huwezi kuwafanya kitu.

Pili, Nimeweka hoja ili wale tulioumizwa na jiji pamoja na kamishna yule mwenye kiburi, tukutane, tutoe walau ushuhuda kupooza mioyo, na kupeana mawazo namna ya kuwakabili.

Tatu, Hatuchafui mtu, hatuonei mtu, ila walioumizwa na hawa watu, wanajua ninachoongea. ni maharamia wa ardhi wakubwa mno, wanamiliki ardhi mno, na wana kiburi mno kwa sababu uhamisho wa serikali kuja dodoma uliwafanya viongozi wengi wawatumie kupata viwanja, sasa ile kuwa na connection na wakubwa waliowatafutia viwanja kumewafanya wawe na kiburi kikubwa mno, na kweli, sisi raia tunaweza tusiwe na uwezo kuwafanya kitu.

kilichobaki tunawashitaki wa Mungu tu.
 
Ila kwa Tanzania kwa tathmini inaongoza Dodoma na Dsm. Kamishna Mkuu wa Ardhi Mathew anawalea sana na yeye ni sababu ya haya yote, na ni kama serikali haioni hili, watu wanaumiza sana uchumi wao kwa watendaji kulelewa maofisini. Na wana lugha chafu, kama huyo kijana wake kamishnaw a mkoa Dodoma, ni nani anampa kiburi? yule aliyekuwepo kabla ya Jabili alikuwa worse, wakaleta Jabili ambaye ni worst. kila nikifuatilia Jabili analalamikiwa na kila mtu, kwa kiburi, majibu machafu wakati watu wamedhurumiwa. niliwahi kumkuta mama mmoja kalizwa viwanja vingi hadi nikaona mimi kama shida yangu ndogo sana.
 
lakini shida ya hawa maafisa ardhi kama mnasema ni nchi nzima ni nini? serikali haioni?
 
Pole!
Yesu ameacha mtu wake upigwe na matapeli.
I guess Yesu alikaa mahali akicheka tu unavyotapeliwa sio?
Sasa unawashtaki hawa matapeli kwa Mungu tena wakati Yesu na Mungu walikuwa wanashuhudia tu wanavyokutapeli?
 
Yesu ameacha mtu wake upigwe na matapeli.
I guess Yesu alikaa mahali akicheka tu unavyotapeliwa sio?
Sasa unawashtaki hawa matapeli kwa Mungu tena wakati Yesu na Mungu walikuwa wanashuhudia tu wanavyokutapeli?
naongea tu ili kama kuna watu wengine tuwajue, ila upande wangu Mungu alishanipa uwezo, vita nimeshashinda ndugu. nakupa miezi 3 nitarudi hapa kukupa mrejesho.
 
Sawa..utanitag.
I am just collecting kujua walioumizwa, kuna mtego mkubwa sana umetegwa ambao hata kama watakuwa na viongozi wa serikalini wanawabeba, safari hii lazima haki za watu zipatikane, hawana uwezo kuuruka kihunzi hiki tena. na ninakusanya hadi majina yao na nitafuatilia hadi mali wanazomiliki hadi viwanja walivyonavyo kila kitu. waligusa pabaya na lazima tuwaokoe wananchi. tukomeshe kabisa ili hata kama wataendelea kuumiza watu waumize wakiwe macho.
 
Pole mkuu, pole sana...

Endelea kuwaanika mitandaoni tu...

Hawa wajinga hufanya upuuzi ila hawataki upuuzi wao ujulikane...

So nina uhakika kama ulicho andika ni kweli, haki yako utaipata.
 
Pole mkuu, pole sana...

Endelea kuwaanika mitandaoni tu...

Hawa wajinga hufanya upuuzi ila hawataki upuuzi wao ujulikane...

So nina uhakika kama ulicho andika ni kweli, haki yako utaipata.
nilichoandika ni kweli 100%. na ninajua kuna wengi sana wameumizwa sana humu na washakutana na huyu kamishna, wanakijua ninachoandika.kama hakuna aliyekutana naye, just wait, mtakutana naye tu na hao vijana wake, labda kama hautakuja kumiliki kiwanja dodoma.
 
Hapo lazima iwepo give and take, and if possible kama mtu kajenga, abaki, yule mwingine serikali ifute hati yake, na imfidie.

Kuna viwanja viangongana, the same.

Billions kadhaa side set aside for the purpose
 
niko na wenzangu, tunakusanya data, tumegundua mambo ya ajabu sana. kuna mawaziri kadhaa pia tumepata viwanja vyao na maeneo kadhaa mengine katikati ya jiji, wanampango kujenga hoteli. kama wanavipata kwa haki, sio shida, shida ni kwamba hawa vijana huwa wanawasaidia viongozi vitu kama hivyo ili na wao wakiumiza raia wale viongozi wanawakingia kifua. kilichopo sasaivi tutakuwa tunataja zurumati wa kiwanja, na viongozi wanaowakingia kifua. uzuri hata wao kwa wao wanashindana na wanafichuana hivyo sio tatizo kupata data. just wait, kitu kinapikwa.
 
Hapo lazima iwepo give and take, and if possible kama mtu kajenga, abaki, yule mwingine serikali ifute hati yake, na imfidie.

Kuna viwanja viangongana, the same.

Billions kadhaa side set aside
kama jiji kama dodoma wanapopasifia kuwa pamepangwa bado kuna double allocation, itakuaje kwa hapa DSM? na kwa nini hii issue ya double allocation imekuwa wimbo wa miaka mingi sana? kama wanashindwa kazi kutatua migogoro, si wapishe watu wengine wakae viti vyao? makamishna wa mikoa wamekuwa miungu watu, kama hako kafupi ka dodoma. analalamikiwa na kila mtu lakini serikali bado inaye tu.
 
Sio Dodoma ardhi tu, kwa sasa ofisi zote za serikali nchi nzima zimeoza, nenda ofisi ya serikali popote uone utakavyohudumiwa. Ni kiburi kwenda mbele na huwezi kumfanya mtu lolote.
Kabisa! Huku Dsm kuna kajamaa kanaitwa Mageni kanakalia miamala ya watu bila sababu. Ardhi kote kumeoza
 
Back
Top Bottom