Philipo D. Ruzige
JF-Expert Member
- Sep 25, 2015
- 9,412
- 26,887
Ila kiujumla sadaka walizotoa wenzetu zimefanikisha mengi sana. Ikiwepo upatikanaji wa uhakika wa huduma na haki za wanafunzi.Kusoma chuo kikuu bongo ni sawa na kupita JKT.
Tuliwahi kucheleweshewa boom miezi miwili, hali ilikua mbaya kweli, kama kawaida taarifa zikasambaa fasta UDSM, MZUMBE, St. JOSEPH, IFM, ARDHI, TUMAINI, KAMPALA kuitisha mgomo wa kuingia darasani J3 yake.
Sijui FFU walipata taarifa vipi, J3 tulikuta defender 3 nje ya vyuo vyote halafu jamaa ndani ya hizo defender wamenuna kinoma. Tukagoma hivo hivo kibishi kibishi. Tulichezea kichapo si cha kitoto, haikuchagua mtu mzima au kijana, mwanaume au mwanamke.
Udom ilikuaga kawaida kukata mawiki bila maji. Unanunua uhai ya 6ltrs , sasa hapo utapambana kukata gogo, kuoga, kunawa uso, kunywa n.k
Sent using Jamii Forums mobile app