thetallest
JF-Expert Member
- Oct 21, 2017
- 8,256
- 9,085
Hakika siku zinakwenda mbio sana na ,ni siku chache sana zimepita toka lile kundi lililojawa furaha isio kifani baada ya aliekua mkuu wa wilaya ya Hai, Sabaya, kupandishwa mahakamani, tabasamu lilikuwa kama lote na Rais Samia kupongezwa na kuambiwa anaupiga mwingi mno.
Ghafla kibao kimegeuka ,Mama Samia kawa mbaya, na anapewa shutuma kibao na wanaomlilia Mbowe, ambaye anatuhuma za kupanga ,kufadhili ugaidi nchini.
Hakika hakuna aijuae dakika moja ijayo kwenye maisha yetu, utulivu ni jambo jema, tusiwe wepesi wa kufurahia madhila ya wenzetu ikiwa sisi hatuijui kesho yetu.
Mwisho, wahenga walinena "Mkuki mtamu kwa nguruwe, kwa binadamu ni mchungu"
Ghafla kibao kimegeuka ,Mama Samia kawa mbaya, na anapewa shutuma kibao na wanaomlilia Mbowe, ambaye anatuhuma za kupanga ,kufadhili ugaidi nchini.
Hakika hakuna aijuae dakika moja ijayo kwenye maisha yetu, utulivu ni jambo jema, tusiwe wepesi wa kufurahia madhila ya wenzetu ikiwa sisi hatuijui kesho yetu.
Mwisho, wahenga walinena "Mkuki mtamu kwa nguruwe, kwa binadamu ni mchungu"