Tuliosoma Shule ya Sekondari Tosamaganga tukutane hapa

Umenikumbusha mbali sana mpendwa. Nilikuwa Tosamanga kati ya mwaka 1983-1985. Namkumbuka headmaster wakati huo Mr. Mpogole maarufu kwa jina la DUDU!
 
Acha kudanganya watu hapo penye nyekundu.

Kwanza Mkwawa hakumuua Zelewisky aka Nyundo kwa mikono yake, bali aliuliwa na majeshi ya Mkwawa.

Pili, Nyundo aliuliwa eneo la Lundamatwe karibu Ilula (mpaka leo mnara wa kaburi lake upo just about 20 mts away from Moro-Irg road). Lundamatwe kuna umbali mkubwa sana hadi Tosa.

Tatu, mapigano yaliyohusisha mlima huo (kabla haujaitwa Tosamaganga) kati ya Mkwawa na wajerumani siyo zamu hiyo aliyokuwepo Nyundo.

Naweka sawa tu, tuendelee na mada.
Sawasawa nimekosea,nilivyomwelewa guide tulipoenda kalenga,alizungumzia mapigano karibu na ipamba,lakini inaonekana siku zote nilikuwa misinformed au sikuilewa hadithi....I know now!! haibani sana.
 
Mkuu Kakaruvi,

Asante kwa Kunikumbusha juu ya Tosa Hill, binafsi nakumbuka yafuatayo:

* Nilikuwa pale toka 1988 hadi 1990,
* Nilikuwa nachukua PCM, darasa langu lilikuwa PCM 3,
* Nilishawahi kutembea mara nyingi sana toka njia panda lami (Tanangozi) hadi Tosamaganga,
* Nakumbuka Dansi lililopigwa pale Iringa Girls (Feb-1990) kwaajili ya kukusanya fedha za kujenga madarasa ya F5 na F6, duu ilikuwa balaa kwani TANCUT Almasi, ndo walitumbuiza pale!
* Nakumbuka Mwl. Pimbi(nick name) huyu alikuwa Mwl wa O-level, na alikuwa mnoko mno hasa kwa A-level,
* Nakumbuka pia CONSTANT (fimbo sita), ulikuwa ukiambiwa constant basi ujue ni bakora sita!
* Mwisho, nakumbuka Quarter Mile na Half Mile.
* Headmaster Dudu Mpogole(RIP), alitisha kama Ukoma!!
Usisahau SELECTION.
 
ahsante kwa kutuwekea hii kitu hapa jamvin......nimekumbuka mbali sana hasa kitimoto ya pale IPAMBA.
Duh!! Umenikumbusha mbali. Ilikuwa ikifika Ijumaa jioni mnafanya mchango. Jumamosi anatumwa mtu kwenda Msiwasi au Ipamba kununua kitimoto, nyanya na vitunguu. Ngoma inakuja kukaangiwa msitu wa nyuma ya PCM block (ambalo pia kulikuwa Biology Lab) au ule wa chini ya nyumba ya h/master. Ngoma inaletwa bwenini imekwisha ungwa ama mnaishukia na bonge ya sima ya ugali huko huko kwa msitu utafikiri wapasua mbao misituni.
 
Du jamani nami mumenigusa, nilikua hapo 1986-1988, namkumbuka mwl mgunja, da jamaa alikua anacharaza viboko ni balaa, kulikua na mwl mrusi wa physics [velichko] jamaa kumbe lilikua shushushu lilipewa notice 24hrs likarudishwa kwao, aisee mdau hongera kwa kumbukumbu nzuri. Hii picha ya pili hapo juu[ hapo assembly] kama sikosei ni mwaka 1988, John vocent mnaemzungumzia sio yule kipanga wa hesabu ?
 
Du jamani nami mumenigusa, nilikua hapo 1986-1988, namkumbuka mwl mgunja, da jamaa alikua anacharaza viboko ni balaa, kulikua na mwl mrusi wa physics [velichko] jamaa kumbe lilikua shushushu lilipewa notice 24hrs likarudishwa kwao, aisee mdau hongera kwa kumbukumbu nzuri. Hii picha ya pili hapo juu[ hapo assembly] kama sikosei ni mwaka 1988, John vocent mnaemzungumzia sio yule kipanga wa hesabu ?

Yeah! Ndiye huyo.....Mgunya alienda kuwa Headmaster shule fulani mikoa ya kusini....Kuna siku alinikimbiza kwa Manurse wa Ipamba....lol....
 
Kaka acha kunivunja mbavu, mwl Mgunja alikua akikukuta ipamba hakika umekwisha, nawakumbuka punk boy [Probe] na Hemedi [KARATE MAN] JG, hv kamanda Siro nae pia si alikua tosa miaka ile kama sikosei, lete majina ya wengine
 
Mchungaji masa kwa sasa na sera za ccm jinsi ilivyo sitashangaa hii shule wakaigeuza university maana duh??
 
Kama ilivyo Mazengo-St John Univ.ya anglican church, Tosa pia inapaswa warudishiwe wenyewe iwe Chuo Kikuu au warudishie ili iendelezwe zaidi.
 
Mchungaji Masa, nawewe enzi hizo ulikuwa unakwenda kwa manesi wanafunzi, kozi ya mwaka mmoja? Ukimkosa jioni basi utavunga unaumwa sana ili yule nesi wa shuleni(RMA) akupe kibali cha kwenda Ipamba. Ukifika Ipamba....mgonjwa ktk mawindo so strategic....duh!
 
Tosa boys who were Dudu's sons, mnakumbuka ile habari ya kuwa Dudu alikuwa anakula watoto wake (mwanafunzi) kila mwaka?
Mnakumbuka jamaa alivyokuwa anatisha?
 
Inanikumbusha mbali sana, wadau mliopitia hapo mpooooo!

View attachment 31724

Baada ya miaka mitano hayo majengo yatakuwa magofu. Mwajua kuwa toka DANIDA school maintanace project ilivyokwisha serikali haijatoa hata senti moja kukarabati majengo ya mashule sio tosa tu ila shule zote za serikali.

Angalia Shule ya Tambaza inavyotia kichefuchefu na hiyo iko mjini Pugu na Minaki hoi sana, sasa za mikoani zikoje?

Wadau chukueni tahadhari
 
Yaani hapo mmenikonga sana tu... Nilikuwa Tosa tangu 2002-2004 may... Mkangwa anatoka na akaingia Mzee wa cigarette(CHARWE-Mungu ailaze mahali pema peponi roho yake)... Mwenge ndio Home kwa Tosa.... Maisha Yale yana utamu wake jamani hasa ukifika Ipamba basii whaooo ukiwaona wanafunzi wa Nursing unaenjoy....
 
Mnaficha majina balaa.... 2004 form 6 ndio nimetoka tosa,it was gud time
 
Tosa boys who were Dudu's sons, mnakumbuka ile habari ya kuwa Dudu alikuwa anakula watoto wake (mwanafunzi) kila mwaka?
Mnakumbuka jamaa alivyokuwa anatisha?

Mkuu,

Hapo kwenye bluu, unanikumbusha jinsi alivyofariki kiajabu-ajabu kijana wa Mh. Horace Kolimba(RIP) aliyekuwa akiitwa VANDU MAKOKO. Kijana huyu aliyekuwa kidato cha pili wakati huo alifariki mapema 1990 wakati sisi tukiwa SIX, duu msiba huu ulitikisa Shule!
 
Back
Top Bottom