Tulifanikiwa kupata nafasi ya katiba mpya tusisahau kuweka mambo haya

chawa wa mama

JF-Expert Member
Jun 8, 2020
289
1,070
1. Tume huru inayowajibika kwa wapiga kura sio kwa serikali au mtu.
2. Kupima afya za akili za wagombea kabla hata ya kuchukua fomu, tena na daktari maalumu.

3. Kuweka ukomo kwa wagombea ubunge.

4. Kigezo cha uwajibikaji kipimwe na tume maalumu, iwe rais, mbunge au diwani. Kama ni rais ikiona hawajibiki imwondoe madarakani kwa kura za wananchi sio bungeni.

5. Jaji mkuu apatikane kwa kupigiwa kura na wananchi wote.

6. Jaji mkuu, M/Rais au Waziri Mkuu au Rais akistaafu waondolewe kinga ya kushtakiwa.

7. Suala la ajira kuingizwe ktk katiba, tuweke kiwango cha ajira, mfano wasioajiriwa ktk nchi wakifika idadi tutakayojiwekea, basi rais huyo hatufai, aondolewe madarakani.

8. Wakuu wa majeshi wote, waidhinishwe na bunge, na bunge liwe na uwezo wa kuwaondoa madarakani.

Salaam sana!!!!
 
9.Rais apunguziwe madaraka asiwe na uwezo wa kuteua baadhi ya sehemu kama wakuu wa mikoa na wakurugenzi.
10.Kuwepo na utaratibu maalumu wenye kutoa fursa sawa kwa wakuu wa mikoa na wakurugenzi ikiwezekana kuwepo na uchaguzi
11.Mawaziri wasitokane na wabunge
12.Mfumo wa elimu ufumuliwe na nchi iwe na sera husika kutoka ngazi ya chini mpaka juu,,,sio le kiwanda,kesho ukiamka kilimo,kesho kutwa kodi
13.Mamlaka zote ziangaliwe upya utendaji wake hasa TRA,TPA ziwekewe mipaka na sera zinazoeleweka.
14.Rais akishachaguliwa kwa kura kuwe na mifumo mingine pia ya kumchuja kuona ana faa au la.
15.Wabunge na wana siasa walipe kodi kama raia wengine

Kuna mengi na mengi
 
Hahaha yani hawahawa wabunge wapitishe hii katiba!!!

Yani wajikaange kwa mafuta yao wenyewe! Wao wanachotaka ni kupitisha vitu vinavyoumiza wananchi ila wao wenye nchi mwendo wa neema tu.

Labda baada ya miaka 50 ijayo.
 
Hahaha yani hawahawa wabunge wapitishe hii katiba!!!

Yani wajikaange kwa mafuta yao wenyewe! Wao wanachotaka ni kupitisha vitu vinavyoumiza wananchi ila wao wenye nchi mwendo wa neema tu.

Labda baada ya miaka 50 ijayo.
Mkuu,Bunge la Katiba si lazima liundwe na Wabunge wa kuchaguliwa....
 
Wakuu wa wilaya na mikoa waingie kwenye uchaguzi na washindanishwe na vyama vingine
 
Majaji wote kuanzia mahakama kuu wawe wanaomba kuupata ujaji na wahojiwe na kamati ya sheria na katiba ya bunge,kamati hii itawachuja na kumplekea majina no 1 ili ateua jaji na uapaji wa majaji hawa ufanywe na jaji mkuu na sio rais,kuondolewa kwenye nafasi ya ujaji ni LAZIMA kundwe tume maalum itakayokuwa na zaidi ya nusu ya wajumbe kutoka nje ya nchi(majaji kutoka foreign countries)ndio itoe uamuzi.
 
1. Tume huru inayowajibika kwa wapiga kura sio kwa serikali au mtu.
2. Kupima afya za akili za wagombea kabla hata ya kuchukua fomu, tena na daktari maalumu.

3.kuweka ukomo kwa wagombea ubunge.

4. Kigezo cha uwajibikaji kipimwe na tume maalumu, iwe rais, mbunge au diwani. Kama ni rais ikiona hawajibiki imwondoe madarakani kwa kura za wananchi sio bungeni.

5. Jaji mkuu apatikane kwa kupigiwa kura na wananchi wote.

6.jaji mkuu, m/rais au waziri mkuu au rais akistaafu waondolewe kinga ya kushtakiwa.

7. Suala la ajira kuingizwe ktk katiba, tuweke kiwango cha ajira, mfano wasioajiriwa ktk nchi wakifika idadi tutakayojiwekea, basi rais huyo hatufai, aondolewe madarakani.

8. Wakuu wa majeshi wote, waidhinishwe na bunge, na bunge liwe na uwezo wa kuwaondoa madarakani.

Salaam sana!!!!
no 8 ni point kubwa mno
 
Hivi Ni kwa NINI wabunge hawalipi Kodi !

Kama hawataki kulipa Kodi Basi wasipitishe mashangingi yao kwenye Hizo barabara zetu ambazo tumezijenga kwa michango ya Kodi zetu wananchi ambao Wengi wetu tuna kipato kidogo Sana.Hii ya wabunge kujitungia Sheria ya kutokulipa Kodi Haina tofauti na wizi.

Ni sawa na kuruhusu watu wenye kipato kikubwa waingie bure,kwenye sherehe ya harusi ambayo imechangishwa kwa watu wenye kipato kidogo,Halafu wale wenye uwezo MKUBWA wa kuchanga waingie bure kwenda Kula na kunywa bueee !

Hii Ni dhambi hata mbele za Mungu.Msipobadili hii Sheria,na kutubu dhambi hii,MTAULIZWA SIKU YA MWISHO(Maana,Mungu Ni Mungu Mwenye haki,Sheria,amri na maagizo yake hayapindishwi ki-ujanja ujanja,eti kwa vile nyie mna cheo.NOOO !)
 
1. Tume huru inayowajibika kwa wapiga kura sio kwa serikali au mtu.
2. Kupima afya za akili za wagombea kabla hata ya kuchukua fomu, tena na daktari maalumu.

3. Kuweka ukomo kwa wagombea ubunge.

4. Kigezo cha uwajibikaji kipimwe na tume maalumu, iwe rais, mbunge au diwani. Kama ni rais ikiona hawajibiki imwondoe madarakani kwa kura za wananchi sio bungeni.

5. Jaji mkuu apatikane kwa kupigiwa kura na wananchi wote.

6. Jaji mkuu, M/Rais au Waziri Mkuu au Rais akistaafu waondolewe kinga ya kushtakiwa.

7. Suala la ajira kuingizwe ktk katiba, tuweke kiwango cha ajira, mfano wasioajiriwa ktk nchi wakifika idadi tutakayojiwekea, basi rais huyo hatufai, aondolewe madarakani.

8. Wakuu wa majeshi wote, waidhinishwe na bunge, na bunge liwe na uwezo wa kuwaondoa madarakani.

Salaam sana!!!!
 
Mkuu wananchi hawawezi kuchagua Jaji badala yake Jaji achaguliwe na wanasheria kupitia TLS Maana wananchi %90 hawana elimu juu ya maswala ya kisheria.
Lakini kwenye Rasim pendekezwa ya Jaji Warioba tulipendekeza Mwanasheria mkuu wa Serkali watume maombi na TLS watusaidie kupata majina matatu yapelekwe Bungeni wabunge wachague kwa niaba yetu.
 
Jaji mkuu apatikane kupitia uteuzi wa tume maalumu ya kijaji au apigiwe kura na TLS na athibitishwe na bunge
 
1. Tume huru inayowajibika kwa wapiga kura sio kwa serikali au mtu.
2. Kupima afya za akili za wagombea kabla hata ya kuchukua fomu, tena na daktari maalumu.

3. Kuweka ukomo kwa wagombea ubunge.

4. Kigezo cha uwajibikaji kipimwe na tume maalumu, iwe rais, mbunge au diwani. Kama ni rais ikiona hawajibiki imwondoe madarakani kwa kura za wananchi sio bungeni.

5. Jaji mkuu apatikane kwa kupigiwa kura na wananchi wote.

6. Jaji mkuu, M/Rais au Waziri Mkuu au Rais akistaafu waondolewe kinga ya kushtakiwa.

7. Suala la ajira kuingizwe ktk katiba, tuweke kiwango cha ajira, mfano wasioajiriwa ktk nchi wakifika idadi tutakayojiwekea, basi rais huyo hatufai, aondolewe madarakani.

8. Wakuu wa majeshi wote, waidhinishwe na bunge, na bunge liwe na uwezo wa kuwaondoa madarakani.

Salaam sana!!!!
Uliona wapi???
 

Similar Discussions

7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom