Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,463
- 39,929
Na. M. M. Mwanakijiji
Tulizaliwa katika mfumo wa kifisadi; tulikua na kuishi katika mfumo huo, na tulikufa tukiujua mfumo huo peke yake. Ndani ya mfumo tulienda na tukawa; watoto wetu na wajukuu wakaukuta mfumo na kuamini ndio maisha pekee wanayoweza kuishi. Ili mtu afanikiwe alitakiwa awe fisadi mwezeshaji au fisadi mwezaji.
Tulitengeneza taifa la mafisadi wakongwe na mafisadi vijana; mafisadi waliopo na mafisadi watarajiwa.
Ndugu zangu, madhara ya maisha haya sasa yanaonekana. Lakini tuweze kuelewa madhara yake ni vizuri kujua kabisa kuwa mfumo huu wa maisha uliwafanya watu waishi, jamii iende, nchi ionekane inakwenda n ahata pale ambapo haikwenda tulifisadiana katika kusaidiana kuifanya ionekane inaenda.
Ufisadi ulikuwa ni sehemu kubwa ya maisha kiasi kwamba watu walipanga bajeti za maisha na maendeleo na ndani yake waliweka bajeti ya ufisadi kukamilisha ndoto zao. Ukitaka kupata kibali cha shilingi 10,000 lazima utenge angalau 50,000 za kulainisha mikono ya watu. Ukitaka kujenga nyumba yako yenye gharama ya milioni mia moja gharama yake halisi ilikuwa kama milioni mia na hamsini – hamsini za kufanikisha mambo yako mbalimbali na yafanikiwe.
Hili lilikuwa kweli katika elimu, maji, afya, huduma mbalimbali na katika ngazi mbalimbali. Ufisadi ulikuwa ni sehemu ya maisha kuanzia kwenye kata vijiji hadi tarafa, wilaya hadi mikoa na tukaona ufisadi kutoka mikoa hadi taifa. Tukazoea kuishi kwenye maisha ya kashfa kubwa kubwa kama vile tunalazimishwa kuishi kwenye maji kama samaki; bila kashfa kubwa nchi ilikuwa haiendi. Kuanzia kashfa za kina Valambhia hadi kufika kina Rostam, kuanzia za kina Iddi Simba hadi Rugemalira Watanzania walizoea ufisadi na ufisadi uliwazoea Watanzania.
Tulicheka na kuchekeana katika ufisadi, tulizoea na kuzoeana , kubembeleza na kubembelezana huku tukisha na kushikana huku tukikodoleana na kutishana! Ufisadi ulikuwa kama dini iliyotuuunganisha, tukipiga magoti na kutoa dhabihu zetu za kushukuru mbele ya mafisadi katika madhabahu yao. Ukitaka kufanikiwa lazima umjue au umjue anayemjua anayejulikana. Ufisadi tungeweza kuuimbia nchi “ooh ufisadi wajenga nchi!” Na tuliamini ufisadi kweli kabisa unajenga nchi. Hata kama tuliulaani hadharani na kuwabeza mafisadi.
Uchaguzi wa 2015 ulikuwa ni ni uchaguzi wa ama kuendelea na maisha yale au kubadilisha mwelekeo. Ulikuwa ni uchaguzi wa kati ya kutamalaki kwa ufisadi au kuvunjwa vunjwa kwa madhabahu ya dini hiyo yenye watu wenye dini zote! Imani ya dini hiyo ni tumbo na kitabu chake kimeandikwa kwa maandishi ya tamaa. Uchaguzi ule ulikuwa ni wa ama kuendelea na tulivyokuwa tukiishi huku tunafurahi katika ufisadi wetu; hakuna maamivu ya moja kwa moja kila mtu akiishi kwa kujifurahisha mwenyewe na familia yake.
Ulikuwa ni uchaguzi wa kuamua kama tunataka kuuvunja mfumo huo haramau au kuulea kidogo kwa sababu tumeuzoea.
Tuliokuwa tumedeka kwenye mfumo huo hatukuweza kufikiria namna nyingine yoyote ya kuishi. Ni kama mtoto anayetoka kwenye familia iliyomdekeza na siku moja anaambiwa hakuna vya bure tena shika jembe ukalime. Mtoto yule anapolima kidogo tu mikono yote inamuuma na kuanza kuchubuka huku ikitokea malengelenge! Machozi yatamlenga na kujiuliza kumbe “kilimo ni kigumu hivyo”.
Hili linanikumbusha nilipoenda kuanza shule ya Sekondari miaka mingi nyuma kwenye shule ya Wazazi ya Boza, Pangani Tanga. Nakumbuka mtoto mmoja binti wa familia ya kitajiri aliyeletwa bweni kuanza maisha na kupaona mahali penyewe palivyo (wakati ule). Binti yule aliangusha kilio gari la wazazi wale lilipoondoka kumuacha na kwa karibu wiki nzima alikuwa hana raha mtoto wa watu, akigoma kula na tunashukuru Mungu hakukuwa na Facebook wala Whatsapp enzi hizo, wala Instagram! Kilichomsaidia binti yule (msema kweli Mpenzi wa Mungu) – ni kuwa alijaliwa “Neema za Allah” na vijana wengi (mimi si mmoja wapo) walijitolea kumsaidia kwa kazi zake mbalimbali – hasa ilipofika zamu ya kwenda kubeba kuni!
Baada ya muda alizoea, akazoea maisha ya kule kwani asingeweza kuwapa vijana wote vile walivyohitaji bila ya kujichafua jina lake. Miaka minne baadaye alipohitimu binti yule alikuwa ni “mama” akiwasaidia mabinti wengine walioifika pale na baadaye akaja kuolewa na mlalahoi mmoja. Aliingia shule akiwa hajui jinsi ya kushika kijiko, alihitimu akijua kushika mwiko; aliingia akiwa na madaha, alitoka akiwa na staha.
Ndugu zangu, ufisadi ulikuwa ni kama dawa ya kulevya; taratibu taratiu watu wakauzoea na mwisho wa siku wakata arosto.
Uchumi wetu na maisha yetu kama taifa na kama mtu mmoja mmoja yalihitaji dozi ya dawa hii ya ufisadi ili mambo yaende. Alichofanya Magufuli na ambacho anaendelea kufanya (japo naona kama mwendo umepungua kidogo) ni kuwakatisha watu kupata dawa hii haramu. Matokeo yake watu sasa wako katika hali ya kuonesha withdrawal symptoms. Yaani, watu sasa wanagundua kuwa hawawezi kuishi bila kupata kitu kidogo kwenye damu zao. Kuna wengine ambao wanaona labda asingefanya kwa ukali hivi kwani wakati mwingine mtu anapokatishwa kutumia madawa kwa ghafla anaweza kuishia kuumwa sana na hata kufa! Je, Magufuli angefanya taratibu, abembeleze, asiguse sana uchumi na aachie achie kidogo ili watu wasiumie?
Ndugu zangu, leo hii wapo watu wanapata shida. Kuanza kumomonyolewa na kubanduliwa kwa mfumo wa utawala wa kifisadi kunawafanya watu wakose pa kushikilia. Wenye kulia wanalia, wenye kuumia wanaumia lakini nawaambia kwa uthabiti kabisa wa moyo kuwa hakuna wakati muhimu sana kwa historia ya Taifa letu kama wakati huu. Miaka hii mitatu ya mwanzo ya Rais Magufuli inanithibitishia kabisa kuwa tulichelewa sana na sasa maumivu tunayoyaona ni maumivu ya mtu aliyechelewa kupata tiba na sasa analazimika kufanyiwa upasuaji mkubwa; si mchezo, si lele mama.
Miaka hii mitatu ya kujaribu kuvunja ufisadi, kujenga taifa la watu wanaojiamini na kujitegemea kifikra si jambo rahisi. Makosa yatafanyika, matatizo mengine yataibuliwa, vingine vitaharibiwa lakini kiujumla wake maisha yataenda tu ndugu zangu. Hata wagonjwa wanapofanyiwa upasuaji si wote wanapona na wakati mwingine kunatoke “complications” lakini nia na uthubutu wa madaktari hauwezi kupuuzwa au kubezwa.
Miaka mitatu baadaye ninapoangalia taifa letu linapokwenda sina sababu yoyote ya kujuta kukata marudio na mwendelezo wa mfumo wa utawala wa kifisadi. Sina majuto ya kuunyoshea kidole na kuukataa hata kama ungerudishwa kwa kisingizio cha “mabadiliko” ya kuzungusha mikono. Mambo yote leo yanafanyika nilivyotarajia? La hasha! Kuna vitu ambavyo ningependa vifanyike na havifanyiki au visifanyike na vinafanyika? Si kidogo! Lakini, kutengeneza nidhamu mpya, njia mpya na mwelekeo bora wa kitaifa linafanyika? Bila ya shaka!
Miaka miwili ijayo, itatupa mwanga zaidi; tutaona zaidi mafanikio ya utawala huu na nina uhakika Watanzania wengi zaidi – pamoja na maumivu na usumbufu wa sasa – watasimama na kusema tunahitaji miaka mingine mitano. Gharama ya kujenga mfumo wa maendeleo ni kubwa sana na tumeanza kuilipa. Nina uhakika yatafanyika masahihisho ya maeneo yanayosumbua sasa hivi. Tusije kuthubutu kuangalia nyuma na kutamani kule tulikotoka. Tukatae kabisa kuambiwa ati wakati wa Kikwete na Mkapa ulikuwa ni mzuri sana kwa sababu tulikula “nyama, matikiti maji na vitunguu saumu”.
Kwamba, kwa vile tuliishi katika Misri ya Ufisadi basi ilikuwa nzuri kwa sababu tulikuwa salama na wenye Amani. Tuwakatae na kuwapinga wanaotaka tukumbuke Misri ile ati tu kwa vile huku kwenye nchi ya ahadi kumbe tunatakiwa kufanya kazi, kuhenyeka na kufanya kazi kama uhai wetu unategemea.
Tusonge mbele kwa jitihada, ufanisi, na uwajibikaji. Tukifanya tunachopaswa kufanya basi kile tunachokifanya tutaona kweli kinatupasa!
Niandikie: klhnews@gmail.com
Tulizaliwa katika mfumo wa kifisadi; tulikua na kuishi katika mfumo huo, na tulikufa tukiujua mfumo huo peke yake. Ndani ya mfumo tulienda na tukawa; watoto wetu na wajukuu wakaukuta mfumo na kuamini ndio maisha pekee wanayoweza kuishi. Ili mtu afanikiwe alitakiwa awe fisadi mwezeshaji au fisadi mwezaji.
Tulitengeneza taifa la mafisadi wakongwe na mafisadi vijana; mafisadi waliopo na mafisadi watarajiwa.
Ndugu zangu, madhara ya maisha haya sasa yanaonekana. Lakini tuweze kuelewa madhara yake ni vizuri kujua kabisa kuwa mfumo huu wa maisha uliwafanya watu waishi, jamii iende, nchi ionekane inakwenda n ahata pale ambapo haikwenda tulifisadiana katika kusaidiana kuifanya ionekane inaenda.
Ufisadi ulikuwa ni sehemu kubwa ya maisha kiasi kwamba watu walipanga bajeti za maisha na maendeleo na ndani yake waliweka bajeti ya ufisadi kukamilisha ndoto zao. Ukitaka kupata kibali cha shilingi 10,000 lazima utenge angalau 50,000 za kulainisha mikono ya watu. Ukitaka kujenga nyumba yako yenye gharama ya milioni mia moja gharama yake halisi ilikuwa kama milioni mia na hamsini – hamsini za kufanikisha mambo yako mbalimbali na yafanikiwe.
Hili lilikuwa kweli katika elimu, maji, afya, huduma mbalimbali na katika ngazi mbalimbali. Ufisadi ulikuwa ni sehemu ya maisha kuanzia kwenye kata vijiji hadi tarafa, wilaya hadi mikoa na tukaona ufisadi kutoka mikoa hadi taifa. Tukazoea kuishi kwenye maisha ya kashfa kubwa kubwa kama vile tunalazimishwa kuishi kwenye maji kama samaki; bila kashfa kubwa nchi ilikuwa haiendi. Kuanzia kashfa za kina Valambhia hadi kufika kina Rostam, kuanzia za kina Iddi Simba hadi Rugemalira Watanzania walizoea ufisadi na ufisadi uliwazoea Watanzania.
Tulicheka na kuchekeana katika ufisadi, tulizoea na kuzoeana , kubembeleza na kubembelezana huku tukisha na kushikana huku tukikodoleana na kutishana! Ufisadi ulikuwa kama dini iliyotuuunganisha, tukipiga magoti na kutoa dhabihu zetu za kushukuru mbele ya mafisadi katika madhabahu yao. Ukitaka kufanikiwa lazima umjue au umjue anayemjua anayejulikana. Ufisadi tungeweza kuuimbia nchi “ooh ufisadi wajenga nchi!” Na tuliamini ufisadi kweli kabisa unajenga nchi. Hata kama tuliulaani hadharani na kuwabeza mafisadi.
Uchaguzi wa 2015 ulikuwa ni ni uchaguzi wa ama kuendelea na maisha yale au kubadilisha mwelekeo. Ulikuwa ni uchaguzi wa kati ya kutamalaki kwa ufisadi au kuvunjwa vunjwa kwa madhabahu ya dini hiyo yenye watu wenye dini zote! Imani ya dini hiyo ni tumbo na kitabu chake kimeandikwa kwa maandishi ya tamaa. Uchaguzi ule ulikuwa ni wa ama kuendelea na tulivyokuwa tukiishi huku tunafurahi katika ufisadi wetu; hakuna maamivu ya moja kwa moja kila mtu akiishi kwa kujifurahisha mwenyewe na familia yake.
Ulikuwa ni uchaguzi wa kuamua kama tunataka kuuvunja mfumo huo haramau au kuulea kidogo kwa sababu tumeuzoea.
Tuliokuwa tumedeka kwenye mfumo huo hatukuweza kufikiria namna nyingine yoyote ya kuishi. Ni kama mtoto anayetoka kwenye familia iliyomdekeza na siku moja anaambiwa hakuna vya bure tena shika jembe ukalime. Mtoto yule anapolima kidogo tu mikono yote inamuuma na kuanza kuchubuka huku ikitokea malengelenge! Machozi yatamlenga na kujiuliza kumbe “kilimo ni kigumu hivyo”.
Hili linanikumbusha nilipoenda kuanza shule ya Sekondari miaka mingi nyuma kwenye shule ya Wazazi ya Boza, Pangani Tanga. Nakumbuka mtoto mmoja binti wa familia ya kitajiri aliyeletwa bweni kuanza maisha na kupaona mahali penyewe palivyo (wakati ule). Binti yule aliangusha kilio gari la wazazi wale lilipoondoka kumuacha na kwa karibu wiki nzima alikuwa hana raha mtoto wa watu, akigoma kula na tunashukuru Mungu hakukuwa na Facebook wala Whatsapp enzi hizo, wala Instagram! Kilichomsaidia binti yule (msema kweli Mpenzi wa Mungu) – ni kuwa alijaliwa “Neema za Allah” na vijana wengi (mimi si mmoja wapo) walijitolea kumsaidia kwa kazi zake mbalimbali – hasa ilipofika zamu ya kwenda kubeba kuni!
Baada ya muda alizoea, akazoea maisha ya kule kwani asingeweza kuwapa vijana wote vile walivyohitaji bila ya kujichafua jina lake. Miaka minne baadaye alipohitimu binti yule alikuwa ni “mama” akiwasaidia mabinti wengine walioifika pale na baadaye akaja kuolewa na mlalahoi mmoja. Aliingia shule akiwa hajui jinsi ya kushika kijiko, alihitimu akijua kushika mwiko; aliingia akiwa na madaha, alitoka akiwa na staha.
Ndugu zangu, ufisadi ulikuwa ni kama dawa ya kulevya; taratibu taratiu watu wakauzoea na mwisho wa siku wakata arosto.
Uchumi wetu na maisha yetu kama taifa na kama mtu mmoja mmoja yalihitaji dozi ya dawa hii ya ufisadi ili mambo yaende. Alichofanya Magufuli na ambacho anaendelea kufanya (japo naona kama mwendo umepungua kidogo) ni kuwakatisha watu kupata dawa hii haramu. Matokeo yake watu sasa wako katika hali ya kuonesha withdrawal symptoms. Yaani, watu sasa wanagundua kuwa hawawezi kuishi bila kupata kitu kidogo kwenye damu zao. Kuna wengine ambao wanaona labda asingefanya kwa ukali hivi kwani wakati mwingine mtu anapokatishwa kutumia madawa kwa ghafla anaweza kuishia kuumwa sana na hata kufa! Je, Magufuli angefanya taratibu, abembeleze, asiguse sana uchumi na aachie achie kidogo ili watu wasiumie?
Ndugu zangu, leo hii wapo watu wanapata shida. Kuanza kumomonyolewa na kubanduliwa kwa mfumo wa utawala wa kifisadi kunawafanya watu wakose pa kushikilia. Wenye kulia wanalia, wenye kuumia wanaumia lakini nawaambia kwa uthabiti kabisa wa moyo kuwa hakuna wakati muhimu sana kwa historia ya Taifa letu kama wakati huu. Miaka hii mitatu ya mwanzo ya Rais Magufuli inanithibitishia kabisa kuwa tulichelewa sana na sasa maumivu tunayoyaona ni maumivu ya mtu aliyechelewa kupata tiba na sasa analazimika kufanyiwa upasuaji mkubwa; si mchezo, si lele mama.
Miaka hii mitatu ya kujaribu kuvunja ufisadi, kujenga taifa la watu wanaojiamini na kujitegemea kifikra si jambo rahisi. Makosa yatafanyika, matatizo mengine yataibuliwa, vingine vitaharibiwa lakini kiujumla wake maisha yataenda tu ndugu zangu. Hata wagonjwa wanapofanyiwa upasuaji si wote wanapona na wakati mwingine kunatoke “complications” lakini nia na uthubutu wa madaktari hauwezi kupuuzwa au kubezwa.
Miaka mitatu baadaye ninapoangalia taifa letu linapokwenda sina sababu yoyote ya kujuta kukata marudio na mwendelezo wa mfumo wa utawala wa kifisadi. Sina majuto ya kuunyoshea kidole na kuukataa hata kama ungerudishwa kwa kisingizio cha “mabadiliko” ya kuzungusha mikono. Mambo yote leo yanafanyika nilivyotarajia? La hasha! Kuna vitu ambavyo ningependa vifanyike na havifanyiki au visifanyike na vinafanyika? Si kidogo! Lakini, kutengeneza nidhamu mpya, njia mpya na mwelekeo bora wa kitaifa linafanyika? Bila ya shaka!
Miaka miwili ijayo, itatupa mwanga zaidi; tutaona zaidi mafanikio ya utawala huu na nina uhakika Watanzania wengi zaidi – pamoja na maumivu na usumbufu wa sasa – watasimama na kusema tunahitaji miaka mingine mitano. Gharama ya kujenga mfumo wa maendeleo ni kubwa sana na tumeanza kuilipa. Nina uhakika yatafanyika masahihisho ya maeneo yanayosumbua sasa hivi. Tusije kuthubutu kuangalia nyuma na kutamani kule tulikotoka. Tukatae kabisa kuambiwa ati wakati wa Kikwete na Mkapa ulikuwa ni mzuri sana kwa sababu tulikula “nyama, matikiti maji na vitunguu saumu”.
Kwamba, kwa vile tuliishi katika Misri ya Ufisadi basi ilikuwa nzuri kwa sababu tulikuwa salama na wenye Amani. Tuwakatae na kuwapinga wanaotaka tukumbuke Misri ile ati tu kwa vile huku kwenye nchi ya ahadi kumbe tunatakiwa kufanya kazi, kuhenyeka na kufanya kazi kama uhai wetu unategemea.
Tusonge mbele kwa jitihada, ufanisi, na uwajibikaji. Tukifanya tunachopaswa kufanya basi kile tunachokifanya tutaona kweli kinatupasa!
Niandikie: klhnews@gmail.com