Tuliambiwa kuwa Idi Amini alikuwa dikteta wa hatari

mtoto wa mchungaji

JF-Expert Member
Oct 24, 2020
279
480
1638439023828.png

Nashindwa kujizuia hili jamaa kuliita Dume na Mwamba wa Afrika

1638437193949.png

1638437533740.png

Tuliambiwa kuwa Idi Amini alikuwa dicteta wa hatari, anakula watu, anakula damu za watu na mambo mengi yanayofanana na hayo lakini siku zinavyozidi kwenda inakuwa tofauti sana. Baba zetu na mama zetu walimuimba sana mashuleni zikiwemo nyimbo za kuudhi kutusi na kashfa za namna kwa Idi Amini Dadaa, Mbio za mchaka mchaka zilikuwa zake pekee wakati ule.

Je, hili dume kweli lilikuwa linakula watu, linakula damu za watu na dicteta?

Baadhi ya mambo niliyoyaona yanashangaza na hayafananini na tuliyo ambiwa. Kwamfano katika kipindi chake cha uongozi Idi Amini Dadaa kuanzia 1971 mpaka 1978 aliupandisha uchumi wa nchi yake kuwa juu ya nchi zote za Afrika mashariki na hata fedha ya Uganda ilikuwa juu ya Tanzania na Kenya kithamani ikichuana na ile dola ya Zimbabwe ya wakati ule.

Alibadilisha jina la Kwini Elizabeti Neshino paki kuwa Ruwenzori neshino paki. Alibadilisha Muschoson Fall kuwa maporomoko ya Kabalega

Alibadilisha jina la Ziwa Albart kuwa ziwa Idi Amini
Alibadilisha jina la barabara ya Kwini Eliza kuwa barabara ya Lumumba
Alibadilisha jina barabara ya Salisbury kuwa barabara ya kwame Nkuruma
Mlima Elgon kuwa Masaba
Aliwalazimisha waganda kuongea kiswahili nchi nzima huku yeye akiongea kiswahili kila mahali.

Alikuwa kiongozi wa kwanza wa kiafirka kusema hadharani kuwa uhuru wa bendera hauna maana yoyote kwa muyuganda, bari uhuru wa kiuchumi ndiyo uhuru kamili kwa mutu ya Uganda kwani wakati anaingia madarakani uchumi wote ulikuwa umeshikwa na waingereza, wahindi na waislael.

Aliwai sema kuwa Uganda ni ya waganda na Israel ni ya waisrael na kama Yesu atakataa amuhukumu sasa hivi.

Aliwafukuza wazungu, wahindi na wana wa Israel nchini Uganda kwa kuwapa masaa 24 na nchi ilimilikiwa na waganda wenyewe kwa miaka 9 na uchumi ulikua kwa kasi ya ajabu.

1638439692844.png


Mi nahisi Afrika kuna tatizo. Na hili nene dikteta tufundishwa maana yake upya linazidi kutupoteza.
 
Kuna haja ya historia hizi kuchunguzwa upya huenda Kuna dosari mahali.Umenikumbusha methali ya kiafrika kuwa "mpaka pale simba atakapopata mwandika historia wake,nje ya hapo historia itaendelea kumtukuza mwindaji".
 
Uchumi kuwa mikononi mwa wananchi 100% ni vigumu. Uchumi unahitaji external na internal forces. Unapowatoa wageni unakosa kiungo na external forces. Hapa Waganda walilamba flat baada ya kuwatoa Wazungu, Waisrael na Wahindi.
 
Kama tu wazungu walituone na wanaendelea kutuonea lakini Amini aliwaonea wazungu huyu kweli alistahili kuitwa adui wa waafrika kwa kuwakwamisha wazungu?
 
Acheni kutetea ujinga, yule alikua dikteta aliyewaua sana Waganda, tuache hizi dhana kwamba mtu akiwadhulumu au kunyanyasa wazungu tunamuona shujaa. Huo ni ubaguzi wa rangi, wengi mumeaminishwa ubaguzi wa rangi tu ni ule ambao ni dhidi ya weusi.

Ndio maana leo akijitokeza kiongozi dikteta kwa watu wake ila anajikosha kwa kuwatukana wazungu mabepari, hapo anaonwa shujaa.....
 
Mleta mada mbona kama hapo pichani wanamuabudu?? hala fu na hii picha ya chini wame mubeba juu!!/ au macho yangu ina maana wazungu walimkubali san bila shaka hapo ni baada ya ushindi wa kishindo au, mbona walimkubali sana hata nyerere alikubali kubebwa kule UNO UONGO/ mwenye picha aweke hapa nyerere alipo bebwa na wazungu.
 
Acheni kutetea ujinga, yule alikua dikteta aliyewaua sana Waganda, tuache hizi dhana kwamba mtu akiwadhulumu au kunyanyasa wazungu tunamuona shujaa. Huo ni ubaguzi wa rangi, wengi mumeaminishwa ubaguzi wa rangi tu ni ule ambao ni dhidi ya weusi.

Ndio maana leo akijitokeza kiongozi dikteta kwa watu wake ila anajikosha kwa kuwatukana wazungu mabepari, hapo anaonwa shujaa.
Popoma ndan ya giza alovishwa

Sent from my TECNO BC2c using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom