Tulikokwenda kombo - tutarudi?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Mtu aliyepotea njia hajitendei haki kwa kuendelea na njia ile ile aliyopotea akitegemea kuwa kwa "bahati" ataweza kufika kule anakotaka kufika. Tanzania tuliyo nayo leo hii ni matokeo ya safari yetu tangu uhuru, safari ambayo bila ya shaka imetufikisha hapa.

Hata hivyo swali ambalo siku moja litahitaji kujibiwa ni kama hapa ndipo tulipotaka kufika? Je safari yetu ya miaka 45 na zaidi ilikuwa na lengo la kufika hapa au kuna mahali tumeenda pembeni?

Binafsi naamini kabisa kuwa kuna mahali tulikosea katika safari yetu na toka hapo tumekuwa tukienda tu "alimradi" tufike lakini hatujajiuliza "ni wapi tulikopaswa" kwenda na kama hapa tulipo ni sehemu ya mwelekeo wa huko tulikotaka kwenda.

Tulipotaka kujenga Taifa la "watu walio huru na sawa" na Taifa ambapo "kila mtu ana haki ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake" hiki tulichonacho leo ndilo Taifa lile tulilolitaka? Matukio ya Tabata siku chache zilizopita ambapo watawala kwa nguvu ambazo waliamini wanazo waliamuru na kwenda kuvunja nyumba za watu na baadaye kugeukana hayana budi kutuuliza kama hili ndilo Taifa tulilolitaka kulijenga?

2943.jpg

Licha ya kuwa taifa linaadhimisha wiki ya maji lakini bado baadhi ya wananchi hawapati maji safi na salama, pichani ni mkazi wa kijiji cha Goba Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, Asma Ali akichota maji katika moja ya visima vilivyopo kijijini hapo jana kwa matumizi ya nyumbani. (Picha na Mroki Mroki)

Picha kama hiyo hapo juu inaelezea kwa kina mahali ambapo tulipo leo hii, hasa tukilinganisha na hii nyingine katika Jiji hilo hilo moja.

jengo.jpg
CENTER]

Kama hili ndilo Taifa tulilolitaka kwanini tusikubali yaishe tu na kufurahia "uzuri wa nchi yetu", kama silo lile hasa tulilolitamania kiasi cha kuamua kudai uhuru, tufanye nini basi kujenga Taifa tunalolitaka?​
 
NI KWELI TUMEENDA KOMBO....(kolimba alisema ....dira na mwelekeo......tumepoteza...)NA KAMA DIRA/COMPASS IMEPOTEA..MWELEKEO/DIRECTION PIA HATUNA(kas,kus,mash&magh) NINI CHA KUFANYA......!
{mawazo yangu tu}WE HAVE TO THINK WAPI TUNADHANI NDIPO TULIPOPOTEZA DIRA NA MWELEKEO WETU.....! HATA WANA WA ISRAELI(ya kidini zaidi) SEHEMU AMBAYO LEO NI TWO HOURS FLIGHT &8HOURS DRIVE IT TOOK THEM 40 YEARS...! KWA NINI SISI IWE ZAIDI YA MIAKA 45......! WHY....! ITS BECAUSE WE LOST SOMEWHERE,(1980's?)......!AS GOOD GEOGRAPHERS LETS GO BACK (ujamaa?) AND NOT GOING ON WITH OUR JOURNEY THINKING WE CAN REACH WHERE WE ARE GOING SIMPLY BECAUSE THE PATH WE ARE USING KUNA DALILI KUWA WATU HUPITA KWANI KUNA ALAMA ZA NYAYO......! HIZO NYAYO TUZIONAZO KUNA MTU ALIKUWA NA SAFARI YAKE ILA SI KULE TUENDAKO SISI.........!
NIMEELEWEKA......?TUPO PAMOJA......?
 
NI KWELI TUMEENDA KOMBO....(kolimba alisema ....dira na mwelekeo......tumepoteza...)NA KAMA DIRA/COMPASS IMEPOTEA..MWELEKEO/DIRECTION PIA HATUNA(kas,kus,mash&magh) NINI CHA KUFANYA......!
{mawazo yangu tu}WE HAVE TO THINK WAPI TUNADHANI NDIPO TULIPOPOTEZA DIRA NA MWELEKEO WETU.....! HATA WANA WA ISRAELI(ya kidini zaidi) SEHEMU AMBAYO LEO NI TWO HOURS FLIGHT &8HOURS DRIVE IT TOOK THEM 40 YEARS...! KWA NINI SISI IWE ZAIDI YA MIAKA 45......! WHY....! ITS BECAUSE WE LOST SOMEWHERE,(1980's?)......!AS GOOD GEOGRAPHERS LETS GO BACK (ujamaa?) AND NOT GOING ON WITH OUR JOURNEY THINKING WE CAN REACH WHERE WE ARE GOING SIMPLY BECAUSE THE PATH WE ARE USING KUNA DALILI KUWA WATU HUPITA KWANI KUNA ALAMA ZA NYAYO......! HIZO NYAYO TUZIONAZO KUNA MTU ALIKUWA NA SAFARI YAKE ILA SI KULE TUENDAKO SISI.........!
NIMEELEWEKA......?TUPO PAMOJA......?

Ndiyo Mzee
 
NOT GOING ON WITH OUR JOURNEY THINKING WE CAN REACH WHERE WE ARE GOING SIMPLY BECAUSE THE PATH WE ARE USING KUNA DALILI KUWA WATU HUPITA KWANI KUNA ALAMA ZA NYAYO......! HIZO NYAYO TUZIONAZO KUNA MTU ALIKUWA NA SAFARI YAKE ILA SI KULE TUENDAKO SISI.........!
NIMEELEWEKA......?TUPO PAMOJA......?


Mahesabu, asante kwa mfano huo na ninaomba ni upanue kidogo niweze kuutumia kwenye makala yangu ya Jumatano..!!
 
Mahesabu, asante kwa mfano huo na ninaomba ni upanue kidogo niweze kuutumia kwenye makala yangu ya Jumatano..!!
RUKSAAAA! And make sure unawatetea watanzania,tena wa hali ya chini ambao hawana mtetezi...WE DARE TO TALK OPENLY!
 
Hiyo picha inatia huzuni sana, yaani wakati nasikia wenzetu huku wanalalamika kuhusu negligible traces za antibiotics na chemicals kwenye drinkable tap water, just for the sake of pursuing the illusion of perfection, sie bado tunakunywa mitope, tena Goba hapo Dar-es-salaam tu.Sasa tukienda Malampaka na Narung'ombe huko?
 
Hiyo picha inatia huzuni sana, yaani wakati nasikia wenzetu huku wanalalamika kuhusu negligible traces za antibiotics na chemicals kwenye drinkable tap water, just for the sake of pursuing the illusion of perfection, sie bado tunakunywa mitope, tena Goba hapo Dar-es-salaam tu.Sasa tukienda Malampaka na Narung'ombe huko?
WE HAVE TO RUN WHILE OTHERS ARE WALKING.....NA SIO KINYUME CHAKE....!
 
Mtu aliyepotea njia hajitendei haki kwa kuendelea na njia ile ile aliyopotea akitegemea kuwa kwa "bahati" ataweza kufika kule anakotaka kufika. Tanzania tuliyo nayo leo hii ni matokeo ya safari yetu tangu uhuru, safari ambayo bila ya shaka imetufikisha hapa.

Hata hivyo swali ambalo siku moja litahitaji kujibiwa ni kama hapa ndipo tulipotaka kufika? Je safari yetu ya miaka 45 na zaidi ilikuwa na lengo la kufika hapa au kuna mahali tumeenda pembeni?

Binafsi naamini kabisa kuwa kuna mahali tulikosea katika safari yetu na toka hapo tumekuwa tukienda tu "alimradi" tufike lakini hatujajiuliza "ni wapi tulikopaswa" kwenda na kama hapa tulipo ni sehemu ya mwelekeo wa huko tulikotaka kwenda.

Tulipotaka kujenga Taifa la "watu walio huru na sawa" na Taifa ambapo "kila mtu ana haki ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake" hiki tulichonacho leo ndilo Taifa lile tulilolitaka? Matukio ya Tabata siku chache zilizopita ambapo watawala kwa nguvu ambazo waliamini wanazo waliamuru na kwenda kuvunja nyumba za watu na baadaye kugeukana hayana budi kutuuliza kama hili ndilo Taifa tulilolitaka kulijenga?

2943.jpg


Licha ya kuwa taifa linaadhimisha wiki ya maji lakini bado baadhi ya wananchi hawapati maji safi na salama, pichani ni mkazi wa kijiji cha Goba Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, Asma Ali akichota maji katika moja ya visima vilivyopo kijijini hapo jana kwa matumizi ya nyumbani. (Picha na Mroki Mroki)

Picha kama hiyo hapo juu inaelezea kwa kina mahali ambapo tulipo leo hii, hasa tukilinganisha na hii nyingine katika Jiji hilo hilo moja.

jengo.jpg


Kama hili ndilo Taifa tulilolitaka kwanini tusikubali yaishe tu na kufurahia "uzuri wa nchi yetu", kama silo lile hasa tulilolitamania kiasi cha kuamua kudai uhuru, tufanye nini basi kujenga Taifa tunalolitaka?

Hayo maji akichota anapeleka wapi? Halafu kuna watu wanakula pesa ya walipa kodi utafikiri shamba la bibi halina mwenyewe.
 
Hayo maji akichota anapeleka wapi? Halafu kuna watu wanakula pesa ya walipa kodi utafikiri shamba la bibi halina mwenyewe.

it seems you guys didn't notice what I was pointing in the second picture... not the big building ... silly..
 
it seems you guys didn't notice what I was pointing in the second picture... not the big building ... silly..

Just curious, huko kwenye maofisi wanakwendaje kujisidia? Au wanakwenda porini? Nauliza tu ........................pengine kuna mapori special kwa vingunge.
 
Ingawa nilishawahi kuutumia mfano wa wana wa Israel kutapatapa Jangwani. Lakini naona tunautumia kujipa moyo tu na kutafuta sababu za kuwaachia matatizo yetu vizazi vinavyokuja.

Mussa alipewa maagizo ya kuwakomboa wanaIsrael kutoka utumwani na kwenda kwenye nchi ya ahadi. Hivyo tayari wao walikuwa na malengo. Na njia walizotumia zilikuwa AD-HOC na zenye kutatua matatizo kwa vipindi tofauti vilivyo wakabili wakiwa njia. Hivyo walikuwa kama wacheza BAO au DRAFT, na mbinu walizotumia kufika zilitegemea na wakati na maadui waliokutana nao njiani.

Sasa tukirudi kwetu, tuna tofauti kubwa. Sisi tumeshaweka njia za kupita lakini hatuna malengo ya wapi tunakwenda. Suala la kufanya watanzania wajitosheleze kwa chakula sio ROCKET SCIENCE. Suala la watanzania kuwa na mavazi sio ROCKET SCIENCE. Ni technologia zenye zaidi ya miaka 3000 duniani na zenye malighafi za kutosha.

Katiba ya nchi inaposema tunataka kujenga taifa la KIJAMAA, kuna maana gani? Ni lazima tuambizane ukweli. Hata primitives wasiohitaji umeme, matibabu ya hospital hawawezi kuishi kwenye purity za ujamaa. Kati yao kuna atayetaka embe kubwa zaidi ya mwenzake.


Watanzania tuache kuwa watu wa itikadi na tujaribu kuwa pragmatic.
 
Tulipotaka kujenga Taifa la "watu walio huru na sawa" na Taifa ambapo "kila mtu ana haki ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake" hiki tulichonacho leo ndilo Taifa lile tulilolitaka? Matukio ya Tabata siku chache zilizopita ambapo watawala kwa nguvu ambazo waliamini wanazo waliamuru na kwenda kuvunja nyumba za watu na baadaye kugeukana hayana budi kutuuliza kama hili ndilo Taifa tulilolitaka kulijenga?

Mfano huu wa Tabata mimi unanitatiza sana. Sehemu ya makazi inaitwa Tabata Dampo kwa hiyo natumai kuwa kuna wakati ilikuwa ikitumika kama dampo. Kama hii ni kweli, sehemu hii ni hatari kwa sababu tunamtindo wa kutupa kila kitu wenye dampo bila kuchambua. Bila shaka basi taka zenye sumu ziliwahi kutupwa sehemu hiyo na zimeingia kwenye udongo wa sehemu hiyo. Sehemu kama hiyo basi kwa vyovyote vile haiwezi kufaa kwa makazi ya binadamu au matumizi mengine bila kuondoa sumu hiyo. Leo watu wanaishi hapo, watoto wanazaliwa hapo, bila shaka wanalima vibustani kwa ajili ya lishe yao bila shaka kwa kukosa sehemu nyingine ya kuishi. Pamoja na kusikitikia jinsi walivyotendewa hasa kwa vile wenye nguvu wanataka kuwatoa ili wampishe mwenye nazo, kinachonisikitisha zaidi ni kuwa miaka 47 baada ya kupata uhuru leo hii mtanzania anaishi mahali kama hapo na kuna watu wanaona hiyo ni stahili yake! Hii ni kama vile tunavyowaangalia wanaoishi katika bonde la Jangwani bila kujali madhara ya mafuriko pamoja na yale yanaotokana na matumizi ya maji ya mto Msimbazi ambao umeishakuwa polluted kupita kiasi! Ni aibu kwetu wote na ni aibu zaidi kuwa hawa( na wengi zaidi) hawana sehemu mbadala ya kuishi! Mantra yetu ya makazi bora imeishia wapi? Hatuwezi kurudi kutafuta tulipokosea njia bali ni lazima hapa tulipo tuangalie ramani na tutafute njia mbadala ya kutupeleka tunakotaka kwenda tukitumia uzoefu tulioupata. Lakini cha maana zaidi, tukubaliane kwa dhati wapi tunataka kwenda! Bila hiyo hata GPS haitatusaidi kitu.
 
Back
Top Bottom