Tukumbushane muziki aina ya mchiliku au mnanda na vituko vyake enzi hizo upo kwenye chati

KOLOKOLONI

JF-Expert Member
Mar 7, 2014
2,477
2,360
Je unakumbuka mnanda/mchiliku na vituko na matukio yake enzi hizo upo kwenye chati.je umeumis mziki huu wenye radha ya aina yake? Ebu tutajia nyimbo unayoijua
 
Daaaa,kitambo,Namkumbuka jamaa mmoja alikuwa anaitwa kibaka mdudu,alikuwa mcheza mchiriku matata sana,pia marehemu mkama shapu[Afande]alikuwa hakosekani kuangalia usalama watu wasipolwe.....
 
atomic! mnanda wa atomic , mziki wa bisibisi, gongo,visu,bangi na ngada looooong time ukipigwa mtaaani lazima muibiwe.
 
Teh teh te naukumbuga ule wa mgambo na kondakta mgambo ataki kulipa nauli anasema yeye chombo cha dola
 
Dah,long time kitambo Mkuu,enzi hizo Maskani Kuu ya Mchiriku ilikuwa Mwembe Yanga Famagusta kwenda mpaka kwa Mpogo. Vibao vya enzi zile kama vile Kinyago Msela,Saidi Kipaka/Masikani Famagusta nk vilikuwa balaa,hapo ni moshi wa msuba kama vile mpo Jamaica. Kwa upande wa sasa Vijana wanajitahidi sana kuuendeleza huu Mziki but cha kusikitisha haupewi kipaumbele kwenye Media karibu zote kama inavyopewa taarabu na wakati huu Mziki una mafundisho makubwa sana kwa hali ya sasa na vile vile ni rahisi sana kuwafikia wahusika wakuu ambao ni Vijana. Embu sikiliza wimbo kama Usije Mjini Kaka,una mafundisho makubwa sana kwa wale Vijana wakijijini wenye mawazo kuwa Mjini ndio kila kitu,jamaa anawaambia kuwa huku Mjini ajira kubwa ni kuokota makopo na scrapers.

Na upande wa pili wakusikitisha kwenye huu mziki ni kuondokewa na waimbaji/watunzi wake mahiri kama vile Omary Omary,Juma Mpogo,General Lupozi n.k R.I.P.
 
Kitu cha kazi ya duka bwana wewe! Acha kabisa ya nini utumbo utupweee wakati wenyewe twalia ndizi teh teh na kitu cha "Kupata majaaliwa" cha Omari Omari weee nikikiskia tu mdundo mi ful kutegesha nyonga standby! Dah mnanda una raha yake askwambie mtu
 
Nakumbuka kuna kundi lilitoka maeneo ya mbezi msakuzi nikakutana nao eneo la makabe nika paki gari pembeni ili kuwapisha, dada moja alisogea kwenye mlango akanengua huku amelegeza macho, mpaka nikaona kizunguzungu
 
Hivi huu muziki asili yake ni wapi? Yani historia yake ikoje? Mziki huu naukubali sana.
 
Teh teh nakumbuka jirani yetu pale mitaa ya kongowe kibaha alikuwa na sherehe yake ya harusi mwanzo wa miaka ya 2000 hivi basi usiku pale ilikuwa jirani na home,umeme wamekuja kuchukua home mbali kidogo,basi mwenye shughuli anataka kupiga taarabu na mnanda tu masela wanataka bongo fleva wameshachoka kusubiri mida ya saa 8 usiku hiyo walifanya tumbwili jamaa wakakata waya wa umeme kwa shoka,
Short ilirudi home bahati iliwahi kujizima kidogo tuunguze nyumba, toka siku hiyo hata aje nani home anataka moto hatupeleki ilikuwa fundisho,
Lakini ilikuwa siku hiyo harufu ya bangi mtaa mzima nakumbuka sijui hayo mambo yako mpala leo
 
Teh teh nakumbuka jirani yetu pale mitaa ya kongowe kibaha alikuwa na sherehe yake ya harusi mwanzo wa miaka ya 2000 hivi basi usiku pale ilikuwa jirani na home,umeme wamekuja kuchukua home mbali kidogo,basi mwenye shughuli anataka kupiga taarabu na mnanda tu masela wanataka bongo fleva wameshachoka kusubiri mida ya saa 8 usiku hiyo walifanya tumbwili jamaa wakakata waya wa umeme kwa shoka,
Short ilirudi home bahati iliwahi kujizima kidogo tuunguze nyumba, toka siku hiyo hata aje nani home anataka moto hatupeleki ilikuwa fundisho,
Lakini ilikuwa siku hiyo harufu ya bangi mtaa mzima nakumbuka sijui hayo mambo yako mpala leo

nimecheka sana,yani umefanya siku yangu ianze vizuri!
 
Daaaa,kitambo,Namkumbuka jamaa mmoja alikuwa anaitwa kibaka mdudu,alikuwa mcheza mchiriku matata sana,pia marehemu mkama shapu[Afande]alikuwa hakosekani kuangalia usalama watu wasipolwe.....

Huyo mdudu ndo Hamadi mdudu? alishawahi kuimbiwa ule wimbo wa utakwenda jela pasipo kutegemea?
, kama ni huyo namfahamu, siku hizi amekuwa mtu mzima, mpole huyo zile vurugu zimeisha na ujana.
 
namkumbuka kibaka mdudu....., kipindi nakaa mtogole jamaa walikuwa wanaomba umeme kufanyia mazoezi .....
 
Zamani pale Msasani zilipo ofisi za Zantel na New Msasani Club kulikuwa kunapigwa mnanda kila weekend...

Palikuwa na eneo la wazi basi wale Wamakonde wa kwa Mussa Hassan (Msasani), Wazaramo na wenyeji wengine wa maeneo ya karibu walikuwa wanajazana hapo...

Kuna jamaa zetu fulani wanaitwa Chikokoti na Said Makacholi ulikuwa huwakosi hapo kwenye disco vumbi hilo...

Nakumbuka hizi nyimbo kama Nipeleke nipeleke, Mama nataka uji au Mama nipe Panadol naumwa gono mimi...
 
Huu mziki asili yake pwani yaani wazaramo ambapo kama unavyoona wale wanaojiita hiphop na wabanapua basi mchiliku uliku kama hiphop na mdundiku au mduara ulikuwa wa wapana pua. Kiukweli ni mziki mzuri kuuzikia ila unafujo sana kwenye show za live.siku hizi umekuwa mziki wa kazi kama vile dogo mfaume, ferouz na r.i.p omar omari
 
Duhh kitambo sana. Ukute kuna Mwali anatolewa ndani, yaani hapo ni mapigo ya Mchiriku na Mdundiko kwa kwenda mbele.
 
nawakubali sana Jagwa music wanapiga mnanda kinoma km vibao vyao Kondakta,jela,saidi misape....yan balaa
 
Back
Top Bottom