Azizi Mussa
JF-Expert Member
- May 9, 2012
- 9,172
- 7,428
Nadhani kwa wale miongoni mwetu ambao tulikuwa na misheni ya kumfitinisha na kuhakikisha tuna mchonganisha Zitto kwa kuwango kikubwa Kadiri iwezekanavyo, ni dhahiri kwmamba mkakati wetu haujafanikiwa vizuri hivyo ni bora tukauacha na kufanya mambo mengine ya kujenga nchi yetu.
Ni dhahiri kwamba miongoni mwetu tulijaribu kumpaka Zitto matope mwili mzima tukidhani tushamchafua na ataonekana hivyo, lakini tulisahau kwamba tulikuwa tunatumia udongo wa Dar es salaam, udongo wenye asili ya mchanga ambao ukikauka kidogo tu huachia wenyewe na kudondoka chini. na kumuacha muhusika na vijimchanga mchanga tu;Ndicho kilichotokea kwa wale tuliokuwa tukimchafua jamaa wa watu.
Hata hivyo sio lazima kuacha kuendelea kumchafua.Kama mtu ana dhamira ya dhati kutoka moyoni kabisa ya kuendelea kumchafua, anaweza kuendelea kufanya hivyo huku akijua malipo ya ubaya aibu!.Ni nani basi anayeweza kuizuia hulka ambayo mwanadamu kapewa na muumba wake ya "Free will"?
Kwa wale watakaoamua kuendelea kumchafua jamaa wa watu (kwa kuwa tu ! wamedhamiria kweli kweli) nawashauri safari hii wasimpake matope maana mbinu hii inaonekana haija fanikiwa kabisa.Chakufanya wampake maji yaliyooshea samaki wabichi huenda akabaki na shombo: Si unajua shombo la samaki!.
Wale wanaokubaliana na mimi kwamba kazi hii ya kuendelea kumfitinisha Zitto kwa sasa hailipi tena, nawashauri kuunganisha nguvu zetu kuwashawishi viongozi wetu wa kitaifa kujenga ofisi ya kisasa ya chama kwa ajili ya makao makuu.Chama kitatakiwa kutafuta kiwanja halafu kila mpenzi wa chama atatakiwa kufikisha tofali moja na sh 1000 eneo la kiwanja (mapendekezo zaidi yanaweza kutolewa), baada ya miezi miwili, ofisi ya maana kabisa itakuwa imepatikana.
Ni dhahiri kwamba miongoni mwetu tulijaribu kumpaka Zitto matope mwili mzima tukidhani tushamchafua na ataonekana hivyo, lakini tulisahau kwamba tulikuwa tunatumia udongo wa Dar es salaam, udongo wenye asili ya mchanga ambao ukikauka kidogo tu huachia wenyewe na kudondoka chini. na kumuacha muhusika na vijimchanga mchanga tu;Ndicho kilichotokea kwa wale tuliokuwa tukimchafua jamaa wa watu.
Hata hivyo sio lazima kuacha kuendelea kumchafua.Kama mtu ana dhamira ya dhati kutoka moyoni kabisa ya kuendelea kumchafua, anaweza kuendelea kufanya hivyo huku akijua malipo ya ubaya aibu!.Ni nani basi anayeweza kuizuia hulka ambayo mwanadamu kapewa na muumba wake ya "Free will"?
Kwa wale watakaoamua kuendelea kumchafua jamaa wa watu (kwa kuwa tu ! wamedhamiria kweli kweli) nawashauri safari hii wasimpake matope maana mbinu hii inaonekana haija fanikiwa kabisa.Chakufanya wampake maji yaliyooshea samaki wabichi huenda akabaki na shombo: Si unajua shombo la samaki!.
Wale wanaokubaliana na mimi kwamba kazi hii ya kuendelea kumfitinisha Zitto kwa sasa hailipi tena, nawashauri kuunganisha nguvu zetu kuwashawishi viongozi wetu wa kitaifa kujenga ofisi ya kisasa ya chama kwa ajili ya makao makuu.Chama kitatakiwa kutafuta kiwanja halafu kila mpenzi wa chama atatakiwa kufikisha tofali moja na sh 1000 eneo la kiwanja (mapendekezo zaidi yanaweza kutolewa), baada ya miezi miwili, ofisi ya maana kabisa itakuwa imepatikana.