Rufiji dam
JF-Expert Member
- Feb 20, 2020
- 3,803
- 8,794
Tokea kuingia kwa janga la Ukimwi kulikuwepo na magari ya sinema yakionyesha madhara na athari za gonjwa hili ambalo lilikuwa na majina kedekede. Kama kawaida yetu wengi sana ndugu zetu wakadharau na kukebehi kuwa hauwezi kula pipi na ganda lake. Matokeo yake kila sehemu ni mwathirika wa janga hili.
Corona nalo janga tena ni janga hasa kushinda hata huo ukimwi japo vyote ni Kulwa na Doto. Tunaambiwa tusijazane lakini watu kama kawaida wanashupaza shingo. Suala la kuvaa Barakoa nalo lina ugumu gani yaani mpaka Makonda atamke tena kwa vitisho ndio tuamini. Hili gonjwa ni hatari sana kama hauna kazi ya kufanya sehemu za mkusanyiko wa watu sio lazima uonekane huko ikibidi vaa mask. Au nayo hauwezi kupumua huku unajiziba na ganda.
UKIFA NA CORONA UNATUPWA KAMA MZOGO WA MBWA ALIYEGONGWA NA GARI.
Corona nalo janga tena ni janga hasa kushinda hata huo ukimwi japo vyote ni Kulwa na Doto. Tunaambiwa tusijazane lakini watu kama kawaida wanashupaza shingo. Suala la kuvaa Barakoa nalo lina ugumu gani yaani mpaka Makonda atamke tena kwa vitisho ndio tuamini. Hili gonjwa ni hatari sana kama hauna kazi ya kufanya sehemu za mkusanyiko wa watu sio lazima uonekane huko ikibidi vaa mask. Au nayo hauwezi kupumua huku unajiziba na ganda.
UKIFA NA CORONA UNATUPWA KAMA MZOGO WA MBWA ALIYEGONGWA NA GARI.