Tulia Akson sio Kiongozi wa CHADEMA na Wala Sio Mahakama: Afuate Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

SHILLINGS

Senior Member
Oct 24, 2013
160
648
Kinachomfanya mtu kuwa ni mbunge ni pale anapokuwa ni mwanachama hai wa chama cha siasa na hii ni kwa mujibu wa katiba. Bunge linapaswa KUHESHIMU ibara ya 71(1)(e) ya KATIBA ya Tanzania.

Bunge siyo Mamlaka ya Rufaa ya Wanachama wa vyama vya Siasa. Kwa maana hiyo, Bunge halina uhalali wowote kujadili taratibu za KINIDHAMU ndani ya CHAMA CHA SIASA. Kwenye sakata linaloendelea hivi sasa Spika Tulia Ackson amepotoka.


IELEWEKE KWAMBA:-

Kamati Kuu na hatimae Baraza Kuu la CHADEMA lilitoa maamuzi juu ya Uanachama wa Halima Mdee na Wenzake na sio Ubunge wao. Kwa lugha rahisi CHADEMA waliwavua uanachama na sio Ubunge wao;

IELEWEKE KWAMBA:-

Kwa mujibu wa Ibara ya 71 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kipengele kidogo cha (e) cha Ibara hiyo kinaeleleza iwapo mbunge atakoma kuwa mwanachama wa chama alichokuwamo wakati alipochaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge, basi atapoteza ubunge wake.

UTATA:-

Kimsingi Halima Mdee na wenzake walikuwa wanachama wa CHADEMA na hawakuteuliwa na chama cha siasa (CHADEMA) kuwa wabunge. Hivyo kwenye muono wa CHADEMA, Halima na wenzake sio wabunge. Taarifa iliyokwenda kwa Spika ni kuvuliwa uanachama kwa wale wanaoitwa wabunge na Ofisi ya Bunge. Sio Wabunge wa CHADEMA kwa kuwa sio wanachama wa CHADEMA.

Ipo hoja kwamba sio kazi ya Bunge au Spika kuhoji wamepatikanaje kama barua ya utambulisho ya NEC imemfikia. Lakini vilevile sio kazi ya Spika kupindisha maamuzi ya vikao halali vya chama badala ya kufuata takwa la kikatiba, ibara ya 71 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kipengele kidogo cha (e). Mchakato wa kisheria wa kuhoji maamuzi ya chama haupaswi kuwa chini ya mwamvuli wa kinga ya Spika wa bunge bali ni mchakato wa kimahakama nje ya bunge.

Zuio lolote la kimahakama dhidi ya Ubunge wao ni zuio dhidi ya Ofisi ya Bunge katika kutekeleza majukumu yake ya kikatiba kwa wale ambao wanawatambua kama wabunge ambayo tayari hawana chama cha siasa ambacho kinawadhamini. Kwa kifupi sio wanachama wa Chama cha Siasa kwa mujibu wa katiba ya chama husika.

KIMSINGI:-

Spika wa Bunge alipaswa kutimizima jukumu lake la kikatiba na Mdee wa wenzake kufuata taratibu zao za kisheria wakiwa nje ya Bunge.
Inawezekanaje Judicial Injunction (Zuio la Mahakama) linatoka baada ya kauli ya Spika lakini Spika anasema kulikuwa na zuio kabla?

HITIMISHO

Kwa kuwa mchakato wote wa kuwapata wabunge hao 19 kutoka CHADEMA kuwa batili, mjadala mpana ulipaswa kujikita katika uadilifu wa Ofisi ya Bunge na Tume wa Taifa uchaguzi. Utaratibu wa kuwapata wabunge haupaswi kuishia CHADEMA, bali unapaswa kuanzia kwenye mchakato mzima wa kuwapata wale wanaoitwa wabunge.
 
It is very simple, kama wakina Mdee walikwenda bungeni kwa tiketi ya Chadema, na Spika anaamini kina Mdee ni wabunge wa viti maalum kupitia Chadema, basi hao Chadema ndio wamewafukuza uanachama wakina Mdee hivyo hawapaswi kuendelea kuwa wabunge wa JMT.

Again, kama Spika anaamini kina Mdee wameonewa na chama chao hivyo wameenda mahakamani kudai haki zao, basi kwanza anatakiwa kuwaondoa bungeni kina Mdee, kwasababu mpaka sasa wapo bungeni bila kuwa wawakilishi wa chama chochote cha siasa, wakishinda rufaa yao mahakamani ndio warudishwe bungeni.
 
It is very simple, kama wakina Mdee walikwenda bungeni kwa tiketi ya Chadema, na Spika anaamini kina Mdee ni wabunge wa viti maalum kupitia Chadema, basi hao Chadema ndio wamewafukuza uanachama wakina Mdee hivyo hawapaswi kuendelea kuwa wabunge wa JMT.

Again, kama Spika anaamini kina Mdee wameonewa na chama chao hivyo wameenda mahakamani kudai haki zao, basi kwanza anatakiwa kuwaondoa bungeni kina Mdee, kwasababu mpaka sasa wapo bungeni bila kuwa wawakilishi wa chama chochote cha siasa, wakishinda rufaa yao mahakamani ndio warudishwe bungeni.
Huyu ajuza ni mbaya kuliko hata Ndugai
 
Kinachomfanya mtu kuwa ni mbunge ni pale anapokuwa ni mwanachama hai wa chama cha siasa na hii ni kwa mujibu wa katiba. Bunge linapaswa KUHESHIMU ibara ya 71(1)(e) ya KATIBA ya Tanzania.

Bunge siyo Mamlaka ya Rufaa ya Wanachama wa vyama vya Siasa. Kwa maana hiyo, Bunge halina uhalali wowote kujadili taratibu za KINIDHAMU ndani ya CHAMA CHA SIASA. Kwenye sakata linaloendelea hivi sasa Spika Tulia Ackson amepotoka.


IELEWEKE KWAMBA:-

Kamati Kuu na hatimae Baraza Kuu la CHADEMA lilitoa maamuzi juu ya Uanachama wa Halima Mdee na Wenzake na sio Ubunge wao. Kwa lugha rahisi CHADEMA waliwavua uanachama na sio Ubunge wao;

IELEWEKE KWAMBA:-

Kwa mujibu wa Ibara ya 71 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kipengele kidogo cha (e) cha Ibara hiyo kinaeleleza iwapo mbunge atakoma kuwa mwanachama wa chama alichokuwamo wakati alipochaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge, basi atapoteza ubunge wake.

UTATA:-

Kimsingi Halima Mdee na wenzake walikuwa wanachama wa CHADEMA na hawakuteuliwa na chama cha siasa (CHADEMA) kuwa wabunge. Hivyo kwenye muono wa CHADEMA, Halima na wenzake sio wabunge. Taarifa iliyokwenda kwa Spika ni kuvuliwa uanachama kwa wale wanaoitwa wabunge na Ofisi ya Bunge. Sio Wabunge wa CHADEMA kwa kuwa sio wanachama wa CHADEMA.

Ipo hoja kwamba sio kazi ya Bunge au Spika kuhoji wamepatikanaje kama barua ya utambulisho ya NEC imemfikia. Lakini vilevile sio kazi ya Spika kupindisha maamuzi ya vikao halali vya chama badala ya kufuata takwa la kikatiba, ibara ya 71 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kipengele kidogo cha (e). Mchakato wa kisheria wa kuhoji maamuzi ya chama haupaswi kuwa chini ya mwamvuli wa kinga ya Spika wa bunge bali ni mchakato wa kimahakama nje ya bunge.

Zuio lolote la kimahakama dhidi ya Ubunge wao ni zuio dhidi ya Ofisi ya Bunge katika kutekeleza majukumu yake ya kikatiba kwa wale ambao wanawatambua kama wabunge ambayo tayari hawana chama cha siasa ambacho kinawadhamini. Kwa kifupi sio wanachama wa Chama cha Siasa kwa mujibu wa katiba ya chama husika.

KIMSINGI:-

Spika wa Bunge alipaswa kutimizima jukumu lake la kikatiba na Mdee wa wenzake kufuata taratibu zao za kisheria wakiwa nje ya Bunge.
Inawezekanaje Judicial Injunction (Zuio la Mahakama) linatoka baada ya kauli ya Spika lakini Spika anasema kulikuwa na zuio kabla?

HITIMISHO

Kwa kuwa mchakato wote wa kuwapata wabunge hao 19 kutoka CHADEMA kuwa batili, mjadala mpana ulipaswa kujikita katika uadilifu wa Ofisi ya Bunge na Tume wa Taifa uchaguzi. Utaratibu wa kuwapata wabunge haupaswi kuishia CHADEMA, bali unapaswa kuanzia kwenye mchakato mzima wa kuwapata wale wanaoitwa wabunge.
Rubbish
 
John Mrema amekonda sana, nadhani mishahara pale ufipa ni tatizo, kwa nini wasibebe tu hizo ruzuku? Mbowe anawakalisha ofisini na Kigaila halafu yeye anaenda kwenye biashara zake
 
Kinachomfanya mtu kuwa ni mbunge ni pale anapokuwa ni mwanachama hai wa chama cha siasa na hii ni kwa mujibu wa katiba. Bunge linapaswa KUHESHIMU ibara ya 71(1)(e) ya KATIBA ya Tanzania.

Bunge siyo Mamlaka ya Rufaa ya Wanachama wa vyama vya Siasa. Kwa maana hiyo, Bunge halina uhalali wowote kujadili taratibu za KINIDHAMU ndani ya CHAMA CHA SIASA. Kwenye sakata linaloendelea hivi sasa Spika Tulia Ackson amepotoka.


IELEWEKE KWAMBA:-

Kamati Kuu na hatimae Baraza Kuu la CHADEMA lilitoa maamuzi juu ya Uanachama wa Halima Mdee na Wenzake na sio Ubunge wao. Kwa lugha rahisi CHADEMA waliwavua uanachama na sio Ubunge wao;

IELEWEKE KWAMBA:-

Kwa mujibu wa Ibara ya 71 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kipengele kidogo cha (e) cha Ibara hiyo kinaeleleza iwapo mbunge atakoma kuwa mwanachama wa chama alichokuwamo wakati alipochaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge, basi atapoteza ubunge wake.

UTATA:-

Kimsingi Halima Mdee na wenzake walikuwa wanachama wa CHADEMA na hawakuteuliwa na chama cha siasa (CHADEMA) kuwa wabunge. Hivyo kwenye muono wa CHADEMA, Halima na wenzake sio wabunge. Taarifa iliyokwenda kwa Spika ni kuvuliwa uanachama kwa wale wanaoitwa wabunge na Ofisi ya Bunge. Sio Wabunge wa CHADEMA kwa kuwa sio wanachama wa CHADEMA.

Ipo hoja kwamba sio kazi ya Bunge au Spika kuhoji wamepatikanaje kama barua ya utambulisho ya NEC imemfikia. Lakini vilevile sio kazi ya Spika kupindisha maamuzi ya vikao halali vya chama badala ya kufuata takwa la kikatiba, ibara ya 71 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kipengele kidogo cha (e). Mchakato wa kisheria wa kuhoji maamuzi ya chama haupaswi kuwa chini ya mwamvuli wa kinga ya Spika wa bunge bali ni mchakato wa kimahakama nje ya bunge.

Zuio lolote la kimahakama dhidi ya Ubunge wao ni zuio dhidi ya Ofisi ya Bunge katika kutekeleza majukumu yake ya kikatiba kwa wale ambao wanawatambua kama wabunge ambayo tayari hawana chama cha siasa ambacho kinawadhamini. Kwa kifupi sio wanachama wa Chama cha Siasa kwa mujibu wa katiba ya chama husika.

KIMSINGI:-

Spika wa Bunge alipaswa kutimizima jukumu lake la kikatiba na Mdee wa wenzake kufuata taratibu zao za kisheria wakiwa nje ya Bunge.
Inawezekanaje Judicial Injunction (Zuio la Mahakama) linatoka baada ya kauli ya Spika lakini Spika anasema kulikuwa na zuio kabla?

HITIMISHO

Kwa kuwa mchakato wote wa kuwapata wabunge hao 19 kutoka CHADEMA kuwa batili, mjadala mpana ulipaswa kujikita katika uadilifu wa Ofisi ya Bunge na Tume wa Taifa uchaguzi. Utaratibu wa kuwapata wabunge haupaswi kuishia CHADEMA, bali unapaswa kuanzia kwenye mchakato mzima wa kuwapata wale wanaoitwa wabunge.
Je Mahakama inataka kuwachagulia CHADEMA aina ya wanachama wanaotakiwa kuwa nao.
 
It is very simple, kama wakina Mdee walikwenda bungeni kwa tiketi ya Chadema, na Spika anaamini kina Mdee ni wabunge wa viti maalum kupitia Chadema, basi hao Chadema ndio wamewafukuza uanachama wakina Mdee hivyo hawapaswi kuendelea kuwa wabunge wa JMT.

Again, kama Spika anaamini kina Mdee wameonewa na chama chao hivyo wameenda mahakamani kudai haki zao, basi kwanza anatakiwa kuwaondoa bungeni kina Mdee, kwasababu mpaka sasa wapo bungeni bila kuwa wawakilishi wa chama chochote cha siasa, wakishinda rufaa yao mahakamani ndio warudishwe bungeni.
Good! Sidhani kama TUlia halielewi suala hili kuwa linapaswa kueleweka hivyo kwa mujibu wa katiba ya jmt,, nadhani anapotosha kwa maksudi
 
Kinachomfanya mtu kuwa ni mbunge ni pale anapokuwa ni mwanachama hai wa chama cha siasa na hii ni kwa mujibu wa katiba. Bunge linapaswa KUHESHIMU ibara ya 71(1)(e) ya KATIBA ya Tanzania.

Bunge siyo Mamlaka ya Rufaa ya Wanachama wa vyama vya Siasa. Kwa maana hiyo, Bunge halina uhalali wowote kujadili taratibu za KINIDHAMU ndani ya CHAMA CHA SIASA. Kwenye sakata linaloendelea hivi sasa Spika Tulia Ackson amepotoka.


IELEWEKE KWAMBA:-

Kamati Kuu na hatimae Baraza Kuu la CHADEMA lilitoa maamuzi juu ya Uanachama wa Halima Mdee na Wenzake na sio Ubunge wao. Kwa lugha rahisi CHADEMA waliwavua uanachama na sio Ubunge wao;

IELEWEKE KWAMBA:-

Kwa mujibu wa Ibara ya 71 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kipengele kidogo cha (e) cha Ibara hiyo kinaeleleza iwapo mbunge atakoma kuwa mwanachama wa chama alichokuwamo wakati alipochaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge, basi atapoteza ubunge wake.

UTATA:-

Kimsingi Halima Mdee na wenzake walikuwa wanachama wa CHADEMA na hawakuteuliwa na chama cha siasa (CHADEMA) kuwa wabunge. Hivyo kwenye muono wa CHADEMA, Halima na wenzake sio wabunge. Taarifa iliyokwenda kwa Spika ni kuvuliwa uanachama kwa wale wanaoitwa wabunge na Ofisi ya Bunge. Sio Wabunge wa CHADEMA kwa kuwa sio wanachama wa CHADEMA.

Ipo hoja kwamba sio kazi ya Bunge au Spika kuhoji wamepatikanaje kama barua ya utambulisho ya NEC imemfikia. Lakini vilevile sio kazi ya Spika kupindisha maamuzi ya vikao halali vya chama badala ya kufuata takwa la kikatiba, ibara ya 71 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kipengele kidogo cha (e). Mchakato wa kisheria wa kuhoji maamuzi ya chama haupaswi kuwa chini ya mwamvuli wa kinga ya Spika wa bunge bali ni mchakato wa kimahakama nje ya bunge.

Zuio lolote la kimahakama dhidi ya Ubunge wao ni zuio dhidi ya Ofisi ya Bunge katika kutekeleza majukumu yake ya kikatiba kwa wale ambao wanawatambua kama wabunge ambayo tayari hawana chama cha siasa ambacho kinawadhamini. Kwa kifupi sio wanachama wa Chama cha Siasa kwa mujibu wa katiba ya chama husika.

KIMSINGI:-

Spika wa Bunge alipaswa kutimizima jukumu lake la kikatiba na Mdee wa wenzake kufuata taratibu zao za kisheria wakiwa nje ya Bunge.
Inawezekanaje Judicial Injunction (Zuio la Mahakama) linatoka baada ya kauli ya Spika lakini Spika anasema kulikuwa na zuio kabla?

HITIMISHO

Kwa kuwa mchakato wote wa kuwapata wabunge hao 19 kutoka CHADEMA kuwa batili, mjadala mpana ulipaswa kujikita katika uadilifu wa Ofisi ya Bunge na Tume wa Taifa uchaguzi. Utaratibu wa kuwapata wabunge haupaswi kuishia CHADEMA, bali unapaswa kuanzia kwenye mchakato mzima wa kuwapata wale wanaoitwa wabunge.
Kila Ubaya utalipwa
 
Kinachomfanya mtu kuwa ni mbunge ni pale anapokuwa ni mwanachama hai wa chama cha siasa na hii ni kwa mujibu wa katiba. Bunge linapaswa KUHESHIMU ibara ya 71(1)(e) ya KATIBA ya Tanzania.

Bunge siyo Mamlaka ya Rufaa ya Wanachama wa vyama vya Siasa. Kwa maana hiyo, Bunge halina uhalali wowote kujadili taratibu za KINIDHAMU ndani ya CHAMA CHA SIASA. Kwenye sakata linaloendelea hivi sasa Spika Tulia Ackson amepotoka.


IELEWEKE KWAMBA:-

Kamati Kuu na hatimae Baraza Kuu la CHADEMA lilitoa maamuzi juu ya Uanachama wa Halima Mdee na Wenzake na sio Ubunge wao. Kwa lugha rahisi CHADEMA waliwavua uanachama na sio Ubunge wao;

IELEWEKE KWAMBA:-

Kwa mujibu wa Ibara ya 71 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kipengele kidogo cha (e) cha Ibara hiyo kinaeleleza iwapo mbunge atakoma kuwa mwanachama wa chama alichokuwamo wakati alipochaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge, basi atapoteza ubunge wake.

UTATA:-

Kimsingi Halima Mdee na wenzake walikuwa wanachama wa CHADEMA na hawakuteuliwa na chama cha siasa (CHADEMA) kuwa wabunge. Hivyo kwenye muono wa CHADEMA, Halima na wenzake sio wabunge. Taarifa iliyokwenda kwa Spika ni kuvuliwa uanachama kwa wale wanaoitwa wabunge na Ofisi ya Bunge. Sio Wabunge wa CHADEMA kwa kuwa sio wanachama wa CHADEMA.

Ipo hoja kwamba sio kazi ya Bunge au Spika kuhoji wamepatikanaje kama barua ya utambulisho ya NEC imemfikia. Lakini vilevile sio kazi ya Spika kupindisha maamuzi ya vikao halali vya chama badala ya kufuata takwa la kikatiba, ibara ya 71 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kipengele kidogo cha (e). Mchakato wa kisheria wa kuhoji maamuzi ya chama haupaswi kuwa chini ya mwamvuli wa kinga ya Spika wa bunge bali ni mchakato wa kimahakama nje ya bunge.

Zuio lolote la kimahakama dhidi ya Ubunge wao ni zuio dhidi ya Ofisi ya Bunge katika kutekeleza majukumu yake ya kikatiba kwa wale ambao wanawatambua kama wabunge ambayo tayari hawana chama cha siasa ambacho kinawadhamini. Kwa kifupi sio wanachama wa Chama cha Siasa kwa mujibu wa katiba ya chama husika.

KIMSINGI:-

Spika wa Bunge alipaswa kutimizima jukumu lake la kikatiba na Mdee wa wenzake kufuata taratibu zao za kisheria wakiwa nje ya Bunge.
Inawezekanaje Judicial Injunction (Zuio la Mahakama) linatoka baada ya kauli ya Spika lakini Spika anasema kulikuwa na zuio kabla?

HITIMISHO

Kwa kuwa mchakato wote wa kuwapata wabunge hao 19 kutoka CHADEMA kuwa batili, mjadala mpana ulipaswa kujikita katika uadilifu wa Ofisi ya Bunge na Tume wa Taifa uchaguzi. Utaratibu wa kuwapata wabunge haupaswi kuishia CHADEMA, bali unapaswa kuanzia kwenye mchakato mzima wa kuwapata wale wanaoitwa wabunge.
Suala hili linahitaji akili ya kawaida sana na inashangaza kwa mtu Tulia, kama PhD yake ya sheria ni ya kweli, jamii ya kawaida inashindwa kuelewa logic aliyotumia huyu mama; Tulia.
Hii inatokana na ukweli kuwa mtu akifukuzwa kazi mahali, na huyu mtumishi asiporidhika na taratibu zilizotumika kumwondoa kazini na akakimbila mahakamani, utumishi wake hukoma pale anapoachishwa kazi hadi pale mahakama itakapotamka aliondolew kimakosa na hivyo arejeshwe kazini na kulipwa stahili zake.
Ila kwa sababu nchi hii ni rahisi mno kuongoza ndipo hapa tulipofika. Kila mtu hujiamulia atakavyo, iwe ni kwa maslahi yake binafsi, kisiasa, kifamilia, kidini au hata kiitikadi
 
1. Hivi mshitakiwa/mdaiwa ktk shauri/kesi hii ya hawa wanawake 19 ni nani? Bunge au CHADEMA..?

2. Wanadai nini hawa wanawake? Uanachama au Ubunge..?

3. Kama ni ubunge, it's too late, wamekosea mahesabu!.. na kama ni uanachama wao, huo ndiyo hakuna nafasi tena, wameshafutwa, kwa hatua hii it's irreversible..!

4. Hawa wamedanganywa. Wangeweza tu kuukoa uanachama na hivyo ubunge wao kwa wakati mmoja kwa kukimbilia mahakamani mara waliposikia fununu za kufutwa uanachama na hiyo ingewawezesha kupata "court injuction" ya kuifunga mikono CHADEMA kuamua lolote juu ya uanachama wao kama alivyofanya Zito Kabwe mwaka 2013..

5. Sasa hapa kila mtu anajiuliza imekuwaje Spika Dr Tulia Ackson adanganye umma kuwa ana nakala ya "court injuction" wakati mpaka wakati huo anatamka hayo (saa 4asb) mahakama ilikuwa haijatoa zuio hilo? Zuio lilitoka saa 9 za alasiri siku hiyo.

Rais Samia (serikali) na Bunge wana nini na CHADEMA kupitia kwa hawa kinamama? Mbona hii ni impunity ya hali juu sana iliyovuka mipaka ya ustaarabu..?

5. Kama wangekuwa makini hawa wanawake, wangeweza kufanya timing kwa kufungua shauri mahakamani kabla hata CC kuamua mwaka Novemba, 2020 la kukihoji chama chao [CHADEMA] uhalali wa mchakato wa kuwafutia uanachama wao. Na wakati shauri likiendelea mahakamani, obviously, wao huku wangekuwa wanakula benefits & privileges za ubunge bila kuliingiza Bunge na Spika Tulia Ackson kwenye mgogoro wa kikatiba na kisheria..

6. Kwa kufanya hiyo namba 3 hapo, wangeendelea kuwa wabunge wa CHADEMA lakini kwa amri tu ya mahakama..

7. Lakini as for now, kimetangulia "kufutwa uanachama" na walinyamaza kimya bila kuchukua hatua.

8. Kwa hili, kama mahakama itafanya kazi yake ya kutafsiri sheria kwa usahihi bila kuingiliwa, basi itapitia proceedings za kuwafukuza uanachama kama zimezingatia katiba na kanuni za chama chao au la..

9. Kama mahakama itaona kuna ukiukwaji wa kanuni na katiba, basi lazima itawarudisha hawa kinamama kwenye chama chao na kuamuru CHADEMA wapitie upya maamuzi yao kwa kuzingatia hadidu za rejea itakayotoa mahakama. Hiyo ndiyo namna sahihi ya hawa kinamama kutetea/kupigania uanachama wao utakaowapa uhalali wa kuendelea kuwa wabunge..

10. As for Spika wa Bunge Dr Tulia Ackson, yeye ndiye kabisaaaa hapaswi kusema chochote isipokuwa kuupokea uamuzi wa CHADEMA kama ulivyo na kuangalia KATIBA ya JMT INASEMAJE na ku - act immediately bila kujali CHADEMA wamekosea au wamewaonea hawa watu maana hiyo siyo kazi ya Spika..

11. Hopefully, baada ya kelele hizi, Spika, Dr Tulia Ackson (labda) akili itamrudia na kubadili maamuzi yake batili haraka kabla karma haijaanza kumtafuna...

CC Pascal Mayalla, JokaKuu Mag3
 
Umefafanua vizuri sana, kuna watu kama Pascal Mayalla wanatumia vibaya sana kupotosha umma. Spika ameshindwa kutii katiba ya nchi ambayo aliapa kuilinda. Kwa nchi ambazo zipo serious hakupaswa kuwa ofisini mpaka sasa. Mhimili unadhalilishwa.
 
Back
Top Bottom