Tulia Ackson: Barabara ya Mbeya- Chunya ni zaidi ya majanga

Lady Whistledown

JF-Expert Member
Aug 2, 2021
1,023
1,609
Spika wa Bunge, Dk Tulia Akson ameitaka Serikali kutenga fedha kwa ajili ya matengenezo ya barabara zinazojengwa ili ziweze kuwa imara wakati wote.

Akizungumza leo Jumanne Aprili 19, 2022 Bungeni jijini Dodoma ameitaja barabara ya kutoka Dodoma kwenda Iringa kuwa ni janga huku akieleza barabara ya Mbeya – Chunya kwamba ni zaidi ya majanga na hivyo kuiomba Serikali kutenga fedha kwa ajili ya matengenezo.

Spika amesema barabara zinajengwa kwa fedha nyingi lakini zinabomoka kwa kuanza na kishimo kidogo na mwisho linakuwa tatizo kubwa.

“Wanachotaka wabunge ni kutenga fedha zitakazotumika kwa ajili ya matengenezo. Barabara inaaza kubomoka kidogo lakini mwisho inakuwa tatizo, mfano ni barabara ya Dodoma- Iringa ambayo ni janga lakini barabara ya Mbeya – Chunya ni zaidi ya janga,” amesema Dk Tulia.

Spika amesema barabara ya Dodoma – Iringa inatakiwa kufumuliwa na kujengwa upya ili kuondoa mashimo na viraka katika barabara hiyo.
 
Chato imepumzishwa
Zamu ya mbeya sasa
Barabara ya Dodoma Iringa kwani ni ya Mbeya? Hii sehemu ya barabara kuu ya Kaskazini. Ni mbovu kuliko kawaida. Ilijengwa kwa wakati moja na barabara ya Dodoma-Babati. Barabara ya Dodoma-Babati ipo bomba sana.

Hii ya Dodoma-Iringa baada ya mwaka moja ilianza kubomoka hovyo. Ilijengwa ya kiwango cha chini sana.
 
Hii barabara ya dodoma-iringa si imejengwa mwaka 2014-2016? Imeshabomoka tayari? Hili ni janga, faida ya 10%
 
Hawa viongozi ni wa ajabu kwani wanashauriwa zijengwe barabara za zege lakini hawataki! Wsnadai wakijenga za zege hawatakuwa na kitu cha kuongea.
 
Barabara ya Dodoma Iringa kwani ni ya Mbeya? Hii sehemu ya barabara kuu ya Kaskazini. Ni mbovu kuliko kawaida. Ilijengwa kwa wakati moja na barabara ya Dodoma-Babati. Barabara ya Dodoma-Babati ipo bomba sana. Hii ya Dodoma-Iringa baada ya mwaka moja ilianza kubomoka hovyo. Ilijengwa ya kiwango cha chini sana.
Tuanze kumtupa ndani aliyesimamia na kuruhusu mkandarasi kulipwa wakati barabara ilikuwa chini ya kiwango...
 
Tuanze kumtupa ndani aliyesimamia na kuruhusu mkandarasi kulipwa wakati barabara ilikuwa chini ya kiwango
Wakati inajengwa Waziri wa ujenzi alikuwa Magu na ilipo kamilika aliipokea mwaka 2016 Magu akiwa Rais na kuifungua rasmi. Kikubwa hapa ni hii barabara kufumuliwa na kujengwa upya kwa kiwango kinachoendana na hadi ya hii barabara. Hii barabara haifunganishi mikoa ya Kusini tu na Dodoma, Bali inaiunganisha Cape Town na Cairo.
 
Tulia yupo Dunia ya wapi yani mpaka Leo ajajua hayo mashimo huwa yanachibwa kwa makusudi na watu wa TANROAD ili badae itangazwe tender ya ukarabati mdogo na wao wachukue tender kupitia vikampuni vyao vya ukandarasi au kampuni za jamaa zao

Watu huwa nawaenda kabisa na sululu wanaanza kuchimba Rami usiku wanatachimba chumba wewe na huenda kuyaongeza hayo mashimo ukubw Kila baada ya siku

Hiyo ndio hujuma inafanyika hakuna sijui chini ya kiwango wala nini

Mtanisamee wapiga deal nimemwaga mboga na ugali
 
Back
Top Bottom