Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,633
- 697,792
Tungekuwa na tafakuri ndogo kabisa tukaishi maandiko ya misahafu, tungekuwa na dunia nyingine kabisa, Afrika nyingine na Tanzania ya aina yake.... Tungejua tafsiri sahihi na asili ya neno USALITI, tungebatilisha maamuzi mengi sana
Daima wanaotusaliti si watu baki, si watu wa mbali la hasha! Bali ni watu tuliowapenda na kuwaamini sana! Sometimes tuliowasaidia wakaweza kusimama wenyewe... Mchawi wako hatoki mbali, msaliti wako yu sehemu ya maisha yako
Msaliti wako ni mtu unayecheka naye na kufanya naye mengi pamoja, ya sirini na ya wazi, yanayojulikana na yasiyojulikana... Matukio mengi ukiyaangalia vema unajua tu kwamba hii ni INSIDE JOB! yani ni mchongo toka ndani mtu wa nje ni ngumu kujua ramani ya ndani
Laiti tungeyaishi maandiko!!! Usaliti haukuanza Leo! Ulikuwepo upo na utaendelea kuwepo! Shetani alimsaliti Mungu pale Eden kwa kutoa siri za mbinguni (huyu ndie baba wa usaliti) Yuda alimsaliti Bwana Yesu, Samson mwenye nguvu nyingi alisalitiwa na binti mrembo Delilah... Tawala na falme nyingi zilianguka na kuangamia kabisa kutokana na usaliti toka ndani... Saddam husseein alisalitiwa na mjomba wake wa damu...
Wale tuliowaamini sana, ndio watu ambao daima wametupa maumivu yasiyomithilika! Wazazi na walezi waliowabeba baadhi ya watoto ama ndugu kwa mbeleko kubwa ya upendeleo (uziwanda) ndio wamekuja kuwaletea majuto mengi katika maisha yao baadae!
Unapojaaliwa tunu ya kuongoza kaya! Jitahidi mno kutumia hekima ya kimungu katika mizania ya haki, jitahidi sana mizani yako isiegemee wala kuzidi upande wowote
Wachukulie watoto wote kwa USAWA, wa kambo, wa kufikia wa jirani na wa kwako pia! Angalia baraka za wanao zisije zikapokwa kwa kuwanyanyapaa wale wasio wako! Maisha bado yapo! Angalia hao wanao unaowabeba kwa mbeleko kubwa ya upendeleo wasije kuwa fimbo ya kuja kukuchapa wewe mwenyewe... Kadiri utakavyo wabeba mgongoni watataka uwabebe mpaka mabegani kishapo kichwani... Wakifika huko tegemea anguko kuu...
Unaposimama mbele ya kaya.. Usiangalie mkono wako wa kulia tu na kudhani hawa wa kulia kwako ndio bora wakutumainia na kuamini kabisa, watakulemea mwishoni na kukuangusha
Tengeneza mtandao sawa toka chini mpaka juu, kushoto mpaka kulia juu mpaka chino mbele mpaka nyuma... Mbali mpaka karibu
Wa kule mpe ukiranja, wa huku mpe jiko wa chini mpe ukokoroni wa pembeni mpe kibubu... Alimradi kila mmoja katika kusanyiko lile apate kidogo na watu wake wafurahi
Usiruhusu malalamiko yawe mengi. Upepo kwenye tairi moja ukizidi sana gari linakosa balance... Jitahidi motokari yako upepo ufanane kwenye gurudumu zote
Nitamatishe kwa kukumbusha kwamba KONDA ni KONDA tuu! Kumbuka alikuwa mpiga debe! Makinika naye anatamani kuwa dereva.... LAKINI kama haitoshi ana ndoto za kutaka kuwa MMILIKI....!
Chonga kinyago chako lakini angalia kisije kukutisha mwenyewe UKAKIKIMBIA.....
KIKULACHO KI NGUONI MWAKO!
Jr
Daima wanaotusaliti si watu baki, si watu wa mbali la hasha! Bali ni watu tuliowapenda na kuwaamini sana! Sometimes tuliowasaidia wakaweza kusimama wenyewe... Mchawi wako hatoki mbali, msaliti wako yu sehemu ya maisha yako
Msaliti wako ni mtu unayecheka naye na kufanya naye mengi pamoja, ya sirini na ya wazi, yanayojulikana na yasiyojulikana... Matukio mengi ukiyaangalia vema unajua tu kwamba hii ni INSIDE JOB! yani ni mchongo toka ndani mtu wa nje ni ngumu kujua ramani ya ndani
Laiti tungeyaishi maandiko!!! Usaliti haukuanza Leo! Ulikuwepo upo na utaendelea kuwepo! Shetani alimsaliti Mungu pale Eden kwa kutoa siri za mbinguni (huyu ndie baba wa usaliti) Yuda alimsaliti Bwana Yesu, Samson mwenye nguvu nyingi alisalitiwa na binti mrembo Delilah... Tawala na falme nyingi zilianguka na kuangamia kabisa kutokana na usaliti toka ndani... Saddam husseein alisalitiwa na mjomba wake wa damu...
Wale tuliowaamini sana, ndio watu ambao daima wametupa maumivu yasiyomithilika! Wazazi na walezi waliowabeba baadhi ya watoto ama ndugu kwa mbeleko kubwa ya upendeleo (uziwanda) ndio wamekuja kuwaletea majuto mengi katika maisha yao baadae!
Unapojaaliwa tunu ya kuongoza kaya! Jitahidi mno kutumia hekima ya kimungu katika mizania ya haki, jitahidi sana mizani yako isiegemee wala kuzidi upande wowote
Wachukulie watoto wote kwa USAWA, wa kambo, wa kufikia wa jirani na wa kwako pia! Angalia baraka za wanao zisije zikapokwa kwa kuwanyanyapaa wale wasio wako! Maisha bado yapo! Angalia hao wanao unaowabeba kwa mbeleko kubwa ya upendeleo wasije kuwa fimbo ya kuja kukuchapa wewe mwenyewe... Kadiri utakavyo wabeba mgongoni watataka uwabebe mpaka mabegani kishapo kichwani... Wakifika huko tegemea anguko kuu...
Unaposimama mbele ya kaya.. Usiangalie mkono wako wa kulia tu na kudhani hawa wa kulia kwako ndio bora wakutumainia na kuamini kabisa, watakulemea mwishoni na kukuangusha
Tengeneza mtandao sawa toka chini mpaka juu, kushoto mpaka kulia juu mpaka chino mbele mpaka nyuma... Mbali mpaka karibu
Wa kule mpe ukiranja, wa huku mpe jiko wa chini mpe ukokoroni wa pembeni mpe kibubu... Alimradi kila mmoja katika kusanyiko lile apate kidogo na watu wake wafurahi
Usiruhusu malalamiko yawe mengi. Upepo kwenye tairi moja ukizidi sana gari linakosa balance... Jitahidi motokari yako upepo ufanane kwenye gurudumu zote
Nitamatishe kwa kukumbusha kwamba KONDA ni KONDA tuu! Kumbuka alikuwa mpiga debe! Makinika naye anatamani kuwa dereva.... LAKINI kama haitoshi ana ndoto za kutaka kuwa MMILIKI....!
Chonga kinyago chako lakini angalia kisije kukutisha mwenyewe UKAKIKIMBIA.....
KIKULACHO KI NGUONI MWAKO!
Jr