mwanaizaya
Senior Member
- Apr 26, 2008
- 133
- 1
Tulikotoka: 'Marais wastaafu wanaifilisi nchi'
*Watumia mamilioni kila mwaka
*Salim Ahmed Salim naye atengewa zake
Dodoma, Agosti 4, 1998
MARAIS wastaafu ni miongoni mwa viongozi ambao wameelezwa kutumia fedha nyingi za walipa kodi hali inayotishia kufilisi nchi na kuzorotesha huduma muhimu za jamii.
Akichangia hotuba ya makadirio ya matumi ya fedha ya Waziri Nchi Ofisi ya Rais Utumishi ya mwaka 1998/99 bungeni jana, Waziri Kivuli wa Utumishi, Bw. Seif Mohamed Azzani, alitaka Serikali kupunguza gharama za kuwakirimu viongozi hao kulingana na hali ya uchumi wa Tanzania.
Bw. Azzani aliainisha gharama hizo kuwa ni kwa ajili ya matumizi ya simu, samani, maji na matengenezo ya magari kwa marais na makamu wa Rais wastaafu.
Aliongeza kuwa kila Rais Mstaafu anagharimiwa na Serikali sh. milioni 7.2 kwa ajili ya simu, sh. milioni 14.4 za kwa ajili ya matengenezo ya magari na sh. milioni 1.2 kwa gharama za maji kwa mwaka.
Alisema kuwa kila Makamu wa Rais Mstaafu analipwa sh. milioni 4.8 kwa ajili ya simu, na kutoa mfano wa sh. milioni 1.5 kwa simu za Dkt. Salim Ahamed Salim, ambaye ni Katibu Mkuu wa Nchi za Umoja wa Afrika (OAU) ambazo ni kubwa mno kulingana na uchumi wa Tanzania.
Alihoji inakuwaje Dkt. Salim ambaye anatumikia OAU kulipwa gharama hizo na Serikali wakati angeweza kulipwa na mwajiri wake?
*Watumia mamilioni kila mwaka
*Salim Ahmed Salim naye atengewa zake
Dodoma, Agosti 4, 1998
MARAIS wastaafu ni miongoni mwa viongozi ambao wameelezwa kutumia fedha nyingi za walipa kodi hali inayotishia kufilisi nchi na kuzorotesha huduma muhimu za jamii.
Akichangia hotuba ya makadirio ya matumi ya fedha ya Waziri Nchi Ofisi ya Rais Utumishi ya mwaka 1998/99 bungeni jana, Waziri Kivuli wa Utumishi, Bw. Seif Mohamed Azzani, alitaka Serikali kupunguza gharama za kuwakirimu viongozi hao kulingana na hali ya uchumi wa Tanzania.
Bw. Azzani aliainisha gharama hizo kuwa ni kwa ajili ya matumizi ya simu, samani, maji na matengenezo ya magari kwa marais na makamu wa Rais wastaafu.
Aliongeza kuwa kila Rais Mstaafu anagharimiwa na Serikali sh. milioni 7.2 kwa ajili ya simu, sh. milioni 14.4 za kwa ajili ya matengenezo ya magari na sh. milioni 1.2 kwa gharama za maji kwa mwaka.
Alisema kuwa kila Makamu wa Rais Mstaafu analipwa sh. milioni 4.8 kwa ajili ya simu, na kutoa mfano wa sh. milioni 1.5 kwa simu za Dkt. Salim Ahamed Salim, ambaye ni Katibu Mkuu wa Nchi za Umoja wa Afrika (OAU) ambazo ni kubwa mno kulingana na uchumi wa Tanzania.
Alihoji inakuwaje Dkt. Salim ambaye anatumikia OAU kulipwa gharama hizo na Serikali wakati angeweza kulipwa na mwajiri wake?