Mapambano Yetu
JF-Expert Member
- Aug 14, 2012
- 1,121
- 2,064
Kwanza kabisa shukrani zimwedee mwenyezi Mungu kwa Uhai anaotupatia, bila yeye hakika tusingeweza kuja hamu JF kuleta mawazo yetu.
Ni rejee kwenye mada,
Kama watanzania wenye malengo na nchi yetu ifikie hatua tuache kupelekwa pelekwa kama Meli isiyokuwa na nahodha. Tuamue kufanya kazi kwa manufaa ya familia zetu na nchi Yetu kwa ujumla. Yanayoendelea kwenye ulingo wa siasa ni maingizo na filamu kali zaidi ya ISIDINGO.
Inapotokea Rais akawatumbua wanaoshindwa kuendana na kasi yake maana yake akiwaacha watafanya Manyanga ambayo kesho yataligharimu Taifa. Na kwa sababu hataki kuona manyanga hayo yakifanyika kwenye uongozi wake ndio maana Tumbua Tumbua haziishi kila kukicha. Hapa namaanisha Makosa ya wateule wake moja kwa moja yatakuwa ni yake kama atayaona na akakaa kimya bila kuchukua hatua. Mfano dhahiri ni majuzi tu kwa kilichomkuta Prof. Muhongo.
Sasa inapotokea Rais aliyeko madarakani, kwa macho yanayotazama na kuona, kwa kichwa kinachofikiri na kutafakari huku akisaidiwa na USALAMA WA TAIFA, anapoyaona maovu, au kupewa taarifa za maovu, akaamua kukaa kimya bila kuchukua hatua zozote kwa nini asilaumiwe? Tunapata wapi ujasiri wa kumkingia kifua kuwa yeye hausiki huku wateule wake tukiwawajibisha?
Sasa hivi kila waziri na wateule wengine wa Rais wanatenda kazi zao kulingana na Matakwa ya Rais. Nape alienda kinyume na matakwa akatumbuliwa mara moja. Kilango naye yalimkuta,
Swali: "Kama Rais wa sasa anataka wateule wake waendane na matakwa yake, na analisimamia hilo - (eti kwa maslahi ya Taifa), amejuaje kuwa hao mawaziri na wateule wa Marais waliomtangulia walikuwa hawaendani na kasi za Marais waliokuwa madakani?"
Nawasilisha.
Ni rejee kwenye mada,
Kama watanzania wenye malengo na nchi yetu ifikie hatua tuache kupelekwa pelekwa kama Meli isiyokuwa na nahodha. Tuamue kufanya kazi kwa manufaa ya familia zetu na nchi Yetu kwa ujumla. Yanayoendelea kwenye ulingo wa siasa ni maingizo na filamu kali zaidi ya ISIDINGO.
Inapotokea Rais akawatumbua wanaoshindwa kuendana na kasi yake maana yake akiwaacha watafanya Manyanga ambayo kesho yataligharimu Taifa. Na kwa sababu hataki kuona manyanga hayo yakifanyika kwenye uongozi wake ndio maana Tumbua Tumbua haziishi kila kukicha. Hapa namaanisha Makosa ya wateule wake moja kwa moja yatakuwa ni yake kama atayaona na akakaa kimya bila kuchukua hatua. Mfano dhahiri ni majuzi tu kwa kilichomkuta Prof. Muhongo.
Sasa inapotokea Rais aliyeko madarakani, kwa macho yanayotazama na kuona, kwa kichwa kinachofikiri na kutafakari huku akisaidiwa na USALAMA WA TAIFA, anapoyaona maovu, au kupewa taarifa za maovu, akaamua kukaa kimya bila kuchukua hatua zozote kwa nini asilaumiwe? Tunapata wapi ujasiri wa kumkingia kifua kuwa yeye hausiki huku wateule wake tukiwawajibisha?
Sasa hivi kila waziri na wateule wengine wa Rais wanatenda kazi zao kulingana na Matakwa ya Rais. Nape alienda kinyume na matakwa akatumbuliwa mara moja. Kilango naye yalimkuta,
Swali: "Kama Rais wa sasa anataka wateule wake waendane na matakwa yake, na analisimamia hilo - (eti kwa maslahi ya Taifa), amejuaje kuwa hao mawaziri na wateule wa Marais waliomtangulia walikuwa hawaendani na kasi za Marais waliokuwa madakani?"
Nawasilisha.