Tukumbushane vipindi vya ITV, CTN, na DTV 1994

Wana jamvi leo nimeona japo turevew miaka hii ya nyuma vipindi vya television enzi zile 1994 kuibukia miaka ya 2000. Binafsi nakumbuka mbali sana hasa vipindi vya television ITV mfano Egoli place of Gold, 21 jump Street, Time trax, movie ya V, Rino Renz, vichekesho Kama Fresh Prince of bell air, family matters, Living Single ya Queen Latifa, Tausi ya mjuba, Vitimbi(masakuu, Ojwang' Othrong'ong'o) Vioja Mahakamani, Mambo hayo ya kina Waridi, Sumbi, bocha na Aisha. Pia kulikuwa na Tamthiliya kama The young and the restless, Sun seat beach, na Acapulco bay.
Aidha nakumbuka tulikuwa tunaangalia UEFA kupitia CFI(Canal France International). Matangazo nakumbuka kama Revola, komoa, lotion ya Jambo, hebu vingine mnisaidie CTN na DTV. Je kipindi kile watangazaji unawakumbuka? Wa ITV, CTN, na DTV. Mimi kwa itv namkumbuka Suzan Mongi nilimpenda sana sana. Karibuni tuflash back jamani.
Hyo rinorenz 21jumpstreet umenikumbusha mbali sana ndugu yangu natamani one day virudiwe big up mkuu kwa kunikumbusha ujana
 
Tausiii ndege wanguu!!ndege wangu wa fahari!

Nakumbuka sinta binti Kasri alivyokuja dar kwao pale kwa manjunji M/mala watu tulivunja ukuta kwenda kumshangaa...!!

Asante mleta Uzi!
Hahahah!! Nakumbuka lile tukio liliweka gumzo haswaaa sinta kutua dar... Kipindi hicho bado ni dogo janja ati nlikuwa siamini kama kweli ametua dar, niliona kama miujiza fulani isiyosadikika hahahahah
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom