Tulioenda majuu na kurudi home, tukutane hapa tupeane uzoefu, mafanikio na sababu zilizotufanya turudi

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
Kuna sababu nyingi sana zinazowafanya watu (Watanzania) kwenda nje na kurudi nchini, moja ya sababu ya kwenda huko ni masomo unakuwa na student visa ikiisha au masomo yakiisha unalazimika kurudi nyumbani, sababu nyingine ni temporary work permit muda au kazi ikiisha unarudi nyumbani.

Sababu nyingine inayowafanya wengi kwenda nje ni kutafuta maisha, wengi huwa ni wazamiaji, wanaweza kuwa na passport halali ila wakifika huko wanazificha au kuzipoteza makusudi, wazamiaji wengine huenda kule wakiwa hawana karatasi (documents) zozote.

Kuna wanaokwenda kama wakimbizi halali na wakimbizi magumashi, kuna wanaokwenda majuu kwa kukimbia kesi mbaya zinazowakabiri kama mauaji ujambazi au madawa ya kulevya, kuna wanaokwenda huko kwa kukwepa majukumu ya kifamilia, kuna wanaokenda kwa ajili ya kuoa au kuolewa ili kupata passport au permanent residence.

Hizo ni baadhi tu ya sababu zinazowafanya watu waende nje au majuu kwa lugha ya mitaani, kama nilivyosema kuna sababu nyingi kila mtu anaenda na kurudi kwa sababu zake.

Sasa tuangalie uzoefu, kwa tuliofanikiwa kufika huko na kurudi nyumbani na wengine kubaki huko, nini kilikufanya urudi kwanini usiishi hukohuko na kuendeleza maisha ughaibuni kama walivyo wengine, na waliobaki huko nini kimewafanya msirudi, na je kama ulirudi, ulikuwa deported au uliamua mwenyewe kurudi.

Mimi binafsi, nilifanikiwa kwenda UK na niliishi huko kwa takribani miaka mitano. Nilienda kwa student visa, baada ya masomo nilianza kazi za kubeba 'box' ambazo ndizo rahisi kupata. Nilibahatika kutengeneza pesa kiasi chake hadi nikajenga kibanda nyumbani TZ. Wenzangu ambao hadi leo wapo huko walinishauri 'nijilipue' waliofika huko wanajua maana yake. Lakini nilishindwa kutokana na majukumu niliyoacha nyumbani na culture ya huko ya ubaguzi, mwafrika hasa ngozi nyeusi huonekana kama kinyesi kwa baadhi ya weupe walio wengi.

Labda nishee experience yangu kidogo. Siku moja mimi na rafiki yangu tuliingia baa 'pub', tukaenda kujoin kwenye meza moja na wazungu, tulipokaa tu wale wazungu wakachukua vinywaji vyao wakaacha kula wakaenda kusimama kaunta tukaachwa peke yetu, nikajisemea moyoni kwanini kudhalilika kwenye nchi za watu namna hii.

Kwa kifupi kilichochangia mimi kurudi pamoja na mambo mengine ni tabia ya ubaguzi ya watu weupe iwe kwenye kazi au kwenye social affairs, kingine ni upweke (loneliness) hakuna jirani wa kukutembelea au kukusalimia asubuhi kama tulivyozoea huku bongo, vile vile hali ya hewa baridi 24/7 umevaa minguo saba vest, shati, koti, sweat na jaketi juu ilinishinda, nk nk.

Kizuri nilichojifunza kwao ni kwamba wazungu are hard working people, they keep time, they keep promises akikuahidi kitu juwa utapata akisema NO ni NO kweli kweli hata ulie machozi ya damu, kingine kizuri kwao hawachagui kazi, serikali zinaheshimu sana kodi, kwa UK huwezi kufanyakazi yeyote hata ya kufagia barabara kama huna (NI Number) National Insurance Number sisi tunaita TIN.
National-insurance-number-card-300x188.png


>Please, share with us your experience.
>S'il vous plaît partagez avec nous votre expérience.
>Bitte teilen Sie uns Ihre Erfahrungen mit.
>请与我们分享您的经验
>Qǐng yǔ wǒmen fēnxiǎng nín de jīngyàn.
>Vær venlig at dele din erfaring med os.
>Por favor, compartilhe conosco sua experiência
==================!

Karibu, Welcome, Bienvenu, Huānyíng/欢迎, Bemvinda, Witamy, أهلا بك, Herzlich Willkommen, स्वागत हे.
 
Kwa wenzetu hasa scandinavia ni pazuri sema kuna ubaguzi ila sio mkubwa na hali ya hela vipinndi virefu vya winter viliniboa sana. Baada tu ya masomo nkaamua kurudi Kufanya kazi Tanzania. Ingawa ni ya kipato cha kati ni bora zaidi na uhuru zaidi kuliko kuajiriwa nje na kubeba box bila kuwekeza.
 
Kwa wenzetu hasa scandinavia ni pazuri sema kuna ubaguzi ila sio mkubwa na hali ya hela vipinndi virefu vya winter viliniboa sana. Baada tu ya masomo nkaamua kurudi Kufanya kazi Tanzania. Ingawa ni ya kipato cha kati ni bora zaidi na uhuru zaidi kuliko kuajiriwa nje na kubeba box bila kuwekeza.
Ungevumilia tu mkuu: kubeba box nje si nasikia inalipa zaidi
 
Kuna sababu nyingi sana zinazowafanya watu (Watanzania) kwenda nje na kurudi nchini, moja ya sababu ya kwenda huko ni masomo unakuwa na student visa ikiisha au masomo yakiisha unalazimika kurudi nyumbani, sababu nyingine ni temporary work permit muda au kazi ikiisha unarudi nyumbani.

Sababu nyingine inayowafanya wengi kwenda nje ni kutafuta maisha, wengi huwa ni wazamiaji, wanaweza kuwa na passport halali ila wakifika huko wanazificha au kuzipoteza makusudi, wazamiaji wengine huenda kule wakiwa hawana karatasi (documents) zozote.

Kuna wanaokwenda kama wakimbizi halali na wakimbizi magumashi, kuna wanaokwenda majuu kwa kukimbia kesi mbaya zinazowakabiri kama mauaji ujambazi au madawa ya kulevya, kuna wanaokwenda huko kwa kukwepa majukumu ya kifamilia, kuna wanaokenda kwa ajili ya kuoa au kuolewa ili kupata passport au permanent residence.

Hizo ni baadhi tu ya sababu zinazowafanya watu waende nje au majuu kwa lugha ya mitaani, kama nilivyosema kuna sababu nyingi kila mtu anaenda kwa sababu zake.

Sasa tuangalie uzoefu, kwa tuliofanikiwa kufika huko na kurudi nyumbani, nini kilikufanya kurudi kwanini usiishi hukohuko na kuendeleza maisha ughaibuni kama walivyo wengine, je ulikuwa deported au uliamua mwenyewe kurudi.

Mimi binafsi, nilifanikiwa kwenda UK na niliishi huko kwa takribani miaka mitano. Nilienda kwa student visa, baada ya masomo nilianza kazi za kubeba 'box' ambazo ndizo rahisi kupata. Nilibahatika kutengeneza pesa kiasi chake hadi nikajenga kibanda nyumbani TZ. Wenzangu ambao hadi leo wapo huko walinishauri 'nijilipue' waliofika huko wanajua maana yake. Lakini nilishindwa kutokana na majukumu niliyoacha nyumbani na culture ya huko ya ubaguzi, mwafrika hasa ngozi nyeusi huonekana kama kinyesi kwa baadhi ya weupe walio wengi.

Labda nishee experience yangu kidogo. Siku moja mimi na rafiki yangu tuliingia baa 'pub', tukaenda kujoin kwenye meza moja na wazungu, tulipokaa tu wale wazungu wakachukua vinywaji vyao wakaacha kula wakaenda kusimama kaunta. Kitendo kile kiliniuma sana nikajisemea moyoni kwanini kudhalilika kwenye nchi za watu namna hii.

Kwa kifupi kilichochangia mimi kurudi pamoja na mambo mengine ni tabia ya ubaguzi ya watu weupe iwe kwenye kazi au kwenye social affairs, upweke (loneliness) hakuna jirani wa kukutembelea au kukusalimia asubuhi kama tulivyozoea huku bongo nk nk. Lakini nilichojifunza kwao ni kwamba wazungu are hard working people, they keep time, they keep promises akikuahidi kitu juwa utapata akisema NO ni NO kweli kweli hata ulie machozi ya damu, kingine kizuri kwao hawachagui kazi.

Please, let us share the experience.
Sababu zako ni za kizembe sana. Eti unaenda kukaa meza moja na wazungu!!! eDIOT. Kwani hapa bongo ndio unaenda tu kwenye meza ya watu unajikalia. huo ni uswahili .
Huku vyuma vimebana sasa
 
Kuna kitu huwa kinanifurahisha mtu mfano mwanaume akiiondoka kwenda majuu siku ya kuondoka huvaa suti ya uhakika na viatu vya kiuhakika na sanduku kubwa la uhakika siku ya kurudi airport unampokea akiwa kavaa kaptula ,t-shirt ,kakofia na miguuni ana makobasi mgongoni kabeba school bag zile Watoto wa Shule hubeba migongoni yenye vitu vyake.Hapo huhitaji kufahamishwa utajiri uko upande gani
 
Back
Top Bottom