Abraham Lincolnn
JF-Expert Member
- Apr 12, 2018
- 2,499
- 4,211
Swali fikirishi,Je ni kwanini Maaskofu,Watawa na makasisi wa Kanisa Katoliki wanaheshimika sana na kuaminika kwa jamii pamoja na waumini wao kuliko madhehebu mengine?
JIBU; Mbali na sababu nyingine kama vile viwango vya elimu,Nimegundua kwamba kitendo cha Watawa wakatoliki kula nadhiri za useja na kujitoa kufunga ndoa na kanisa zimewafanya waumini wao kuwaheshimu sana.Jaribu kufikiria kiongozi ni Askofu alafu ana mke na watoto,Je kwa akili za haraka haraka mtu huyu kweli ataweza kulitumikia kanisa na kulisha kondoo za Bwana? Ni vigumu kutumikia mabwana wawili! Patia picha huyo askofu ametoka nyumbani amekorofishana na mke wake na mtoto wake wa kiume anatumia madawa ya kulevya na binti yake amefumaniwa gesti na mume wa mtu! Huyu kweli atakuwa sawa?! Sikatai huenda wapo mapadre wanaenda kinyume na nadhiri zao lakini angalau anafanya hivyo akijua anakosea na haiwi kwa uhuru na wingi kiasi cha kuathiri kanisa kiujumla!
Hata wewe ukiona mtu amejitoa maisha yake kutokuoa/kutokuolewa kwa ajili ya Kristu lazima utampatia heshima kuliko yule aliyeoa/kuolewa huku anahudumia kanisa!
JIBU; Mbali na sababu nyingine kama vile viwango vya elimu,Nimegundua kwamba kitendo cha Watawa wakatoliki kula nadhiri za useja na kujitoa kufunga ndoa na kanisa zimewafanya waumini wao kuwaheshimu sana.Jaribu kufikiria kiongozi ni Askofu alafu ana mke na watoto,Je kwa akili za haraka haraka mtu huyu kweli ataweza kulitumikia kanisa na kulisha kondoo za Bwana? Ni vigumu kutumikia mabwana wawili! Patia picha huyo askofu ametoka nyumbani amekorofishana na mke wake na mtoto wake wa kiume anatumia madawa ya kulevya na binti yake amefumaniwa gesti na mume wa mtu! Huyu kweli atakuwa sawa?! Sikatai huenda wapo mapadre wanaenda kinyume na nadhiri zao lakini angalau anafanya hivyo akijua anakosea na haiwi kwa uhuru na wingi kiasi cha kuathiri kanisa kiujumla!
Hata wewe ukiona mtu amejitoa maisha yake kutokuoa/kutokuolewa kwa ajili ya Kristu lazima utampatia heshima kuliko yule aliyeoa/kuolewa huku anahudumia kanisa!