Kenya 2022 Tulieni, tupo kwenye zoezi la kuhakiki kura na mpaka sasa hakuna aliyekidhi idadi ya kutunukiwa Urais

Kenya 2022 General Election

MK254

JF-Expert Member
May 11, 2013
31,757
48,403
Naona MaCCM humu yamechachamaa kufungua nyuzi ili kutafuta mbinu za kupaka tope uchaguzi uliofanyika Kenya, yanajaribu kutumia hizo mbinu kuficha aibu ya dhuluma zao kwao huko Tanzania.

Ifahamike kawaida baada ya kukamilisha zoezi la kuhesabu kura, huwa hatukimbilii kumtangaza mshindi na kumuapisha kama kwenu huko, huwa lazima kura zihakikiwe kwa mbinu zinazokubalika na wagombea wote, tena mbele ya waangalizi wa kimataifa na vyombo vya habari, ili kuhakikisha anayeshindwa hata akienda mahakamani hatakua na sababu zozote au hoja zozote zenye mashiko.

Kingine, katiba inahitaji mshindi lazima awe aliyekubalika na Wakenya, maana kwamba lazima ashinde kwa asilimia 50%+1 na mpaka sasa hakuna aliyekidhi hicho kigezo, hivyo kuna uwezekano tukarudia zoezi la ushindani baina ya wagombea namba moja na mbili, wengine watoswe.

Hii yote ni kwa ajili ya kuhakikisha tunampata kiongozi anayekubaliwa na wananchi, sio kulazimishiwa mtu. Kwa hivyo tulizeni nyuzi zenu hizo kila mara ooh "Kenya kimenuka", "Kenya kitawaka", "Kenya kitaiva", "Kenya watakatana mapanga".....mumekaa kama mafisi yenye njaa mnasubiri mkono udondoke hamuna hata aibu....ha ha ha!!!
 
Kwenye hili wana CCM wote wamekua kitu kimoja, wanaponda mchakato mzima kuanzia kupiga kura hadi kuchakata matokeo, wanadai mshindi amechelewa kutangazwa? Wapi?? Wenzenu wana siku 7 za kukamilisha kila kitu hiyo kuchelewa mmeitoa wapi, na mbaya zaidi wao ndio wanaoongoza kwa kusema kitanuka, ni kama wanaombea mambo yaende kombo ili wapate kujustify uhuni wao ifikapo 2025.

Wameonesha kutishwa na uwazi hasa wa access waliyopewa vyombo vya habari.

Wasome kwa Id zao utawaelewa, mwanaCCM pekee ambaye yuko neutral ni yule Sunk fallacy mlamba asali, walau anaombea Samia alete mchakato kama ule unaoendelea Kenya ijapo 2025.
 
Kumbe ata Kenya mnajua kuwa CCM ni tatizo.

Ukweli ni kwamba ccm inaogopa sana kitu kinaitwa uwazi, Pia wanatamani mambo yaharibike huko Kenya ili waweze kujustify uchafu waliouzoeya.

Kenya mmeonyesha njia na mimi kama Mtanzania mpenda Haki, Amani, na Maendeleo nawaomba kwa Mungu uchaguzi wenu uhitimike salama
 
Naona MaCCM humu yamechachamaa kufungua nyuzi ili kutafuta mbinu za kupaka tope uchaguzi uliofanyika Kenya, yanajaribu kutumia hizo mbinu kuficha aibu ya dhuluma zao kwao huko Tanzania.

Ifahamike kawaida baada ya kukamilisha zoezi la kuhesabu kura, huwa hatukimbilii kumtangaza mshindi na kumuapisha kama kwenu huko, huwa lazima kura zihakikiwe kwa mbinu zinazokubalika na wagombea wote, tena mbele ya waangalizi wa kimataifa na vyombo vya habari, ili kuhakikisha anayeshindwa hata akienda mahakamani hatakua na sababu zozote au hoja zozote zenye mashiko.

Kingine, katiba inahitaji mshindi lazima awe aliyekubalika na Wakenya, maana kwamba lazima ashinde kwa asilimia 50%+1 na mpaka sasa hakuna aliyekidhi hicho kigezo, hivyo kuna uwezekano tukarudia zoezi la ushindani baina ya wagombea namba moja na mbili, wengine watoswe.
Hii yote ni kwa ajili ya kuhakikisha tunampata kiongozi anayekubaliwa na wananchi, sio kulazimishiwa mtu. Kwa hivyo tulizeni nyuzi zenu hizo kila mara ooh "Kenya kimenuka", "Kenya kitawaka", "Kenya kitaiva", "Kenya watakatana mapanga".....mumekaa kama mafisi yenye njaa mnasubiri mkono udondoke hamuna hata aibu....ha ha ha!!!
Kila laheri Majirani
 
Ruto ndiye rais baada ya Uhuru, ni lazima ashinde, mi ndivyo nafahamu. Watajizungusha ila mwisho wa siku rais ni Ruto!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom