Tukubaliane, hatuna wimbo wa taifa

Cicadulina

JF-Expert Member
Sep 8, 2015
961
2,345
Kwa faida tu ya wasomaji, ngoja nieleze historia fupi ya wimbo huu. Katika dunia nzima, hasa Afrika Kusini kwenyewe ulikoanzia, unajulikana kama “Nkosi Sikelel’ iAfrika” – maneno ya lugha ya ki-Xhosa, yenye maana ya “Mungu Ibariki Afrika.”

Mtunzi wake anaitwa Enoch Sontonga, aliyekuwa mwalimu katika shule moja ya misheni ya Kimethodisti, Johannesburg, Afrika Kusini.

Aliutunga ukiwa kama utenzi mwaka 1897. Uliimbwa kwa mara ya kwanza hadharani mwaka 1899 katika ibada ya kuwekwa wakfu mchungaji Boweni, wa Kanisa la Methodist.

Kwaya ya Sontonga na kwaya nyinginezo zikawa zinauimba mara kwa mara katika matukio jijini Johannesburg na Natal. Watu wakaupenda.

Mnamo Januari 8, mwaka 1912, katika mkutano wa kwanza wa Chama cha Wazawa wa Afrika Kusini (SANNC), mtangulizi wa ANC, wimbo huo uliimbwa mara baada ya sala ya kufunga mkutano.

Mwaka 1925, ANC ikauchukua kama wimbo wake rasmi ulioimbwa mwishoni mwa mikutano yake. Tangu hapo, wimbo huo umejulikana nje ya Bara la Afrika kama wimbo wa ANC, kwani ulikuwa ukiimbwa katika mikutano ya ANC katika harakati za ukombozi.

Harakati hizo ndizo zilifikisha wimbo huo hadi kwetu. Nasi tulipopata uhuru, tukauchukua kama wimbo wa taifa, tukautafsiri kwa Kiswahili, tukapunguza baadhi ya aya na kuubakiza kama ulivyo leo.

Zambia nao walifanya hivyo. Namibia pia waliutumia. Zimbabwe nao waliuiga, lakini baadaye “walipopata akili” wakautema, wakatunga wimbo wao.

Kwa kipindi kirefu, Afrika Kusini ilikuwa na “nyimbo mbili za taifa.” Mmoja ulijulikana kama wimbo rasmi na mwingine, usio rasmi.

Wimbo rasmi (uliotumiwa na serikali ya makaburu) uliitwa kwa jina la Die Stem (ki-Afrikaans), yaani Wito wa Afrika Kusini; na usio rasmi (uliotumiwa za wanaharakati wa ANC), ndio huo Mungu Ibariki Afrika.

Siku ANC iliposhinda uchaguzi wa kwanza kidemokrasia mwaka 1994, nyimbo hizo mbili zikatangazwa kuwa nyimbo rasmi za taifa, lakini mwaka 1996 ziliunganishwa; yakachukuliwa maneno huku na huku, ghani ikabaki ile ile ya wimbo wa ANC, ukakarabatiwa na kuwa kama ulivyo leo.

Kwa Afrika Kusini, Nkosi Sikelel’ iAfrika, kabla na baada ya uhuru, ni ishara ya uhuru na mapambano ya ukombozi wao. Unaimbwa katika lugha mbalimbali Kixhosa, Kiingereza, Kisesotho na Kiafrikaans.

Maneno yaliyo katika aya ya kwanza yaliandikwa na mtunzi mwenyewe (Enoch) katika lugha yake ya Xhosa. Mwaka 1927, aliyekuwa mmoja wa washairi maarufu wa nchi hiyo, Samuel Mqhayi, aliongeza aya nyingine saba katika lugha hiyo hiyo.

Kabla ya hapo, mwaka 1923, Solomon Plaatje, mmoja wa waandishi mahiri nchini humo, ambaye pia alikuwa miongoni mwa waasisi wa ANC, ndiye alikuwa mtu wa kwanza kuurekodi wimbo huo katika studio jijini London, akisindikizwa na muziki wa piano uliopigwa na Sylvia Colenso.

Mwaka huo huo, kiwanda cha uchapaji cha Lovedale Press, katika Jimbo la Eastern Cape, kilichapisha nakala yenye aya zote katika kijitabu. Juni 11, 1927, wimbo huo ulichapishwa katika gazeti la Umtetela Wa Bantu, ukaingizwa pia katika kitabu cha ushairi cha Kixhosa kwa ajili ya kuwafundishia watoto shuleni.

Wimbo huo pia uliingizwa rasmi katika kitabu cha nyimbo za Kixhosa kwenye Kanisa la Wapresbyteri kilichojulikana kama Ingwade Yama-culo Ase-rabe, mwaka 1929. Mwaka 1942, Moses Mphahlele, alichapisha nakala nyingine za wimbo huo katika lugha hiyo na kuzisambaza ili umma ukariri vema maneno yake.

Kwaya ya Ohlange Zulu, ya Mchungaji John L. Dube, ndiyo iliyokuza wimbo huo, kwa kuuimba mara kwa mara katika matamasha mbalimbali jijini Johannesburg.

Taratibu ukawa wimbo maarufu katika mikusanyiko ya kidini, kijamii na kisiasa; badaye ukarekodiwa pia na wasanii kina Ladysmith, Black Mambazo, Boom Shaka na Mahotella Queens.

Historia hiyo pekee inaonesha kwamba sisi bado hatuna wimbo. Kama tunavyoimbiwa na wasanii wa CCM kwamba “CCM ina wenyewe,” basi tuna sababu ya kuamini pia kwamba hata wimbo huu tunaouita wa taifa, una wenyewe – na wenyewe ni Afrika Kusini. Nadhani Wazimbabwe waliligundua hilo mapema. Wakaachana nao. Sisi tunangoja nini?

Ni bahati mbaya kwamba vijana wale waliobishana nami hawakuwa wanajua historia ya wimbo huo kama nilivyoieleza hapa. Vinginevyo, walikuwa na hoja; na wangetuaibisha. Tuna wasanii wa kutosha kutunga nyimbo zetu.

Watunge. Kama hatutaki mpya, basi tuchukue zilizopo, zinazoeleza kwa kina historia na utaifa wetu, tuzifanye rasmi nyimbo zetu za taifa, kwani huu tunaoimba sasa si wimbo wetu.


Kwa hisani ya Ansbert Ngurumo

 
leta proposal" iliyoshiba "ya wimbo unaokusudia uwe Wimbo wa taifa lako kiasi kwamba wimbo huo utaondoa maneno ya Mungu ibariki Africa na kudhibitisha maneno hayo hayana maana .
 
umeeleza vyema sana mkuu

Wimbo wa taifa ni nembo muhimu sana ya taifa ila kama nchi kuna mambo mengi bado hayajakaa sawa mitaani walalahoi hawajui hatma ya mlo unaofuata.

hili la "wimbo" na lile la "vazi la taifa" wacha litulie kwanza kama mchakato wa katiba
 
Ndugu ungetoa Credit kwa Mwandishi Ansert Ngurumo aliyeandika hiyo Makala kupitia Gazeti la Mseto liliotoka Alhamisi but umefanya vizuri kuileta jukwaani watu wajue ukweli maana tumekuwa wakuiga tu....
 
leta proposal" iliyoshiba "ya wimbo unaokusudia uwe Wimbo wa taifa lako kiasi kwamba wimbo huo utaondoa maneno ya Mungu ibariki Africa na kudhibitisha maneno hayo hayana maana .
Nadhani hoja ya mleta mada siyo kupinga uwepo wa maneno "Mungu ibariki Afrika" kwamba hayana maana. Kwa jinsi nilivyomwelewa, anasema kwa kiasi kikubwa wimbo huu ulinakiliwa na kutafsiriwa kutoka lugha ambazo ajili yake si Tanzania. Kwa maneno mengine, wimbo huu unakosa "ubunifu wa kitaifa" na melodia za asili za Watanzania, mambo ambayo ni muhimu kwa wimbo wa taifa.

Binafsi nadhani hii ni hoja nzuri inayohitaji mjadala wa kina na wakitaifa. Wizara husika ingeanza kukusanya maoni kuhusu jambo hili mapema iwezekanavyo. Suala hili ni muhimu kuliko hata vazi la taifa.
 
naungana nawe kwa asilimia zote, kwa kuongezea na bila kuharibu bajeti... tuubariki ule wimbo wetu wa
' Tanzania nakupenda' , maana naona umebeba kila sifa na alama za taifa hili.
Na Mimi naunga mkono pia, wimbo wetu wa taifa siyo mbaya, tatizo ni kwamba tumeuiga, tayari hiyo tune yake inajulikana dunia nzima kama wimbo wa taifa wa Afrika kusini. Wimbo wa Tanzania Tanzania nakupenda kwa moyo wote ni pendekezo zuri kuwa wimbo wa taifa.
 
Ndugu ungetoa Credit kwa Mwandishi Ansert Ngurumo aliyeandika hiyo Makala kupitia Gazeti la Mseto liliotoka Alhamisi but umefanya vizuri kuileta jukwaani watu wajue ukweli maana tumekuwa wakuiga tu....
Soma aya nzima na kamtaja
 
Kumbe tumeanza zamani kudesa. Kweli sisi "vlz"
Hata wimbo! Hakuna cha ajabu na wala hatuko pekee etu, wapo wengi mfano wa Cyprus.
 
Duuh kumbe ata zamani vilaza walikuwepo..!!! Fulu kudesea kwa watu! Tanzania ya vilaza
 
Nadhani hoja ya mleta mada siyo kupinga uwepo wa maneno "Mungu ibariki Afrika" kwamba hayana maana. Kwa jinsi nilivyomwelewa, anasema kwa kiasi kikubwa wimbo huu ulinakiliwa na kutafsiriwa kutoka lugha ambazo ajili yake si Tanzania. Kwa maneno mengine, wimbo huu unakosa "ubunifu wa kitaifa" na melodia za asili za Watanzania, mambo ambayo ni muhimu kwa wimbo wa taifa.

Binafsi nadhani hii ni hoja nzuri inayohitaji mjadala wa kina na wakitaifa. Wizara husika ingeanza kukusanya maoni kuhusu jambo hili mapema iwezekanavyo. Suala hili ni muhimu kuliko hata vazi la taifa.
Nadhani hoja ya mleta mada siyo kupinga uwepo wa maneno "Mungu ibariki Afrika" kwamba hayana maana. Kwa jinsi nilivyomwelewa, anasema kwa kiasi kikubwa wimbo huu ulinakiliwa na kutafsiriwa kutoka lugha ambazo ajili yake si Tanzania. Kwa maneno mengine, wimbo huu unakosa "ubunifu wa kitaifa" na melodia za asili za Watanzania, mambo ambayo ni muhimu kwa wimbo wa taifa.

Binafsi nadhani hii ni hoja nzuri inayohitaji mjadala wa kina na wakitaifa. Wizara husika ingeanza kukusanya maoni kuhusu jambo hili mapema iwezekanavyo. Suala hili ni muhimu kuliko hata vazi la taifa.
Nadhani hoja ya mleta mada siyo kupinga uwepo wa maneno "Mungu ibariki Afrika" kwamba hayana maana. Kwa jinsi nilivyomwelewa, anasema kwa kiasi kikubwa wimbo huu ulinakiliwa na kutafsiriwa kutoka lugha ambazo ajili yake si Tanzania. Kwa maneno mengine, wimbo huu unakosa "ubunifu wa kitaifa" na melodia za asili za Watanzania, mambo ambayo ni muhimu kwa wimbo wa taifa.

Binafsi nadhani hii ni hoja nzuri inayohitaji mjadala wa kina na wakitaifa. Wizara husika ingeanza kukusanya maoni kuhusu jambo hili mapema iwezekanavyo. Suala hili ni muhimu kuliko hata vazi la taifa.
Nadhani hoja ya mleta mada siyo kupinga uwepo wa maneno "Mungu ibariki Afrika" kwamba hayana maana. Kwa jinsi nilivyomwelewa, anasema kwa kiasi kikubwa wimbo huu ulinakiliwa na kutafsiriwa kutoka lugha ambazo ajili yake si Tanzania. Kwa maneno mengine, wimbo huu unakosa "ubunifu wa kitaifa" na melodia za asili za Watanzania, mambo ambayo ni muhimu kwa wimbo wa taifa.

Binafsi nadhani hii ni hoja nzuri inayohitaji mjadala wa kina na wakitaifa. Wizara husika ingeanza kukusanya maoni kuhusu jambo hili mapema iwezekanavyo. Suala hili ni muhimu kuliko hata vazi la taifa.
Nadhani hoja ya mleta mada siyo kupinga uwepo wa maneno "Mungu ibariki Afrika" kwamba hayana maana. Kwa jinsi nilivyomwelewa, anasema kwa kiasi kikubwa wimbo huu ulinakiliwa na kutafsiriwa kutoka lugha ambazo ajili yake si Tanzania. Kwa maneno mengine, wimbo huu unakosa "ubunifu wa kitaifa" na melodia za asili za Watanzania, mambo ambayo ni muhimu kwa wimbo wa taifa.

Binafsi nadhani hii ni hoja nzuri inayohitaji mjadala wa kina na wakitaifa. Wizara husika ingeanza kukusanya maoni kuhusu jambo hili mapema iwezekanavyo. Suala hili ni muhimu kuliko hata vazi la taifa.
Nadhani hoja ya mleta mada siyo kupinga uwepo wa maneno "Mungu ibariki Afrika" kwamba hayana maana. Kwa jinsi nilivyomwelewa, anasema kwa kiasi kikubwa wimbo huu ulinakiliwa na kutafsiriwa kutoka lugha ambazo ajili yake si Tanzania. Kwa maneno mengine, wimbo huu unakosa "ubunifu wa kitaifa" na melodia za asili za Watanzania, mambo ambayo ni muhimu kwa wimbo wa taifa.

Binafsi nadhani hii ni hoja nzuri inayohitaji mjadala wa kina na wakitaifa. Wizara husika ingeanza kukusanya maoni kuhusu jambo hili mapema iwezekanavyo. Suala hili ni muhimu kuliko hata vazi la taifa.
Twende taratibu, melody zenye asili ya kitanzania ni zipi? Hivi unajua nini kiliyumbisha upatikanaji wa vazi la taifa? Kwa maoni yangu tuendelee na wimbo huu. kwani unahimiza kuthamini utanzania wetu na u Africa wetu. hizo gharama za kubuni wimbo tuzielekeze kwenye kutengeneza ajira za kudumu.
 
Twende taratibu, melody zenye asili ya kitanzania ni zipi? Hivi unajua nini kiliyumbisha upatikanaji wa vazi la taifa? Kwa maoni yangu tuendelee na wimbo huu. kwani unahimiza kuthamini utanzania wetu na u Africa wetu. hizo gharama za kubuni wimbo tuzielekeze kwenye kutengeneza ajira za kudumu.
Ni kweli twende taratibu. Rudia kusoma comment yangu taratibu.
 
Ni jambo la ajabu kusema hatuna wimbo wa taifa, ni kweli asili ya wimbo huu ni South Africa, Lakin haina mantiki kusema sio wa kwetu. Maneno ya Mungu ibariki Africa na melody ndio vina match na wa South Africa..... Lakin ni wetu ukizingatia tumekuwa wa Kwanza kupata Uhuru ni vyema kujivunia huu wimbo.... Tanzania Tanzania hauna hadhi ya kuwa wimbo wa taifa. Moja ni mrefu, pili hauna hisia. Kama huamni ulizia mzuka wa wimbo wa taifa ukiwa ume malizia course yoyote ya kijeshi. Tuna wimbo Mzuri, mfupi na wenye melody nzuri.
 
Back
Top Bottom