Lady Whistledown
JF-Expert Member
- Aug 2, 2021
- 1,023
- 1,609
Spika wa Bunge, Dk Tulia Akson ameitaka Serikali kutenga fedha kwa ajili ya matengenezo ya barabara zinazojengwa ili ziweze kuwa imara wakati wote.
Akizungumza leo Jumanne Aprili 19, 2022 Bungeni jijini Dodoma ameitaja barabara ya kutoka Dodoma kwenda Iringa kuwa ni janga huku akieleza barabara ya Mbeya – Chunya kwamba ni zaidi ya majanga na hivyo kuiomba Serikali kutenga fedha kwa ajili ya matengenezo.
Spika amesema barabara zinajengwa kwa fedha nyingi lakini zinabomoka kwa kuanza na kishimo kidogo na mwisho linakuwa tatizo kubwa.
“Wanachotaka wabunge ni kutenga fedha zitakazotumika kwa ajili ya matengenezo. Barabara inaaza kubomoka kidogo lakini mwisho inakuwa tatizo, mfano ni barabara ya Dodoma- Iringa ambayo ni janga lakini barabara ya Mbeya – Chunya ni zaidi ya janga,” amesema Dk Tulia.
Spika amesema barabara ya Dodoma – Iringa inatakiwa kufumuliwa na kujengwa upya ili kuondoa mashimo na viraka katika barabara hiyo.
Akizungumza leo Jumanne Aprili 19, 2022 Bungeni jijini Dodoma ameitaja barabara ya kutoka Dodoma kwenda Iringa kuwa ni janga huku akieleza barabara ya Mbeya – Chunya kwamba ni zaidi ya majanga na hivyo kuiomba Serikali kutenga fedha kwa ajili ya matengenezo.
Spika amesema barabara zinajengwa kwa fedha nyingi lakini zinabomoka kwa kuanza na kishimo kidogo na mwisho linakuwa tatizo kubwa.
“Wanachotaka wabunge ni kutenga fedha zitakazotumika kwa ajili ya matengenezo. Barabara inaaza kubomoka kidogo lakini mwisho inakuwa tatizo, mfano ni barabara ya Dodoma- Iringa ambayo ni janga lakini barabara ya Mbeya – Chunya ni zaidi ya janga,” amesema Dk Tulia.
Spika amesema barabara ya Dodoma – Iringa inatakiwa kufumuliwa na kujengwa upya ili kuondoa mashimo na viraka katika barabara hiyo.