SANCTUS ANACLETUS
JF-Expert Member
- Mar 5, 2016
- 3,337
- 4,664
Ni lazima tuelezane ukweli wote watanzania. Muda wa kupewa Peremende kama Watoto wadogo kama njia ya kunyamazishana ilhali mahitaji yetu ni makubwa hayavumiliki na yanachosha.Kama ni mambo ya uchawa basi ni uchawa wa kishamba sana.
Nina jambo nataka tufichuane akili. Tupeane Mangwa. Tusadiane kufikiri. Tubebeane kufikiri kwa wale machawa wa Kufikiri.
Ni hivi kuna baadhi ya binadamu wakikosa majawabu katika magumu yayowakabili huishia kujikunakuna kuanzia kichwani mpaka kwenye maungo yao na huko huonyesha kuwa pengine tatizo ni Chawa, Kunguni au Siafu waliowapandalia kupitia Suruali au Sketi zao. Hapa nakumbuka wakati tuko Shule za Msingi na Sekondari na Vyuoni wakati wa Mitihani, Mwalimu anapomsimamisha Mwanfunzi Fulani na kumtaka atoe jibu la Swali Fulani. Ikitokea mwanafunzi Husika Swali limekuwa gumu kwake Ndipo utashuhudia mhusika kuishia kujikunakuna kuanzia kichwani na kisha kuishia Maungoni akiashiria tatizo la yeye kukosa jibu limechangiwa labda na Chawa au Kunguni walioko eneo hilo.
Sasa kwa ufupi sana lakini bila kupoteza maudhui ya bandiko hili ni Hivi: Wakati Uviko-19, ilipotuvamia na Dunia ikawa inahangaika isijue cha Kufanya, Raisi Magufuli alijikuna Kichwa na kutoka na njia tatu kuu kama kitulizo cha tatizo: Kukataa kujifungia ndani kama Mbuzi wa Shughuli na hivi kutuepusha na kuishia kuwa kama Kuku wa mdondo Pili, aliruhusu tutumie Mimea ya asili kama njia ya kuimarisha Kinga ya Miili yetu dhidi ya virusi wa Uviko. Na tatu, alikataa mambo ya kutaja idadi za watu waliokuwa wanakufa kila siku kwa tatizo hilo kama njia ya kuonyesha kuwa tatizo hilo na hapa kwetu lipo na linaendelea kuwepo.
Maajabu ya Musa, kuna baadhi ya watu waliojiona wana akili sana wakamrukia sana kwamba ameacha njia za Kisayansi ambazo zimependekezwa na Shirika la Afya Dunia katika kutatua tatizo la Uviko na badala yake ametuletea Njia za Kishirikina na kisukuma! Sitaki kueleza baadaye nani alionekana alikuwa anaona mbali kati ya Raisi Magufuli “Mshirikina” na wale Timu ya kujifungia ndani kama Kuku wa Kichina.
Maajabu mengine sasa yametufika. Kuna mgogoro mwingine wa Vita kati ya Ukraine na Urusi. Na sababu ya mgogoro huo tunaambiwa ndio maana Mafuta yamepanda bei. Na tunaambiwa Vita hiyo ikiisha Bei ya Mafuta itarudi kama awali.
Maajabu ya Firauni kuna kundi la watu wanatuaminisha maelezo hayo ni njia ya Kisayansi dhidi ya tatizo hili na wala sio ushirikina na wala sio mambo ya Kizenjibari na Umakunduchini.
Ninataka sasa kuwasilisha hoja kadhaa katika mtindo wa Maswali ya Kifalsafa ili yatusaidie kuona kama tuko Kisayansi Zaidi au Kishirikina Zaidi kwa namna tunavyolitatua tatizo la Bei ya Mafuta. Ni hivi:
1. Je, ni kweli suala la Bei ya Mafuta ni la Dunia nzima na suala la Uviko halikuwa la Dunia nzima kiasi “mshirikina” Raisi Magufuli ndio maana alihitaji kutumia akili zake kulingana na mazingira yetu kupata kitulizo cha tatizo la Uviko?
2. Vyombo vya dola, mintarafu idara ya kukusanya taarifa za Kiintelijinsia ilishakwenda kule Ukraine na Urusi na kukusanya taarifa za kuaminika na kuziwasilisha kwa mama lini vita hiyo itaisha na hivi tujivike moyo wa kusubiria tu kidogo maana hali itarejea kama kawaida kama anavyotusihi mama tuwe wavumilivu? Kama Sivyo, hili ombi kwa watanzania kuwa tuendelee kuyakabili magumu hayo ni njia ya kisayansi au ya kishirikina na tena ushirikina wa kigitali?
3. Raisi Magufuli alituhasa tutumie “Ruzuku” za Malimao, Tangawizi na kujifukiza dhidi ya Uviko na huo ukawa ushamba wa kiutawala na mambo ya uchato-chato. Katika suala la Mafuta tunaambiwa kuna Ruzuku ya Bilioni 100 kila Mwezi kama njia ya Kisayansi ya kuondokana na tatizo.
Najiuliza: Hii Ni njia ya kisayansi kweli au nao ni ushirikina tu kuamini kuwa Ruzuku hiyo inapunguza tatizo la Makali ya Bei? Hebu Fikiria mfano huu: Mimi ni Mvuvi wa kutumia Meli. Meli yetu moja katika msimu wa mwaka 2021 kabla ya Marehemu Magufuli kuchukuliwa na Mungu tulikuwa tunajaza Meli kwa Lita 30,000 za Mafuta ya Dizeli kwa Mwezi mmoja tu kwa shilini milioni 45. Sasa kwa Mwezi mmoja kwa kiwango hicho hicho cha Lita 30,000 tunatumia Shilingi Milioni 100,000! Hebu najiuliza Ruzuku inanisadiaje mimi kwenye bidhaa ya Samaki ninaowasafririsha nje? Nitapandisha bei na kulieleza soko kuwa ni kutokana na Ongezeko la bei ya mafuta kufuatia Vita ya Ukraine na Urusi?
4. Hapa Nyumbani tuna gesi. Na “ushirikina” uliofanyiwa utafiti unaonyesha kuwa gesi inaweza kutumika siku hizi katika kuendesha Mitambo mbalimbali badala ya Mafuta.
5. Je, Hivi Sayansi isingalikuwa ni Serikali kuongeza uzalishaji wa Gesi mraradufu au mara tatu na kuyalipa Makampuni yanayofanya Conversion ya system ya mitambo ya Magari na mitambo mingine Bilioni 100 kila mwezi ili wananchi wapeleke magari yao na sisi wenye meli tukafunge Mitambo ya Gesi ya kuendesha vyombo hivyo na hivi fedha hizo kubakia hapa Nyumbani badala ya kuchukua Bilioni 100 kila mwezi kwenda kufidia kununua Mafuta na hivi Fedha hizo kujenga uchumi wa hao wanaokoboana makonde huko Ukraini na urusi na huko Uarabuni au Marekani?
Nina Maswali mengi sana dhidi ya hiki kinachoonekana ndio Sayansi ya mama dhidi ya tatizo la Bei ya Mafuta lakini labda niulize moja tu kubwa: Hivi hii Dunia toka iumbwe kumewahi kuwa ufumbuzi mmoja au unaofanana tu wa tatizo fulani? Je, ina maana Nchi zingine nazo zimekaa zinasubiria Vita ya Ukraine ne Urusi iishe kama Njia ya kuondokana na tatizo la Mafuta? Pili, inaonekana Ukraine na Urusi ndio wazalishaji mojawapo wakubwa wa Mafuta Duniani na Hivi hii Vita imezuia au imepunguza uzalishaji. Sawai ko hivyo.Lakini Najiuliza sasa “Kishirikina” na sio Kisayansi: wakati ule wa Covid ambako wenzetu huko Ulaya, Marekani na Asia walijifungia ndani, ni Malaika na Majini ndio waliokuwa wanazalisha Mafuta kiasi kwamba hakukutokea au hatukushudia athari kubwa kama hivi katika suala la Mafuta kama tunavyoona sasa?
Kwa kweli sayansi inakwenda kwa kasi sana na Uongozi wa Nchi kwa Afrika siku hizi ni kitu kilichofanyiwa mapinduzi kama yale ya kutoka kunywea Vikombe vya shaba na Glasi hadi kunywea Makopo ya maboga.
Ni hivi: Uongozi siku hizi sio kitu cha kutumia akili kuonyesha ubunifu na kiongozi kuumiza kichwa chake kwa kadri Mungu alivyomujalia na kwa kuangalia rasilimali gani Mungu kalijalia Taifa bali ni suala la kukaa kitako na kusubiria ku-pesiti wengine wamefanyaje huko Duniani?
Ninapoona Viongozi wa Afrika wanaishia kutoa majibu kama haya tunayopewa hapa kwetu mintarafu suala la bei ya mafuta nakumbuka ule mfano wangu mwanzoni mwa uzi huu wa Mwanafunzi kukosa jibu nay eye kuishia kukukuna mwili mpaka maungoni na kusingizia Chawa au Kunguni kuwa huenda hao wamemtatiza kupata jibu sahihi kwa swali la Mwalimu wake.
Nina jambo nataka tufichuane akili. Tupeane Mangwa. Tusadiane kufikiri. Tubebeane kufikiri kwa wale machawa wa Kufikiri.
Ni hivi kuna baadhi ya binadamu wakikosa majawabu katika magumu yayowakabili huishia kujikunakuna kuanzia kichwani mpaka kwenye maungo yao na huko huonyesha kuwa pengine tatizo ni Chawa, Kunguni au Siafu waliowapandalia kupitia Suruali au Sketi zao. Hapa nakumbuka wakati tuko Shule za Msingi na Sekondari na Vyuoni wakati wa Mitihani, Mwalimu anapomsimamisha Mwanfunzi Fulani na kumtaka atoe jibu la Swali Fulani. Ikitokea mwanafunzi Husika Swali limekuwa gumu kwake Ndipo utashuhudia mhusika kuishia kujikunakuna kuanzia kichwani na kisha kuishia Maungoni akiashiria tatizo la yeye kukosa jibu limechangiwa labda na Chawa au Kunguni walioko eneo hilo.
Sasa kwa ufupi sana lakini bila kupoteza maudhui ya bandiko hili ni Hivi: Wakati Uviko-19, ilipotuvamia na Dunia ikawa inahangaika isijue cha Kufanya, Raisi Magufuli alijikuna Kichwa na kutoka na njia tatu kuu kama kitulizo cha tatizo: Kukataa kujifungia ndani kama Mbuzi wa Shughuli na hivi kutuepusha na kuishia kuwa kama Kuku wa mdondo Pili, aliruhusu tutumie Mimea ya asili kama njia ya kuimarisha Kinga ya Miili yetu dhidi ya virusi wa Uviko. Na tatu, alikataa mambo ya kutaja idadi za watu waliokuwa wanakufa kila siku kwa tatizo hilo kama njia ya kuonyesha kuwa tatizo hilo na hapa kwetu lipo na linaendelea kuwepo.
Maajabu ya Musa, kuna baadhi ya watu waliojiona wana akili sana wakamrukia sana kwamba ameacha njia za Kisayansi ambazo zimependekezwa na Shirika la Afya Dunia katika kutatua tatizo la Uviko na badala yake ametuletea Njia za Kishirikina na kisukuma! Sitaki kueleza baadaye nani alionekana alikuwa anaona mbali kati ya Raisi Magufuli “Mshirikina” na wale Timu ya kujifungia ndani kama Kuku wa Kichina.
Maajabu mengine sasa yametufika. Kuna mgogoro mwingine wa Vita kati ya Ukraine na Urusi. Na sababu ya mgogoro huo tunaambiwa ndio maana Mafuta yamepanda bei. Na tunaambiwa Vita hiyo ikiisha Bei ya Mafuta itarudi kama awali.
Maajabu ya Firauni kuna kundi la watu wanatuaminisha maelezo hayo ni njia ya Kisayansi dhidi ya tatizo hili na wala sio ushirikina na wala sio mambo ya Kizenjibari na Umakunduchini.
Ninataka sasa kuwasilisha hoja kadhaa katika mtindo wa Maswali ya Kifalsafa ili yatusaidie kuona kama tuko Kisayansi Zaidi au Kishirikina Zaidi kwa namna tunavyolitatua tatizo la Bei ya Mafuta. Ni hivi:
1. Je, ni kweli suala la Bei ya Mafuta ni la Dunia nzima na suala la Uviko halikuwa la Dunia nzima kiasi “mshirikina” Raisi Magufuli ndio maana alihitaji kutumia akili zake kulingana na mazingira yetu kupata kitulizo cha tatizo la Uviko?
2. Vyombo vya dola, mintarafu idara ya kukusanya taarifa za Kiintelijinsia ilishakwenda kule Ukraine na Urusi na kukusanya taarifa za kuaminika na kuziwasilisha kwa mama lini vita hiyo itaisha na hivi tujivike moyo wa kusubiria tu kidogo maana hali itarejea kama kawaida kama anavyotusihi mama tuwe wavumilivu? Kama Sivyo, hili ombi kwa watanzania kuwa tuendelee kuyakabili magumu hayo ni njia ya kisayansi au ya kishirikina na tena ushirikina wa kigitali?
3. Raisi Magufuli alituhasa tutumie “Ruzuku” za Malimao, Tangawizi na kujifukiza dhidi ya Uviko na huo ukawa ushamba wa kiutawala na mambo ya uchato-chato. Katika suala la Mafuta tunaambiwa kuna Ruzuku ya Bilioni 100 kila Mwezi kama njia ya Kisayansi ya kuondokana na tatizo.
Najiuliza: Hii Ni njia ya kisayansi kweli au nao ni ushirikina tu kuamini kuwa Ruzuku hiyo inapunguza tatizo la Makali ya Bei? Hebu Fikiria mfano huu: Mimi ni Mvuvi wa kutumia Meli. Meli yetu moja katika msimu wa mwaka 2021 kabla ya Marehemu Magufuli kuchukuliwa na Mungu tulikuwa tunajaza Meli kwa Lita 30,000 za Mafuta ya Dizeli kwa Mwezi mmoja tu kwa shilini milioni 45. Sasa kwa Mwezi mmoja kwa kiwango hicho hicho cha Lita 30,000 tunatumia Shilingi Milioni 100,000! Hebu najiuliza Ruzuku inanisadiaje mimi kwenye bidhaa ya Samaki ninaowasafririsha nje? Nitapandisha bei na kulieleza soko kuwa ni kutokana na Ongezeko la bei ya mafuta kufuatia Vita ya Ukraine na Urusi?
4. Hapa Nyumbani tuna gesi. Na “ushirikina” uliofanyiwa utafiti unaonyesha kuwa gesi inaweza kutumika siku hizi katika kuendesha Mitambo mbalimbali badala ya Mafuta.
5. Je, Hivi Sayansi isingalikuwa ni Serikali kuongeza uzalishaji wa Gesi mraradufu au mara tatu na kuyalipa Makampuni yanayofanya Conversion ya system ya mitambo ya Magari na mitambo mingine Bilioni 100 kila mwezi ili wananchi wapeleke magari yao na sisi wenye meli tukafunge Mitambo ya Gesi ya kuendesha vyombo hivyo na hivi fedha hizo kubakia hapa Nyumbani badala ya kuchukua Bilioni 100 kila mwezi kwenda kufidia kununua Mafuta na hivi Fedha hizo kujenga uchumi wa hao wanaokoboana makonde huko Ukraini na urusi na huko Uarabuni au Marekani?
Nina Maswali mengi sana dhidi ya hiki kinachoonekana ndio Sayansi ya mama dhidi ya tatizo la Bei ya Mafuta lakini labda niulize moja tu kubwa: Hivi hii Dunia toka iumbwe kumewahi kuwa ufumbuzi mmoja au unaofanana tu wa tatizo fulani? Je, ina maana Nchi zingine nazo zimekaa zinasubiria Vita ya Ukraine ne Urusi iishe kama Njia ya kuondokana na tatizo la Mafuta? Pili, inaonekana Ukraine na Urusi ndio wazalishaji mojawapo wakubwa wa Mafuta Duniani na Hivi hii Vita imezuia au imepunguza uzalishaji. Sawai ko hivyo.Lakini Najiuliza sasa “Kishirikina” na sio Kisayansi: wakati ule wa Covid ambako wenzetu huko Ulaya, Marekani na Asia walijifungia ndani, ni Malaika na Majini ndio waliokuwa wanazalisha Mafuta kiasi kwamba hakukutokea au hatukushudia athari kubwa kama hivi katika suala la Mafuta kama tunavyoona sasa?
Kwa kweli sayansi inakwenda kwa kasi sana na Uongozi wa Nchi kwa Afrika siku hizi ni kitu kilichofanyiwa mapinduzi kama yale ya kutoka kunywea Vikombe vya shaba na Glasi hadi kunywea Makopo ya maboga.
Ni hivi: Uongozi siku hizi sio kitu cha kutumia akili kuonyesha ubunifu na kiongozi kuumiza kichwa chake kwa kadri Mungu alivyomujalia na kwa kuangalia rasilimali gani Mungu kalijalia Taifa bali ni suala la kukaa kitako na kusubiria ku-pesiti wengine wamefanyaje huko Duniani?
Ninapoona Viongozi wa Afrika wanaishia kutoa majibu kama haya tunayopewa hapa kwetu mintarafu suala la bei ya mafuta nakumbuka ule mfano wangu mwanzoni mwa uzi huu wa Mwanafunzi kukosa jibu nay eye kuishia kukukuna mwili mpaka maungoni na kusingizia Chawa au Kunguni kuwa huenda hao wamemtatiza kupata jibu sahihi kwa swali la Mwalimu wake.