Tuliooa kwa mahari ndogo tuje tuseme lolote juu ya jambo letu hili

Kupewa mke bila mahari au mahari Kiduchu ni Mtego mkubwa
Wakati naoa niliomba wazee waende ukweni kwa mzee Macha ili waeleze nia ya kijana wao na kupewa taratibu za mahari.

Kichwani kwangu nilikuwa nawaza hiyo list ya mahari maana mzee alikuwa jeuri na binti amemsomesha. Wazee wakaambiwa njooni mwezi ujao na huyo kijana niwatajie mahari, tulipofika mzee akaita binti yake, Mankaaaaa njoo hapa! Mzee akamuuliza Unamjua huyu kijana? Umempenda mwenyewe? Manka akajibu ndio baba. Mzee akaniambia kijana kama mmependana nawapa baraka mkaishi vizuri hayo Ndio mahari.

Sasa ni Mtego Kwasababu ukweni wakikohoa tu Nimeshafika kwa jinsi ninavyowaheshimu na kuwapenda, yaani niko frontline utadhani mimi mtoto wao wa kiume.
Kiherehere chako tu...
 
Chief! MUNGU hajawahi kuweka ukomo wa idadi ya wanawake wa kuoa, aliliacha suala hilo mikononi mwetu,
Huu ulioandika ni uongo wa wazi. Kila mitume na sheria zao, hao ulio ona wameoa wake zaidi ya wanne sheria yao iliwaruhusu, na ukomo wa idadi ya Wanawake kuoa ni wanne kwa sheria ya umma huu, hakuna zaidi ya hapo.

Naomba unithibitishie ya kuwa idadi ya wake wanne sheria hii imetungwa wanadamu au mwanadamu ?
 
Huu ulioandika ni uongo wa wazi. Kila mitume na sheria zao, hao ulio ona wameoa wake zaidi ya wanne sheria yao iliwaruhusu, na ukomo wa idadi ya Wanawake kuoa ni wanne kwa sheria ya umma huu, hakuna zaidi ya hapo.

Naomba unithibitishie ya kuwa idadi ya wake wanne sheria hii imetungwa wanadamu au mwanadamu ?
Chief! Punguza hasira, maana unauliza swali halafu unajijibu mwenyewe (Hii yote ni kwa ajili ya hasira tu). Mimi siyo muongo kwa maana MUNGU hajawahi kutunga sheria(Na hawezi kufanya hivyo) yeye alitoa amri kumi tu (zipo ndani ya torati) na katika amri zote hizo hakuna amri iliyoweka ukomo wa kuoa.

Upo sahihi kuwa sheria ziliwekwa na wanadamu (siyo MUNGU) ili kurahisisha utawala na zinabadilika kulingana na aina ya utawala uliopo. Enzi za mtume MOHAMMAD S.A.W kuna mfuasi wake mmoja alimuuliza swali kwamba ni idadi gani ya wanawake wanaruhusiwa kuoa. Mtume alijibu kwa kusema "Hata wanne" (neno "nne" ndio lililomjia akilini kwa wakati huo). Baada Mtume MOHAMMAD S.A.W kwenda zake, waliobaki ndio wakagongelea msumari kwenye "NNE" na hatimaye kuifanya kuwa sheria.

Sasa naomba unitafutie maana ya neno "Hata" kwa kiarabu lina maanisha nini? (Ikiwa linamaanisha "Mwisho" basi nitakubaliana na wewe lakini kama halimaanishi hivyo kubali kuwa MUNGU hajaweka ukomo wa kuoa bali aliliacha kwetu tuamue wenyewe. Hata hawa walioamua kuwa na ndoa ya mke mmoja ni sheria za wanadamu (kupitia kanisa) lakini MUNGU hajakataza, Hata Mapadre wa Kikatoliki kutooa na Watawa (Sisters) kutoolewa nazo pia ni sheria za wanadamu kupitia Kanisa lakini wala siyo maagizo ya MUNGU.
 
Chief! Punguza hasira, maana unauliza swali halafu unajijibu mwenyewe (Hii yote ni kwa ajili ya hasira tu). Mimi siyo muongo kwa maana MUNGU hajawahi kutunga sheria(Na hawezi kufanya hivyo) yeye alitoa amri kumi tu (zipo ndani ya torati) na katika amri zote hizo hakuna amri iliyoweka ukomo wa kuoa.
Hakuna hasira hapo, nimekupa stahiki yako. Ni uchachefu wa maarifa kusema Mola hajatunga sheria bali alitoa amri, sasa nitakuuliza hili umelipata wapi ? Nimekuomba uthibitishe ya kuwa mwanadamu ametunga hizo sheria katika hizo dini, hujafanya hilo.
Upo sahihi kuwa sheria ziliwekwa na wanadamu (siyo MUNGU)
Hakuna sehemu niliyosema ya kuwa sheria zimewekwa na mwanadamu, hili umedai wewe, na umeshindwa kulithibitisha. Unatakiwa kutuliza akili na kuongeza umakini ili usizulie watu uongo.

Sheria ndiyo amri kijana,ndiyo maana kila nabii alikuwa na sheria zake kulingana na haja, lakini Mola gani awaumbe waja wake bila kuwawekea sheria za kuwaongoza ? Hili akili inakataa.
Enzi za mtume MOHAMMAD S.A.W kuna mfuasi wake mmoja alimuuliza swali kwamba ni idadi gani ya wanawake wanaruhusiwa kuoa. Mtume alijibu kwa kusema "Hata wanne" (neno "nne" ndio lililomjia akilini kwa wakati huo). Baada Mtume MOHAMMAD S.A.W kwenda zake, waliobaki ndio wakagongelea msumari kwenye "NNE" na hatimaye kuifanya kuwa sheria.
Kwanza unatakiwa utuwekee marejeo ya hiki ulichokisema tunakipata katika kitabu gani.

Pili, mtume haongei kwa matamanio yake isipokuwa ni Wahayi toka kwa Allah aliyejuu.

Tamko Hata ni tamko lenye kuonyesha sharti katika kujibu swali na huonyesha ukomo kadhalika, yaani "mpaka wanne".
 
Walitaka laki tisa plus mazagazaga kama kofia ,koti, mtoto wa kike akataka dressing table

Nikawaambia sawa nilipogeuza hawakuniona tena na mtoto wao nilimchana hiyo hela sina labda elfu 50 ila baadaye nikaamua nimpige chini huyu atanisumbua mpka leo ananilaani eti nimemleta uchuro eti nimekuja kutoa posa bila kuoa

Nakubaliana na kulipa mahari ila sio kwa kukomoana maana hata sisi tuna thamani kwa wazazi wetu
sio vzr ulichofanya
 
Sijui kwanini sijui wanakuwa kama wamekuuzia kitu eti mara ng'ombe mbili,, mara milion moja na laki tano jamani hizi hela hatuokoti kwani hawaoni kama nimewapunguzia mzigo wa kutunza mtoto wao
 
Sijui kwanini sijui wanakuwa kama wamekuuzia kitu eti mara ng'ombe mbili,, mara milion moja na laki tano jamani hizi hela hatuokoti kwani hawaoni kama nimewapunguzia mzigo wa kutunza mtoto wao
Ndugu nikwel ila shukuru kuoa Tanzania atupigani mzinga mikubwa mikubwa, nenda kwa wenzetu Kenya mahari unaweza kujengea nyumba bongo. Wao wanakupigia gharama zote za kuanzia anasoma had hapo alipo
 
Ila Uislamu ni raha asikudanganye mtu, nilifunga ndoa pamoja na mahari kwa shillingi 70,000 ukijumulisha pamoja na usafiri.......sasa ni mwaka wa 9 watoto watatu, nyumba tumejenga gari tunazo mahaba tunayo pia
Mahaba umeyataja mwishoni inaonekana yakumulika kwa tochi
 
Walitaka laki tisa plus mazagazaga kama kofia ,koti, mtoto wa kike akataka dressing table

Nikawaambia sawa nilipogeuza hawakuniona tena na mtoto wao nilimchana hiyo hela sina labda elfu 50 ila baadaye nikaamua nimpige chini huyu atanisumbua mpka leo ananilaani eti nimemleta uchuro eti nimekuja kutoa posa bila kuoa

Nakubaliana na kulipa mahari ila sio kwa kukomoana maana hata sisi tuna thamani kwa wazazi wetu
Dah! 😝😝😝😝 nimecheka sana
 
Back
Top Bottom