Tuliosoma Shule ya Sekondari Tosamaganga tukutane hapa

Gonga sana kitimoto maeneo ya ipamba,nadhani manakumbuka sumu na haragwe ukilila sana inakuwa so kwenye kohooo,weekend taratibu amaeneo ya ipamba kwenda kugonga kitimoto,baada ya hapo tunapitia mtoni tunaoga na kurejea shuleni.
 
What a NOSTALGIA!!! Mkubwa umenikumbusha mbali sanaaaaa. Mimi katika waalimu ambao sitawasaha ni mwalimu MGUNYA!!! Alikua akikubamba mitaa ya Ipamba hospital umekwisha!!! Kabla ya kukugaragaza anakuuliza "UNA KILO NGAPI WEWE?" Duh!! Enzi za Mpogole AKA DUDU, AKA Simba wa Tsavo! NOSTALGIA In deed....
 
What a NOSTALGIA!!! Mkubwa umenikumbusha mbali sanaaaaa. Mimi katika waalimu ambao sitawasaha ni mwalimu MGUNYA!!! Alikua akikubamba mitaa ya Ipamba hospital umekwisha!!! Kabla ya kukugaragaza anakuuliza "UNA KILO NGAPI WEWE?" Duh!! Enzi za Mpogole AKA DUDU, AKA Simba wa Tsavo! NOSTALGIA In deed....
Mgunya alienda kuwa Headmaster kigonsera akaharibu sahv yuko moshy ni mkuu wa college fulan hv
 
Kwa wale 2liosoma miaka ya 2006/08 tulikuwa na bahati mbaya yaan ndan ya miaka minne wenze2 wanne walitutoka,sababu ni magonjwa km kuhara dam na kipindupindu.Niliumia sana mwenze2 m1 2lishiriki nae mahafali ya ku2agwa alikuwa 4m6 mwenzetu,then baada ya cku km mbili hv akafariki.Sitosahau pia 2lipofanya maandamano ya kumtoa mwenze2 aliyekamatwa ki2o cha police Ipamba,katika hali ambayo hatukutarajia 2livamiwa na wanakijiji waliokuwa na silaha km mishale,mapanga,rungu na kupelekea mwenzetu m1 kufarik na wengine kujeruhiwa.R.I.P kwa wote waliofariki,tunamshukuru mungu tuliotoka salama
 
Kwa wale 2liosoma miaka ya 2006/08 tulikuwa na bahati mbaya yaan ndan ya miaka minne wenze2 wanne walitutoka,sababu ni magonjwa km kuhara dam na kipindupindu.Niliumia sana mwenze2 m1 2lishiriki nae mahafali ya ku2agwa alikuwa 4m6 mwenzetu,then baada ya cku km mbili hv akafariki.Sitosahau pia 2lipofanya maandamano ya kumtoa mwenze2 aliyekamatwa ki2o cha police Ipamba,katika hali ambayo hatukutarajia 2livamiwa na wanakijiji waliokuwa na silaha km mishale,mapanga,rungu na kupelekea mwenzetu m1 kufarik na wengine kujeruhiwa.R.I.P kwa wote waliofariki,tunamshukuru mungu tuliotoka salama

Hebu jifunze kuandika vizuri. Utafikiri umesoma shule za kata kumbe umesoma shule yenye jina kubwa. Ona sasa mwenze2, ki2o ndiyo nini? Aghrrrr!!Au wewe mamluki siyo Tosa boy?
 
Vipi ulanzi ulikuwepo kama wale wa malangali?
Hilo siyo la kuuliza. Wanywaji walikuwa wanakwenda Banavanu, Msiwasi au Ipamba mpaka junction (kilometa 7 toka shuleni). Na wale wataalamu walikuwa wanakwenda kuwapiga stop wakina mama-muuza anapotoka nao sehemu kupeleka kilabuni au nyumbani kwake. Inapigwa ya chap-chap ikibidi nyingine inahifadhiwa kwenye gudulia la lita tano na kufichwa machaka hadi jioni kitu inaibukiwa. Ili wewmuuza uendelee kuipata hela ya wanafunzi lazima uwe na sifa ya kuwaficha wateja wako(wanafunzi) wanapokuja. Maana wakikamatwa suspension au kufukuzwa.Pia shule ilikuwa inamiliki kilabu cha pombe za wenyeji kwa ajili ya staff wake.
 
Duuh! Jamaa inaonekana umepta pale kipajini long tyme xna kaka,kuna changez kubwa sana nowdayz,me nimemalza pale 2010 form6 pgm,afu hyo mandela annex haionekani,instead ni old mandela!
 
Kweli Tosa Hill inatukumbusha mbali sana!!!!!!!!! Lakini hizo picha ni baada ya Muungano kuwa Mandela, pia assembly ilikuwa ikifanyika next to the Basket ball ground tofauti na ilivyo ktk picha ambapo ni mbele ya ofisi za waalimu. Na enzi zetu sisi wengine, Muungano ilikuwa roofed kwa tiles wakati Azimio na Mwenge hayakuwa yameezekwa kwa bati.
 
Hakuna furaha kama kukumbuka ulikotoka tulikuwa tunakula bondo (ugali) na ndondo (maharage) mchana / jioni x 7 x 4. mpaka kuna jamaa walidiriki kusema siku wakiwa na familia zao watapiga marufuku ugali na maharage (sijui wamefanya hivyo). siku moja alipita kutusalimu Kamishna wa elimu ya shule za sekondari toka Wizarani RIP Mzee Alexander Ndeki akatutia moyo eti tuna bahati sana kwani wao wamewahi kula ugali kitoweo kikiwa uji (imagine).
Kule Mandela no 89 kuna jamaa walikuwa hawali chakula cha shule wako full kila kitu, walikamatwa siku moja wana -temper na jiko la umeme wakapewa suspension mpaka siku ya mtihani.
Nilikaa Ujamaa room no 14 nikijulikana kama COWI (Computer Wizard) kisa wakati huo wengi wakiwa hawajui computer mimi nilikuwa nafahamu vizuri MOUSE (wakati huo ni MS-DOS Kisha Window 95) story zangu nyingi zilihusu computer mengine nilikuwa nawadanganya si unajua nimetoka Dar kwa hiyo waliotoka Lupembe lwa Senga hakuna kubisha, teh teh teh leteni story Jamani ila nasikitika pia HP wetu wakati huo RIP Ayoub Zuber amefariki miaka kama mitatu sasa imepita.
 
Sinagogi, kila jioni 1.00-1.30 UKWATA, halafu kuna ratiba ya IPYA.TYCS waliingia kanisani.THISDASO walitumia darasa fulani huku nyuma ya Mandela dom sasa wanakuita Mandela annex. Moja kwa moja, wewe O level ulifundishwa na Sanga ASK na A level ulifundishwa na Sanga N.Ulivipata vitisho vya Dudu na mnyoosho wa Contra. Bila kusahau kuibiwa na Pimbi.


ni kweli kabisa mnyamahodzo, nimekugongea thanks ya live
 
Enzi za Marehemu Mpogole "DUDU"

Mkuu tulikuwa darasa moja! Usiuliuze combination ukaconnect dots

kabla ya kufanya mitihani nadhani ilikuwa May 1990, Dudu alikuwa anachechemea sana nami niliugua sana na ikagundulika nilikuwa na Appendecitis ikabidi nifanyiwe operation. Washikaji walikuwa wakija kunicheck wananiambia Mchungaji wewe uko kwenye selection lol! Nilikuwa naogopa sana, bahati akaja kufa yule dogo Vandu Makoko RIP!

Homeboy, huyu "DUDU" alikuwa balaa. Ilijulikana kwamba ukiona mguu wake unauma (yaani anachechemea zaidi) ni dalili kuwa kuna mwanafunzi lazima afe. Baada ya kutoka Tosamaganga alikuja Mkwawa. Na kweli kuna kipindi mguu ulimuuma na mwanafunzi mmoja alikufa. Sasa sijuwi kama ilikuwa coincidence au ni kweli. Waliokuwa Tosamaganga waseme zaidi maana Mkwawa hakukaa muda mrefu.
 
inatia raha sana unapokumbushwa sehemu ulizopitia those days.....nilikuwepo hapa '93 to '96
nawakumbuka sana walimu wangu especially Mr Ugulumu(namheshimu sana,alinijenga sana kihesabu kwa kauli mbiu ya Mathematics is by doing!!!)Sanga ASK-geography,Mazege &mrs Mazege-Chemistry and Add maths resp,Kiondo-Biology,Sigimba-kiswahili....duhhhhh
kuna sister alikuwa anatufundisha kiinglishi alikuwa na matusi huyooooo dunia nzima(aliwahi kumuambia mtu kuwa una miguu kama ya mbu na akamuambia kama umekosa dekio si ungetoa li...r. lako uliburute lisafishe darasa, mimi aliwahi kuniambia wewe hujui kabisa kiinglishi najitahidi tu ili usiniongezee idadi ya Fs ila thanks God nilipata B ),mofuga alinifundisha Livestocking,tolley na wengine wengi kwa maana Tosa walimu tulijaaliwa walikuwepo wengi sana.

Secondmaster wetu alikuwa Contra...duh mzee alinichapa fimbo sita na kuniregister blackbook kisa nimesababisha mche wa mti kufa kwenye kiunga nilichopangiwa, wapambe sasa....!wakati mie nachapwa majirani wangu kwenye kiunga cha usafi wakasogea karibu na alipomaliza kunipa dozi akawageukia wao na kuwaambia kila siku nasisitiza mtu akikosea lazima mmuonye na akikaidi mtoe taarifa mbona hakuna aliyetoa taarifa ya kufa kwa mche huu? basi bana akawaunganisha kwenye kosa langu na kuwalamba stick sitasita pia na kuwaingiza blackbook na tukaongezewa adhabu ya kwenda maliasili mjini kununua mche mwingine kwa gharama zetu na muda wetu...mwe what a punishment!!!kosa langu lilirekodiwa kama ''destroying public properties'' i wish huyu jamaa angekuwa waziri mkuu labda public funds zingesalimika.....


sadly nasi tulimpoteza mwenzetu mmoja tukiwa 4m4,ilituuma sana.......

kuna mengi ya kukumbuka Tosa.....ntaenda tena kutembea na familia yangu....i like the place kwa kweli.
 
Umetukumbusha mbali sana. Navuta kumbukumbu kisha naona yale mabweni- Azimio, Ujamaa, Mapinduzi, Mandela. Madarasa ya CBG, PCB, PCM na EGM. Kisha namwona Zitto Kabwe na mwenzie Twahili Njoki wanaonywa kwa kosa la kuongoza kundi la Skauti lililompiga mwalimu (....nimemsahau jina) usiku alipokatiza eneo la shule akitoka kulewa. Halafu nipo Azimio pale juu nikiiona Halfmaili yetu na ile Club ya Pombe kwa waalimu pale bondeni. Kisha nipo pale juu ulipotundikwa ungo naiona Ipamba yoooote na ile barabara ya kwenda Njiapanda kwenye ulazi. aaaah Tosa_Maganga a.k.a Tupa_Mawe
 
inatia raha sana unapokumbushwa sehemu ulizopitia those days.....nilikuwepo hapa '93 to '96
nawakumbuka sana walimu wangu especially Mr Ugulumu(namheshimu sana,alinijenga sana kihesabu kwa kauli mbiu ya Mathematics is by doing!!!)Sanga ASK-geography,Mazege &mrs Mazege-Chemistry and Add maths resp,Kiondo-Biology,Sigimba-kiswahili....duhhhhh
kuna sister alikuwa anatufundisha kiinglishi alikuwa na matusi huyooooo dunia nzima(aliwahi kumuambia mtu kuwa una miguu kama ya mbu na akamuambia kama umekosa dekio si ungetoa li...r. lako uliburute lisafishe darasa, mimi aliwahi kuniambia wewe hujui kabisa kiinglishi najitahidi tu ili usiniongezee idadi ya Fs ila thanks God nilipata B ),mofuga alinifundisha Livestocking,tolley na wengine wengi kwa maana Tosa walimu tulijaaliwa walikuwepo wengi sana.

Secondmaster wetu alikuwa Contra...duh mzee alinichapa fimbo sita na kuniregister blackbook kisa nimesababisha mche wa mti kufa kwenye kiunga nilichopangiwa, wapambe sasa....!wakati mie nachapwa majirani wangu kwenye kiunga cha usafi wakasogea karibu na alipomaliza kunipa dozi akawageukia wao na kuwaambia kila siku nasisitiza mtu akikosea lazima mmuonye na akikaidi mtoe taarifa mbona hakuna aliyetoa taarifa ya kufa kwa mche huu? basi bana akawaunganisha kwenye kosa langu na kuwalamba stick sitasita pia na kuwaingiza blackbook na tukaongezewa adhabu ya kwenda maliasili mjini kununua mche mwingine kwa gharama zetu na muda wetu...mwe what a punishment!!!kosa langu lilirekodiwa kama ''destroying public properties'' i wish huyu jamaa angekuwa waziri mkuu labda public funds zingesalimika.....


sadly nasi tulimpoteza mwenzetu mmoja tukiwa 4m4,ilituuma sana.......

kuna mengi ya kukumbuka Tosa.....ntaenda tena kutembea na familia yangu....i like the place kwa kweli.

Anaitwa Sister Mdalingwa.
 
Back
Top Bottom