TUMEPOKEA kwa masikitiko makubwa amri ya serikali kusimamisha utoaji hati za ardhi kwa wote wenye nyumba na viwanja huko Kigamboni. Kwa kifupi kulingana na sheria mpya ya ardhi inayotka kumpa uwezo mwananchi kuitumia ardhi kama njia ya kujikwamua na umasikini huu ni uonevu na mauaji ya kiuchumi.
Ni haki kwa kila mtu hata kama ananunua ardhi leo huko Kigamboni kupewa hati ya ardhi ili hao wenye matrilioni ya halali na ufisadi wanapotaka kuja kujenga wanunue ardhi hiyo toka kwa wananchi na sio kwa wajanja wachache serikalini.
Inavyoonekana ni kwamba Wizara ya Ardhi inataka wao na wanasiasa waliowaweka hapo wafaidike pale ardhi hiyo itakapopaa bei na wananchi wa kawaida Kigamboni waendelee kula kisamvu, dagaa na ugali wa bada. Hilo hatulikubali.
Tunaomba serikali itengue uamuzi huo na kama wizara hiyo haina fedha ya kutengeneza hati za umiliki viwanja na ardhi basi wapewe wakala watu au makampuni yenye uwezo kufanya kazi hiyo. Inatuuma sana maana wizara hii ndiyo inachoyachangia kwa kiasi kikubwa umasikini wetu na matatizo yanayotukabili sisi wananchi wa kawaida hapa Tanzania.
Ni haki kwa kila mtu hata kama ananunua ardhi leo huko Kigamboni kupewa hati ya ardhi ili hao wenye matrilioni ya halali na ufisadi wanapotaka kuja kujenga wanunue ardhi hiyo toka kwa wananchi na sio kwa wajanja wachache serikalini.
Inavyoonekana ni kwamba Wizara ya Ardhi inataka wao na wanasiasa waliowaweka hapo wafaidike pale ardhi hiyo itakapopaa bei na wananchi wa kawaida Kigamboni waendelee kula kisamvu, dagaa na ugali wa bada. Hilo hatulikubali.
Tunaomba serikali itengue uamuzi huo na kama wizara hiyo haina fedha ya kutengeneza hati za umiliki viwanja na ardhi basi wapewe wakala watu au makampuni yenye uwezo kufanya kazi hiyo. Inatuuma sana maana wizara hii ndiyo inachoyachangia kwa kiasi kikubwa umasikini wetu na matatizo yanayotukabili sisi wananchi wa kawaida hapa Tanzania.