Ronal Reagan
JF-Expert Member
- Nov 4, 2010
- 5,299
- 3,055
Mkuu Barafu pole sana. Umeandika kwa uwazi na hisia pia hukupunja.Ni dhahiri kuwa kwa sasa Rais John Pombe Magufuli anajionyesha kuwa katika uongozi wake,suala la majanga na uhai wa wananchi wake hayana vipaumbele.Kwake ni pesa na kuona uchumi unakuwa.Rais wetu tofauti na matarajio yetu,amelinganisha uhai na thamani ya pumzi ya watu wake na uchumi wa nchi,kwake Uchumi kwanza uhai baadae.
Huyu sio Rais ambaye kwa sasa unaweza kutoka mbele ya wafiwa na wahanga wa corona na kuwaeleza kuwa ni Rais wa wanyonge, hata mara maja, abadani haitawezekana kwa sasa. Ni kama mkubwa wetu huyu kayaweka maisha ya watu wake rehani na kuutazama kwanza uchumi na pesa.
Kuna malalamiko mengi juu ya ubovu wa huduma za afya katika sehemu walizotengewa wagonjwa wa COVID-19,anatumia mpaka magazeti ya serikali kueneza propaganda kuwa vifaa tiba vimejaa kila mahali, ukweli ni kuwa, huko Mnazi Mmoja, Amana na Mwananyamala wahudumu wa afya ni kweli wanawakimbia wagonjwa sababu na wao wanaokoa maisha yao kwa kukosa PPE.
Watu wanakufa,watu wanaambukizana na kwa kweli wengine wanaangamia kwa sababu ya kauli za Rais na matendo yake.Hali ni mbaya ndugu zangu,tusisikilize propaganda.
Sasa bila shaka kila mtaa umeanza kukumbwa na vifo vya Corona,juma la jana,familia ya rafiki yangu waliuguliwa na mzee wao kwa ugonjwa wa Corona,wakatoka nyumbani kwenda hospitali ya jirani ya Palestina,huko wakawaambia waende Amana,kufika hapo wakaambiwa wanatakiwa kwenda Buguruni kwa Mnyamani ndio kuna kituo kinashughilikia,kufika Buguruni wakaambiwa waende Mloganzila maana ndio watapata haduma.
Safari yote hiyo mgonjwa hana huduma yoyote,walipofika Mloganzila wakaambiwa hawana huduma yoyote,katikati ya bumbuwazi mgonjwa akafariki bila matibabu,na baadae serikali kuuchukua mwili na kuuzika kwa madai kuwa wamechukua sampuli za maiti na kuona maambukizi,familia nzima sasa ipo karantini.
Ummy Mwalimu na Serikali,iseme sasa,na iseme tena,kwanini kila mahali wagonjwa wanakataliwa??Wagonjwa wetu tupeleke wapi?
Habari mbaya kwangu,na ngumu sana,ni kumpoteza rafiki yangu wa muda mrefu,mwanafunzi wangu na comrade wangu mcheshi,huyu alikuwa rubani wa ndege za TANAPA ambaye amepoteza maisha kwa janga la corona na hayupo hata katika kundi la watu waliotangazwa kuwa wamekufa na ugonjwa huu.Huyu ameondoka na watu kadhaa nyuma yake ambao walimbukizana.Na hao watu wameambukiza wengine...Hali ni mbaya na bado serikali inashindwa kutoa sauti ya kimamlaka kuonyesha kuwa hali ni mbaya.
Marehemu huyu(nahifadhi jina lake) siku kadhaa nyuma tuliwasiliana akienda kuhuisha mambo yake ya leseni za urubani na vibali kadhaa pale mamlaka ya Usafiri wa Anga,na baadae kuwa na training nje ya jiji la Dsm wakiwa na mwenzake na watumishi kadhaa wa mamlaka,maanake alikutana na watumishi hapo mahali,hao watumishi wana familia zao,na hao sehemu ya familia wana jamaa zao wengine makazini na mitaani.
Naambiwa sehemu ya ofisi za Mamlaka hizo watumishi wapo karantini sababu waligusana au kuchangamana na marehemu rafiki mpendwa na mwenzake.
Kwa hali hii,bado serikali imejaa vitisho,haizuii misongamano,haiuzuiii mjii wa Dsm kusongamana katika bars,kumbi za starehe na mikusanyiko mingi.Mji upo wazi kusambaza magonjwa mikoani kwa jina la "Kukuza Uchumi".Huu ni unyama gani?Tunawaza pesa juu ya uhai?
Mgonjwa mmoja wapo kule Rukwa,alitokea Dsm kwa njia ya ndege ya ATCL,akapanda ndege mpaka Mpanda na akasogea mpaka Sumbawanga,hapo kaacha ugonjwa kuanzia kwenye ndege,Mpanda hadi Sumbawanga,maanake alichangamana na abiria wengine,alioambukiza ndio wenye dalili na walio hoi,maanake tamaa za uchumi na pesa,zinafanya tunarusha ndege toka Dsm kwenda Mpanda ili ipeleke ugonjwa ukasambae vijijini kwa masikini na wanyonge.Hao Emirates na wengine walifunga safari sio kwamba hawajui pesa,wanajali uhai wa watu wao.
Hizi ni dalili mbaya za kiuongozi,huu ni uuwaji usiokuwa wa moja kwa moja au ni tuseme wa moja kwa moja.Ni ukosefu wa utu na upendo kwa watu ulioapa kuwalinda ukiwa na katiba kuume na kitabu cha dini kushoto.Wewe baba badilika,okoa watu wako...hiyo ndio kazi tuliokupa kwa njia ya kura.
Sasa ni kama hata data zinapikwa,watu wengi wanakufa,tumeanza kupoteza hata wahudumu wa afya ambao ni askari wetu wa mstari wa mbele...Watumishi wa afya wameanza kufa kwa maambukizi ya kukosa PPE!
Serikali ipo,inaaminisha tutapona kwa mvuke,ni labda kweli,lakini kwanza ilipaswa tuwaambie watu wetu kuwa hali ni mbaya,kukiri kuzidiwa na ugonjwa huu sio udhaifu wa kiuongozi bali ni uimara wa kiuongozi,hii ni kwasababu unawapa watu wako taarifa iliyo kamili na bora.
Sasa barakoa zilizothibitishwa na mamlaka za viwango zinakosa wateja,sababu Rais kaongea hadharani kuwa haziaminiki sababu zinaweza kuwa na virusi.Kazi hii sasa imeachiwa kwa machinga na mafundi cherehani,ambao sasa wanachonga barakoa zisizo thibitishwa ubora wake na mamlaka yoyote.
Si mbaya kuwa na barakoa ya kitambaa,lkn ni hakika kuwa wataalamu wanaeleza kuwa haizuii virusi kwa kiwango hicho zaidi ya kuzuia vumbi tu,lkn haya yote ni sababu ya kauli ya Rais ambayo ina mamlaka ndani yake.
Katika masoko,makanisani na misikitini bado watu wanajazana...Hali ni mbaya,na kwa sababu kwa siku kadhaa serikali imeanza kutaja tu wanaopona kwa idadi kubwa,hatutaji tena vifo,tukidhani kifo ni aubu,kumbe kwa mantiki ya ugonjwa huu wanaopona hata wakiwa 1000,lazima tulie na aliyekufa mmoja,sababu uhai na utu wa mtu una thamani isiyofananishika.Kila mahali sasa watu wamelegeza kufuata kanuni za afya na kujikinga wakiona kuwa wataugua na kupona.
Kuusema ukweli juu ya ugonjwa huu si kuleta hofu,ni kuelezea ukweli na uhalisia wa madhara ya gonjwa hili.Kuficha data sio sifa za uongozi bora,bali ni sifa za uongozi mbovu unaouwa watu wake kwa kufanya "Massaging of data"
Toka mafichoni Rais,wewe ni Amiri Jeshi mkuu,kaa mstari wa mbele...Umekuwa ukivaa magwanda kuonyesha u mwanajeshi,sasa onyesha kwa vitendo...Njoo mbele baba njoo,wasisitize watu wako kuwa hali ni mbaya.
Mikoa iliyoathirika kama Dsm,si lazima uifunge,ruhusu magari ya mizigo na chakula kuingiza na kutoa bidhaa kupeleka mikoani.Hii itasaidia kupunguza maambukizi.
Huwezi kuelewa bandiko hili,mpaka sehemu ya ndugu au jamaa yako afe kwa ugonjwa huu katika mazingira ambayo kuna uzembe mkubwa kutoka kwa watu tuliowapa dhamana...Hii ni ujinga,ni ajabu sana kwanini watu wanashindwa thamini maisha ya watu na wanaona pesa ni bora zaidi.
Zile tambo zote na mikakati mliyotutambia kuwa hii ni serikali mpya,mbana zimefifia??Okoa maisha ya watu wako,pesa makaratasi.
Naungana na kauli na ushauri wako.