Tuliomkataa Lowassa, Makuwadi wa Mabadiliko "Yale" na Waliojipanga Nyuma Kosa Letu Nini?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
Hivi ni kweli kuwa watu wote tunaopenda mabadiliko tulitakiwa tupige magoti mbele ya Lowassa na kumuunga mkono? Watu wote ambao tulikuwa tunaunga mkono upinzani kwamba tulitakiwa alipotangazwa Lowassa na alipoungana na kina Kingune na Sumaye, Masha na wengine sote tulitakiwa - ili kuonesha kuwa tunamaanisha kweli tunataka mabadiliko - basi tuunge mkono. Na kama kupinga basi tulitakiwa tupinge kimoyo moyo tusipinge hadharani?

Kwamba, kwa vile tuliikosoa CCM - na wengine bado tutaendelea kufanya hivyo bila kuangalia nyuso zao - basi tulitakiwa (ili kupata uhalali mbele ya wengine) tumkubali Lowassa , makuwadi wake (natumia neno kuwadi jinsi wao wanavyotumia neno wasaliti kututaja tuliomkataa Lowassa) na tuimbe sifa kwa kuzungurusha mikono "Mabadiliko Lowassa, Lowassa Mabadiliko"?

Hivi ina maana sasa hivi wapinzani wa kweli na wenye mawazo ya kweli ya kuleta mabadiliko ni wale waliompokea na kumuuza Lowassa kwa wananchi kiasi kwamba yeyote aliyeenda kinyume cha Lowassa basi amekuwa msaliti wa "mabadiliko yale".

Hivi hawajui kuwa Watanzania walichokataa siyo mabadiliko yaliyoahidiwa bali yaliyoshuhudiwa? Sasa leo wenzetu inaonekana katika kilichoitwa "mahaba" hawajakubali kabisa walifanya makosa na matokeo yake wanafikiria wengine wote tulikosea kumkataa Lowassa na makadokado yake isipokuwa wao? Wanatushangaa kwanini hatukupiga magoti na kutoa sadaka za sifa kwenye madhabahu ya Lowassa.

Well, jibu langu ni rahisi tu. Kila mtu anaishi kwa ukuu wa dhamira yake. Wenzetu mliamini Mabadiliko ni Lowassa na bila ya yeye haiwezekani kuwa na mabadiliko sisi wengine tuliamin mabadiliko yanwezekana hata bila Lowassa.

Sasa kosa letu hapa nini? Kwamba tulitakiwa kama tunampinga Lowassa basi tusijioneshe waziwazi kwa vile tuliipinga CCM ambayo Lowassa alikuwa ni mmoja wa waumini na mtumishi wake wa muda mrefu? Kama wenzetu mmeamua kutetea mabadiliko yale ya Lowassa kiasi kwamba hamtaki au hamko tayari kuona mabadiliko tuliyoyapigania sisi wengine yanawezekana na yanafaa kwa taifa sioni tatizo; ni haki yenu na ninaamini wala haipunguzii uzalendo au utu wenu kama Watanzania. Naamini, mmefanya hivyo mkiwa na nia na moyo safi wa uzalendo -hata kama umepotoshwa!

Na sisi wengine tuna haki hiyo hiyo ambayo wengine mnafikiria kuwa ni himaya yenu; tuna haki ya kuchagua upande ule ambao tunaamini katika dhamira safi unawakilisha mabadiliko tuyakatayo. Katika hili hatuna wa kumwomba radhi au kujipendekeza kwake.

MMM
 
Mmm utaandika sana ila comment umeziona wewe usemi ubaya wa ccm na umafia wenu
 
Duh!

Maskini Lowassa!

Licha ya kuwa uchaguzi ushaisha lakini bado tu watu mmemkomalia koo!

Kwa nini?

Kuna nini kingine ambacho labda wengi wetu hatukijui?

Manake tayari huyo mtu hawezi kuja kuwa rais wa Tanzania.

Sasa yote haya ya nini?

Things that make you go hmmm......
 
Sema na ubaya wa ccm maana umafia wa ilala na umafia wa kinondoni ujawahi kuusema sasa Ndio nchi nzima ulifanyika
 
Tatizo la nchi hii ni mfumo mbaya wa ccm..
hakuna wa kuleta mabadili ya mfumo ndani ya ccm..bila shaka umeona hata juhudi za magufuli zimeanza kufifia baada ya kubanwa na wenye chama kawarudisha hakina muhongo..

ata kikwete alikuwa mzuri mwanzoni lakini kilichotokea kila mtu anajua.. magufuri atamaliza vibaya kuliko kikwete maana shida ni mfumo ndio maana tuliyaunpa mkono mabadiliko ya Lowassa
 
Walisema Tanzania itauza umeme nje,jana waziri Muhongo kasema Tanzania itanunua umeme Ethiopia sasa sijui ni deal ya Lowassa haa haaa CCM ni ile ile.
 
Tatizo sio kumkataa,tatizo ni sababu za kumkataa mnazotoa,ukilinganisha na sababu za upande unaoukubali.Ndiyo hasa makandokando yako yalipo.
 
Duh!

Maskini Lowassa!

Licha ya kuwa uchaguzi ushaisha lakini bado tu watu mmemkomalia koo!

Kwa nini?

Kuna nini kingine ambacho labda wengi wetu hatukijui?

Manake tayari huyo mtu hawezi kuja kuwa rais wa Tanzania.

Sasa yote haya ya nini?

Things that make you go hmmm......

NN, binafsi wala sina sababu ya kumzungumzia huyu lakini wao wenyewe (waliomtaka Lowassa na mabadiliko yake) hawataki tuamini uchaguzi umekwisha. Lowassa mwenyewe haamini uchaguzi umekwisha na as a matter of fact inaonekana anadai Magufuli ni impostor. Na wapo wengine ambao hawaamini kuwa Magufuli ameshinda kihalali na hivyo wanamvumilia kwa sababu hawana namna nyingine. Sasa kama wao hawajaamini na kukubali uchaguzi umekwisha na mshindi kapatikana (kwa halali au la) na wanataka sisi wengine tujisikie vibaya kwa vile tulimpinga mtu wao tunatakiwa kufanya nini? kukubali na kuinamisha vichwa kwa haya au kuwaomba radhi kwamba "samahani jamani kwa kumkataa Lowassa wenu" halafu yaishe. Au tunawajibu wa kutetea dhamira zetu kuwa tulikuwa sahihi?
 
Umeulizwa issue ya umeya Ilala au nao kagombea lowasa.
Mbona kukemea CCM umeacha? Issue ya Makonda na Kubenea mbona husemi? Si lazima uandike makala lkn mtu anavyokutag na kukuuliza mbona hujibu? Bifu yako na Lowassa si ilianzia alivyokuchunia interview sasa mbona nawe hujibu simple questions.
 
Huyo ndo imetoka hiyo.

Hata akigombea tena atashindwa tu.

Binafsi sioni sababu yoyote ile ya kuendelea kumjadili mtu ambaye si 'relevant' kivile.

Huwezi jua,wapinzani huwa wanapanda graph kutokana na serikali kushindwa kufanya kazi,hizi bwembwe za serikali hii itafanya watu wasahau upinzani kwa mda ila wakizoeleka na kuboronga upinzani utarudi kwenye ulingo
 
Tatizo la nchi hii ni mfumo mbaya wa ccm..
hakuna wa kuleta mabadili ya mfumo ndani ya ccm..bila shaka umeona hata juhudi za magufuli zimeanza kufifia baada ya kubanwa na wenye chama kawarudisha hakina muhongo..

ata kikwete alikuwa mzuri mwanzoni lakini kilichotokea kila mtu anajua.. magufuri atamaliza vibaya kuliko kikwete maana shida ni mfumo ndio maana tuliyaunpa mkono mabadiliko ya Lowassa

Mfumo ni kitu gani ndugu naomba ufafanuzi wa dhati kwa hilo
 
Hivi ni kweli kuwa watu wote tunaopenda mabadiliko tulitakiwa tupige magoti mbele ya Lowassa na kumuunga mkono? Watu wote ambao tulikuwa tunaunga mkono upinzani kwamba tulitakiwa alipotangazwa Lowassa na alipoungana na kina Kingune na Sumaye, Masha na wengine sote tulitakiwa - ili kuonesha kuwa tunamaanisha kweli tunataka mabadiliko - basi tuunge mkono. Na kama kupinga basi tulitakiwa tupinge kimoyo moyo tusipinge hadharani?

Kwamba, kwa vile tuliikosoa CCM - na wengine bado tutaendelea kufanya hivyo bila kuangalia nyuso zao - basi tulitakiwa (ili kupata uhalali mbele ya wengine) tumkubali Lowassa , makuwadi wake (natumia neno kuwadi jinsi wao wanavyotumia neno wasaliti kututaja tuliomkataa Lowassa) na tuimbe sifa kwa kuzungurusha mikono "Mabadiliko Lowassa, Lowassa Mabadiliko"?

Hivi ina maana sasa hivi wapinzani wa kweli na wenye mawazo ya kweli ya kuleta mabadiliko ni wale waliompokea na kumuuza Lowassa kwa wananchi kiasi kwamba yeyote aliyeenda kinyume cha Lowassa basi amekuwa msaliti wa "mabadiliko yale".

Hivi hawajui kuwa Watanzania walichokataa siyo mabadiliko yaliyoahidiwa bali yaliyoshuhudiwa? Sasa leo wenzetu inaonekana katika kilichoitwa "mahaba" hawajakubali kabisa walifanya makosa na matokeo yake wanafikiria wengine wote tulikosea kumkataa Lowassa na makadokado yake isipokuwa wao? Wanatushangaa kwanini hatukupiga magoti na kutoa sadaka za sifa kwenye madhabahu ya Lowassa.

Well, jibu langu ni rahisi tu. Kila mtu anaishi kwa ukuu wa dhamira yake. Wenzetu mliamini Mabadiliko ni Lowassa na bila ya yeye haiwezekani kuwa na mabadiliko sisi wengine tuliamin mabadiliko yanwezekana hata bila Lowassa.

Sasa kosa letu hapa nini? Kwamba tulitakiwa kama tunampinga Lowassa basi tusijioneshe waziwazi kwa vile tuliipinga CCM ambayo Lowassa alikuwa ni mmoja wa waumini na mtumishi wake wa muda mrefu? Kama wenzetu mmeamua kutetea mabadiliko yale ya Lowassa kiasi kwamba hamtaki au hamko tayari kuona mabadiliko tuliyoyapigania sisi wengine yanawezekana na yanafaa kwa taifa sioni tatizo; ni haki yenu na ninaamini wala haipunguzii uzalendo au utu wenu kama Watanzania. Naamini, mmefanya hivyo mkiwa na nia na moyo safi wa uzalendo -hata kama umepotoshwa!

Na sisi wengine tuna haki hiyo hiyo ambayo wengine mnafikiria kuwa ni himaya yenu; tuna haki ya kuchagua upande ule ambao tunaamini katika dhamira safi unawakilisha mabadiliko tuyakatayo. Katika hili hatuna wa kumwomba radhi au kujipendekeza kwake.

MMM

Mpinzani wa kweli ni lazima Stoke ndani ya ccm, so lowassa kwangu ndiye mpinzani wa kweli.......!!!!!
 
Huwezi jua,wapinzani huwa wanapanda graph kutokana na serikali kushindwa kufanya kazi,hizi bwembwe za serikali hii itafanya watu wasahau upinzani kwa mda ila wakizoeleka na kuboronga upinzani utarudi kwenye ulingo

Definitely wataboronga maana expectation za watu ni kubwa mno na hivyo watachemka tu. Hata upinzani tungechukua bado tusingemeet expectations hizo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom