Tukubali yaishe?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,928
Nimeamka leo na mawazo ya ajabu sana! Maajabu kiasi cha kunishangaza mimi mwenyewe, na siyo tu kunishangaza bali kunistaajabisha kwa kunishangaza jinsi ninavyoshangaa! Hata hivyo ni mawazo ambayo kwa hakika ni ya mtu aliyefikia ukingoni... Tumepiga kelele hawakushtuka, tumeimba hawakucheza, na tumewaita hawakuitika! Wameamua kuendelea kufanya wafanyalo, kulinda walindalo, na kuendeleza kile kinachoitwa "libeneke".

Hata kama mtu ni shabiki wa timu ya mpira wa soka, kuna wakati ule ushabiki unakutoka hasa timu yako inapobugizwa magoli utadhani mchezo wa mpira wa kikapu. Ukifungwa goli moja unaweza kusikitika lakini bado ukaendelea kuishangalia timu, lakini goli la tatu, la nne, la tano, hata kama ni shabiki wa kuzaliwa inabidi uvue jezi na kuishangalia timu ya upinzani au kuamua kujing'atua uwanjani pole pole!

Bila ya shaka hadi hivi sasa hakuna shaka ni serikali gani tunayo mkononi, tunafahamu kwa hakika kuwa sera yao ya kulindana bado inaendelea, wako pole pole kushughulikia masuala ya mustakabali wa Taifa, na kwa hakika hadi hivi sasa hawana kipaumbele cha utendaji! Serikali haiwezi kufanya kila kitu kwa kiasi kikubwa ndani ya muda ule ule isipokuwa mpaka ichague kipaumbele na kipi kitangulie. Kama ni miundo mbinu, elimu, afya, madini n.k serikali makini ni lazima ijue inataka kuweka msisitizo wapi. Haiwezekani hata kidogo kumridisha kila mtu kwani matokeo yake hakuna atakayeridhika.

Waswahili walisema "panya wengi hawachimbi shimo refu". Maana ya msemo huo inashabihiana kabisa na ile "law of diminishing returns" ambapo inafika mahali faida inazidi kupungua pale vitu fulani (variables) vinazidi kuongezwa. Kwa kuongeza wakulima zaidi kwenye shamba la ekari moja haina maana mavuno yataleta faida zaidi! Kwa jinsi serikali yetu inavyokwenda nina uhakika tumefikia mahali pa diminishing returns na hatuna budi kupunguza vitu fulani.

Tupunguze vitu vya kufanya ndani ya miaka mitano ya mwanzo (sasa mitatu iliyosalia). Rais Kikwete na timu yake wake chini na kuingalia Ilani ya CCM na waamue kwa dhati ndani ya miaka mitatu iliyobakia ni nini kitatiliwa kipaumbele ili ifikapo 2010 angalau vitu hivyo viwe vimefikiwa angalau asilimia 95 ya malengo yake. Kwa kufanya hivi napendekeza kuwa na vipaumbele vya aina mbili.

a. Vipaumbele vya Msingi. Hivi ni vipaumbele ambavyo ni lazima serikali yoyote ihakikishe vinaendelezwa kila mwaka. Vipaumbele hivi vinahusu huduma za jamii (afya, elimu, na maji); vipaumbele vya Usalama (majeshi, ulinzi n.k) na vipaumbele vya miundo mbinu (barabara, umeme, simu n.k).

b. Vipaumbele vya Kati: Hivi ni vipaumbele ambavyo kila serikali inafanyia kazi kwa kadiri ya inavyochaguliwa. Mara nyingi vipaumbele hivi vinafuata sekta maalumu au eneo maalumu la kiuchumi. Lengo la vipaumbele hivi vya kati ni kufikia vipaumbele vya msingi. Maeneo ambayo serikali inaweza kuyatilia maanani katika sehemu hii ni vitu kama : Ubadilishaji wa sheria, utungaji wa taratibu, usimamizi na uchunguzi wa mambo fulani n.k Hivyo masuala kama ya mikataba n.k yangeweza kutiliwa maanani mara moja kwa kubadilisha taratibu na sheria na kufanya uchunguzi ili vipaumbele vya msingi viweze kufanikiwa pasipo matatizo.

Tatizo tulilonalo sasa ni kuwa watawala wetu wanajaribu kufanya mambo mengi kwa muda mfupi kwa kutumia watu wengi zaidi. Hili kwa hakika itakapofika 2010 tutajikuta hatujafanya mengi. Kwa vile watawala wetu wanajaribu kuridhisha kila mtu na kwa maneno yao mengi wanajaribu kufanya kila wawezalo kuonesha wako ontop of everything, na kwa sababu siamini hata kidogo kuwa wataweza kufanya yote waliyoyasema na kuyaahidi, nimeamua kuweka manyanga chini hasa katika suala la kuikosoa serikali.

Nimeamua na mimi kuungana na wale watafutao yale mazuri ya serikali na kuyapigia mbiu na kuyatangaza! Nimekubali yaishe... Nimekubali kuwa wao ndio watawala na walichaguliwa kwa asilimia 80, wanapendwa na wananchi na wanakubalika kutawala miaka mingine hamsini ijayo... kama walivyosema wengine "kama huwezi kuwashinda, jiunge nao".

CCM here I come, naomba kadi au ukada wa aina fulani....
 
Duh, mwanakijiji unasema kuwa umeamua kujiunga nao?ama nimekusoma vibaya?

Kama huwawezi jawabu sio kujiunga nao bali ni kuendelea kutafuta wengine wakuunge wewe kwa nguvu za hoja na sio kujiunga nao kwa vile tuu wamekushinda.

Ingekuwa wakikushinda unajiunga nao basi leo kusingekuwa na timu za simba na yanga tena na wala kusingekuwa na vyama vya siasa vinavyopingana duniani tena .

Nimesoma neno libeneke ,kwa kweli umenikumbusha mbali sana wakati nasoma shule ya sekondari mzambaraoni kule kwetu na hata nilipohamia chuo cha mrutunguru kule ukerewe tulikuwa tunafanya kusoma kwa libeneke, nawe hupaswi kujiunga nao iloa unapaswa kuendeleza libeneke mpaka kieleweke.
 
Nimeamka leo na mawazo ya ajabu sana! Maajabu kiasi cha kunishangaza mimi mwenyewe, na siyo tu kunishangaza bali kunistaajabisha kwa kunishangaza jinsi ninavyoshangaa! Hata hivyo ni mawazo ambayo kwa hakika ni ya mtu aliyefikia ukingoni... Tumepiga kelele hawakushtuka, tumeimba hawakucheza, na tumewaita hawakuitika! Wameamua kuendelea kufanya wafanyalo, kulinda walindalo, na kuendeleza kile kinachoitwa "libeneke".

Hata kama mtu ni shabiki wa timu ya mpira wa soka, kuna wakati ule ushabiki unakutoka hasa timu yako inapobugizwa magoli utadhani mchezo wa mpira wa kikapu. Ukifungwa goli moja unaweza kusikitika lakini bado ukaendelea kuishangalia timu, lakini goli la tatu, la nne, la tano, hata kama ni shabiki wa kuzaliwa inabidi uvue jezi na kuishangalia timu ya upinzani au kuamua kujing'atua uwanjani pole pole!

Bila ya shaka hadi hivi sasa hakuna shaka ni serikali gani tunayo mkononi, tunafahamu kwa hakika kuwa sera yao ya kulindana bado inaendelea, wako pole pole kushughulikia masuala ya mustakabali wa Taifa, na kwa hakika hadi hivi sasa hawana kipaumbele cha utendaji! Serikali haiwezi kufanya kila kitu kwa kiasi kikubwa ndani ya muda ule ule isipokuwa mpaka ichague kipaumbele na kipi kitangulie. Kama ni miundo mbinu, elimu, afya, madini n.k serikali makini ni lazima ijue inataka kuweka msisitizo wapi. Haiwezekani hata kidogo kumridisha kila mtu kwani matokeo yake hakuna atakayeridhika.

Waswahili walisema "panya wengi hawachimbi shimo refu". Maana ya msemo huo inashabihiana kabisa na ile "law of diminishing returns" ambapo inafika mahali faida inazidi kupungua pale vitu fulani (variables) vinazidi kuongezwa. Kwa kuongeza wakulima zaidi kwenye shamba la ekari moja haina maana mavuno yataleta faida zaidi! Kwa jinsi serikali yetu inavyokwenda nina uhakika tumefikia mahali pa diminishing returns na hatuna budi kupunguza vitu fulani.

Tupunguze vitu vya kufanya ndani ya miaka mitano ya mwanzo (sasa mitatu iliyosalia). Rais Kikwete na timu yake wake chini na kuingalia Ilani ya CCM na waamue kwa dhati ndani ya miaka mitatu iliyobakia ni nini kitatiliwa kipaumbele ili ifikapo 2010 angalau vitu hivyo viwe vimefikiwa angalau asilimia 95 ya malengo yake. Kwa kufanya hivi napendekeza kuwa na vipaumbele vya aina mbili.

a. Vipaumbele vya Msingi. Hivi ni vipaumbele ambavyo ni lazima serikali yoyote ihakikishe vinaendelezwa kila mwaka. Vipaumbele hivi vinahusu huduma za jamii (afya, elimu, na maji); vipaumbele vya Usalama (majeshi, ulinzi n.k) na vipaumbele vya miundo mbinu (barabara, umeme, simu n.k).

b. Vipaumbele vya Kati: Hivi ni vipaumbele ambavyo kila serikali inafanyia kazi kwa kadiri ya inavyochaguliwa. Mara nyingi vipaumbele hivi vinafuata sekta maalumu au eneo maalumu la kiuchumi. Lengo la vipaumbele hivi vya kati ni kufikia vipaumbele vya msingi. Maeneo ambayo serikali inaweza kuyatilia maanani katika sehemu hii ni vitu kama : Ubadilishaji wa sheria, utungaji wa taratibu, usimamizi na uchunguzi wa mambo fulani n.k Hivyo masuala kama ya mikataba n.k yangeweza kutiliwa maanani mara moja kwa kubadilisha taratibu na sheria na kufanya uchunguzi ili vipaumbele vya msingi viweze kufanikiwa pasipo matatizo.

Tatizo tulilonalo sasa ni kuwa watawala wetu wanajaribu kufanya mambo mengi kwa muda mfupi kwa kutumia watu wengi zaidi. Hili kwa hakika itakapofika 2010 tutajikuta hatujafanya mengi. Kwa vile watawala wetu wanajaribu kuridhisha kila mtu na kwa maneno yao mengi wanajaribu kufanya kila wawezalo kuonesha wako ontop of everything, na kwa sababu siamini hata kidogo kuwa wataweza kufanya yote waliyoyasema na kuyaahidi, nimeamua kuweka manyanga chini hasa katika suala la kuikosoa serikali.

Nimeamua na mimi kuungana na wale watafutao yale mazuri ya serikali na kuyapigia mbiu na kuyatangaza! Nimekubali yaishe... Nimekubali kuwa wao ndio watawala na walichaguliwa kwa asilimia 80, wanapendwa na wananchi na wanakubalika kutawala miaka mingine hamsini ijayo... kama walivyosema wengine "kama huwezi kuwashinda, jiunge nao".

CCM here I come, naomba kadi au ukada wa aina fulani....

MWANAKIJIJI UPO SERIOUS NA HILI ?? SEMA KAMA KWELI HALAFU UNITUMIE FULL INFO YAKO KAMILI ILI JAMAA WAKUTUMIE HIYO KADI YA UANACHAMA, KAMA KWELI UPO SERIOUS !
 
Duh, mwanakijiji unasema kuwa umeamua kujiunga nao?ama nimekusoma vibaya?

Kama huwawezi jawabu sio kujiunga nao bali ni kuendelea kutafuta wengine wakuunge wewe kwa nguvu za hoja na sio kujiunga nao kwa vile tuu wamekushinda.

Ingekuwa wakikushinda unajiunga nao basi leo kusingekuwa na timu za simba na yanga tena na wala kusingekuwa na vyama vya siasa vinavyopingana duniani tena .

Nimesoma neno libeneke ,kwa kweli umenikumbusha mbali sana wakati nasoma shule ya sekondari mzambaraoni kule kwetu na hata nilipohamia chuo cha mrutunguru kule ukerewe tulikuwa tunafanya kusoma kwa libeneke, nawe hupaswi kujiunga nao iloa unapaswa kuendeleza libeneke mpaka kieleweke.


Mkuu hamna tatizo lolote na yeye kujiunga na CCM iwapo atatimiza vigezo vyote vya kuwa mwanachama, tunamkaribisha kwa mikono yote miwili !
 
Nimeamka leo na mawazo ya ajabu sana! Maajabu kiasi cha kunishangaza mimi mwenyewe, na siyo tu kunishangaza bali kunistaajabisha kwa kunishangaza jinsi ninavyoshangaa! Hata hivyo ni mawazo ambayo kwa hakika ni ya mtu aliyefikia ukingoni... Tumepiga kelele hawakushtuka, tumeimba hawakucheza, na tumewaita hawakuitika! Wameamua kuendelea kufanya wafanyalo, kulinda walindalo, na kuendeleza kile kinachoitwa "libeneke".

Hata kama mtu ni shabiki wa timu ya mpira wa soka, kuna wakati ule ushabiki unakutoka hasa timu yako inapobugizwa magoli utadhani mchezo wa mpira wa kikapu. Ukifungwa goli moja unaweza kusikitika lakini bado ukaendelea kuishangalia timu, lakini goli la tatu, la nne, la tano, hata kama ni shabiki wa kuzaliwa inabidi uvue jezi na kuishangalia timu ya upinzani au kuamua kujing'atua uwanjani pole pole!

Bila ya shaka hadi hivi sasa hakuna shaka ni serikali gani tunayo mkononi, tunafahamu kwa hakika kuwa sera yao ya kulindana bado inaendelea, wako pole pole kushughulikia masuala ya mustakabali wa Taifa, na kwa hakika hadi hivi sasa hawana kipaumbele cha utendaji! Serikali haiwezi kufanya kila kitu kwa kiasi kikubwa ndani ya muda ule ule isipokuwa mpaka ichague kipaumbele na kipi kitangulie. Kama ni miundo mbinu, elimu, afya, madini n.k serikali makini ni lazima ijue inataka kuweka msisitizo wapi. Haiwezekani hata kidogo kumridisha kila mtu kwani matokeo yake hakuna atakayeridhika.

Waswahili walisema "panya wengi hawachimbi shimo refu". Maana ya msemo huo inashabihiana kabisa na ile "law of diminishing returns" ambapo inafika mahali faida inazidi kupungua pale vitu fulani (variables) vinazidi kuongezwa. Kwa kuongeza wakulima zaidi kwenye shamba la ekari moja haina maana mavuno yataleta faida zaidi! Kwa jinsi serikali yetu inavyokwenda nina uhakika tumefikia mahali pa diminishing returns na hatuna budi kupunguza vitu fulani.

Tupunguze vitu vya kufanya ndani ya miaka mitano ya mwanzo (sasa mitatu iliyosalia). Rais Kikwete na timu yake wake chini na kuingalia Ilani ya CCM na waamue kwa dhati ndani ya miaka mitatu iliyobakia ni nini kitatiliwa kipaumbele ili ifikapo 2010 angalau vitu hivyo viwe vimefikiwa angalau asilimia 95 ya malengo yake. Kwa kufanya hivi napendekeza kuwa na vipaumbele vya aina mbili.

a. Vipaumbele vya Msingi. Hivi ni vipaumbele ambavyo ni lazima serikali yoyote ihakikishe vinaendelezwa kila mwaka. Vipaumbele hivi vinahusu huduma za jamii (afya, elimu, na maji); vipaumbele vya Usalama (majeshi, ulinzi n.k) na vipaumbele vya miundo mbinu (barabara, umeme, simu n.k).

b. Vipaumbele vya Kati: Hivi ni vipaumbele ambavyo kila serikali inafanyia kazi kwa kadiri ya inavyochaguliwa. Mara nyingi vipaumbele hivi vinafuata sekta maalumu au eneo maalumu la kiuchumi. Lengo la vipaumbele hivi vya kati ni kufikia vipaumbele vya msingi. Maeneo ambayo serikali inaweza kuyatilia maanani katika sehemu hii ni vitu kama : Ubadilishaji wa sheria, utungaji wa taratibu, usimamizi na uchunguzi wa mambo fulani n.k Hivyo masuala kama ya mikataba n.k yangeweza kutiliwa maanani mara moja kwa kubadilisha taratibu na sheria na kufanya uchunguzi ili vipaumbele vya msingi viweze kufanikiwa pasipo matatizo.

Tatizo tulilonalo sasa ni kuwa watawala wetu wanajaribu kufanya mambo mengi kwa muda mfupi kwa kutumia watu wengi zaidi. Hili kwa hakika itakapofika 2010 tutajikuta hatujafanya mengi. Kwa vile watawala wetu wanajaribu kuridhisha kila mtu na kwa maneno yao mengi wanajaribu kufanya kila wawezalo kuonesha wako ontop of everything, na kwa sababu siamini hata kidogo kuwa wataweza kufanya yote waliyoyasema na kuyaahidi, nimeamua kuweka manyanga chini hasa katika suala la kuikosoa serikali.

Nimeamua na mimi kuungana na wale watafutao yale mazuri ya serikali na kuyapigia mbiu na kuyatangaza! Nimekubali yaishe... Nimekubali kuwa wao ndio watawala na walichaguliwa kwa asilimia 80, wanapendwa na wananchi na wanakubalika kutawala miaka mingine hamsini ijayo... kama walivyosema wengine "kama huwezi kuwashinda, jiunge nao".

CCM here I come, naomba kadi au ukada wa aina fulani....

Hongera sana kwa kugundua haya yote mkuu !
Ndio haya niliyokuwa nikipigia kelele humu Forum, lakini hakuna kibaya chochote kilichoharibika !
Ni vizuri kuwa umeelewa yote hayo, nakushauri Mkuu uachane na agano la zamani na ufungue kurasa mpya !
(ARI MPYA,NGUVU MPYA, KASI MPYA.)
 
Naamini hawezi kutimiza vigezo kwani yeye ni mtu asiyekubaliana na ufisadi na hilo pekee litamnyima sifa kwani hatakuwa mweenzao .....

Kama akijiunga basi hana haja ya kukaa kimya kama kautamaduni ketu kanavyosema kuwa hupaswi kuandika kwenye jf bali yazungumze kimya kimya ili yaishe yasiwafikie wengine....

Kada uliwahi kusoma mashairi na lugha za mafumbo?kama ndio usingekuwa na hamasa na mhemko wa kumkaribisha mwanakijiji haraka hivyo kwani anasema yupo kutangaza mazuri , nawe hatua ya kwanza ulipaswa kumpa mazuri ili yamvutie kwanza.......
 
Bravo!
"If you can beat us join us!"Sawa mkuu naona umeamua kumalizana nao na kukubali yaishe. Sisi bado tunaendeleza libeneke, hadi tuone hatima yake. Tutaendelea kusifia, kukosoa na kuonya pale inapobidi, hata kama maoni na maonyo yetu hayatafanyiwa kazi. Tutaendelea kumkumbusha Msola kuhusu matatizo ya elimu ya juu, tutaendelea kukomaa na Mama sita kuhusu watoto wa shule za msingi kukaa sakafuni bila madawati, tutaendelea kukomaa na Karamagi kuhusu mkataba feki wa Ki-Mangungu na mambo yanayofanana na hayo. Tutaendelea kumsifu muungwana kwa kupambana na ujambazi, ila hatutasita kumshauri kuwa majambazi wakubwa anao yeye mwenyewe nguoni mwake.
Tuendeleze libeneke.
 
I woke up very serious.. na sijiungi nao ili kukaa kimya ila kujaribu kuyatoa mawazo mumo kwa mumo. Kupiga kelele toka nje nadhani inafaa kwa wakati wake lakini wakati mwingine mabadiliko lazima yaletwe toka ndani. "Upinzani wa Kweli utatoka ndani ya CC" alisema Mwalimu na kwa mbali kama vile ukungu naweza kuona ukweli wa maneno hayo hasa baada ya uchaguzi Mkuu wa CCM uliopita.

Kada nifanyie mpango wa hiyo Kadi... na nitafurahi kupokea kadi ninapokuja kijijini Disemba/Januari katika moja ya mikutano ya wakubwa.. (usiniulize kwanini siwezi kupokea kimya kimya).. I can't wait to put the yellow and green attire.. !!
 
hayo mashairi nimesoma sana tena miaka ile kuna mwalimu wangu mmoja anaitwa Mshumbusi, huyu alikuwa baab kubwa aisee !

yeye kutokukubaliana na ccm siyo tatizo, maana pia binafsi nikiwa mwanachama kuna baadhi ya mambo sikubaliani nayo, but that doesnt provoke uanachama wangu !

sikia kitu kimoja, hii kitu inahitaji moyo sana ! kama yeye mwanakijiji alivyosema ni kwamba, ALIVYOAMKA LEO, kumaanisha anaweza akaamka kesho akasikia vingine, so its up to him to be consistence with this decision, after that he can commit to be a member of CHAMA CHA MAPINDUZI CCM !

Mkuu Mpaka kieleweke, trust me it doesnt take much kuwa mwanachama wa ccm regardless na utofauti, maana naamini kutofautiana kwa mawazo ndiko kunakofanya watu wawe krietivu au unasemaje ?
 
I woke up very serious.. na sijiungi nao ili kukaa kimya ila kujaribu kuyatoa mawazo mumo kwa mumo. Kupiga kelele toka nje nadhani inafaa kwa wakati wake lakini wakati mwingine mabadiliko lazima yaletwe toka ndani. "Upinzani wa Kweli utatoka ndani ya CC" alisema Mwalimu na kwa mbali kama vile ukungu naweza kuona ukweli wa maneno hayo hasa baada ya uchaguzi Mkuu wa CCM uliopita.

Kada nifanyie mpango wa hiyo Kadi... na nitafurahi kupokea kadi ninapokuja kijijini Disemba/Januari katika moja ya mikutano ya wakubwa.. (usiniulize kwanini siwezi kupokea kimya kimya).. I can't wait to put the yellow and green attire.. !!

Mhhhh,

Good luck Mwanakijiji,
Angalau CCM watapata mtu mwenye bollz!

Nimeku-imagine ukiwa umevaa yellow and green nikacheka like crazy! It is sad but I hope it's all for the greater good.
 
I woke up very serious.. na sijiungi nao ili kukaa kimya ila kujaribu kuyatoa mawazo mumo kwa mumo. Kupiga kelele toka nje nadhani inafaa kwa wakati wake lakini wakati mwingine mabadiliko lazima yaletwe toka ndani. "Upinzani wa Kweli utatoka ndani ya CC" alisema Mwalimu na kwa mbali kama vile ukungu naweza kuona ukweli wa maneno hayo hasa baada ya uchaguzi Mkuu wa CCM uliopita.

Kada nifanyie mpango wa hiyo Kadi... na nitafurahi kupokea kadi ninapokuja kijijini Disemba/Januari katika moja ya mikutano ya wakubwa.. (usiniulize kwanini siwezi kupokea kimya kimya).. I can't wait to put the yellow and green attire.. !!

babu unasema unataka kuleta upinzani ndani ya CC ? utafika huko,? ukipewa post moja utasahau upinzani milele wewe ! you dont think so ? waulize waliopewa watakwambia ! teh teh

kuhusu kadi poa mzee, ntaongea na jamaa then nitakujulisha !
 
MWANAKIJIJI UPO SERIOUS NA HILI ?? SEMA KAMA KWELI HALAFU UNITUMIE FULL INFO YAKO KAMILI ILI JAMAA WAKUTUMIE HIYO KADI YA UANACHAMA, KAMA KWELI UPO SERIOUS !

wewe kweli husomagi katikati ya mstari, yaani MKJJ amekuingiza mkenge kirahisi namna hii, duh! Yaani maneno yake mazito yote hujayaona isipokuwa haka ka-sentensi kamwisho tu basi?
 
I don't think Mwanakijiji is serious. I think what he wrote is sarcastic. Kuna wakati kule bcstimes.com yeye mwenyewe alisema kuwa ni mwanachama wa CCM na alimshabikia Kikwete. But lately he's been sounding more and more like he is in the opposition camp. So which is which? I just don't buy it a single bit..!!! Sorry...utajiunga mara ngapi na CCM?
 
nimemsoma sana, FORGET ABOUT WHAT HE SAID.... lets talk about the quotations i made ! tunamkaribisha, yeye ana uhuru wa kusema chochote anachoamini just like anybody else, hata ndani ya ccm sio wote wanaosema mazuri kuna wale pia wanaosema ovyo, wanaopingana na viongozi wa ccm na kadhalika !

tatizo liko wapi ??

mkenge huo kaingia kada au mwingine ??
 
wewe kweli husomagi katikati ya mstari, yaani MKJJ amekuingiza mkenge kirahisi namna hii, duh! Yaani maneno yake mazito yote hujayaona isipokuwa haka ka-sentensi kamwisho tu basi?

Ndiyo comprehension ya makada wengi wa CCM hiyo...na huyu Kada wetu humu anawakilisha wenzake vizuri sana....kwikwikwiiii
 
I don't think Mwanakijiji is serious. I think what he wrote is sarcastic. Kuna wakati kule bcstimes.com yeye mwenyewe alisema kuwa ni mwanachama wa CCM na alimshabikia Kikwete. But lately he's been sounding more and more like he is in the opposition camp. So which is which? I just don't buy it a single bit..!!! Sorry...utajiunga mara ngapi na CCM?

is he a flip flop now ?? mwanakijiji hapa inakuwaje bana ? anyway lets forget it kwanza tuangalie kukuhamisha uingie CCM !
 
Mhhhh,

Good luck Mwanakijiji,
Angalau CCM watapata mtu mwenye bollz!

Nimeku-imagine ukiwa umevaa yellow and green nikacheka like crazy! It is sad but I hope it's all for the greater good.


dadangu we, ni uamuzi wa machozi.. sasa hivi nimeoda kakofia kangu ka kijani kenye nembo ya jembe na nyunzo za rangi ya njano. Halafu shati litakuwa kama lile la Lowassa la rangi ya kijani kibichi (lime) la kumeta meta.. tatizo langu kubwa sijui kama nitapewa nafasi ya kufungua mdomo au ndio nimejikatia leseni ya ukimya..
 
I don't think Mwanakijiji is serious. I think what he wrote is sarcastic. Kuna wakati kule bcstimes.com yeye mwenyewe alisema kuwa ni mwanachama wa CCM na alimshabikia Kikwete. But lately he's been sounding more and more like he is in the opposition camp. So which is which? I just don't buy it a single bit..!!! Sorry...utajiunga mara ngapi na CCM?

I remember this too. Na nimekuwa nikijiuliza ni mwanakijiji yule wa bcs au? Kule nakumbuka kulikuwa na wanachama wawili wa CCM walikokuwa wanabishana juu ya nani anaijua zaidi CCM yaani Manakijiji na Mzee ES, je, unaikumbuka hii Nyani? Lakini sasa nilifikiri sio yule mwanakijiji wa kule. Kwa sababu kule kulikuwa na Mwanakijiji halafu baadaye akaibuka Mzee Mwanakijiji ambaye nafikiri ndiye huyu tuliye naye hapa. Naendelea kuamini kwamba kuna tofauti kati ya Mwanakijiji (kada wa CCM kule bcs) na Mzee Mwanakijiji (Thinker, debator, writer, lover of his country, controversial as he could be) ambaye ndiye huyu tuliye naye hapa.

Mzee Mwanakijiji unaweza kunitegulia hiki kitendawili msee wangu?
 
I don't think Mwanakijiji is serious. I think what he wrote is sarcastic. Kuna wakati kule bcstimes.com yeye mwenyewe alisema kuwa ni mwanachama wa CCM na alimshabikia Kikwete. But lately he's been sounding more and more like he is in the opposition camp. So which is which? I just don't buy it a single bit..!!! Sorry...utajiunga mara ngapi na CCM?

mzee Nyani, ushabiki wangu wa Kikwete haukuwa na kificho na mapenzi yangu kwa CCM sijawahi kuyaficha. Hata hivyo muda huo wote SIKUWA MWANACHAMA nilikuwa shabiki tu hasa ukizingatia nililelewa ndani ya CCM na kunyweshwa maji ya bendera. Na kwa muda wote sijawahi kuwa na kadi yoyote ile isipokuwa ya CCM niliyopewa miaka ileeeeee wakati natakiwa kwenda mafunzo ya Mgambo!(ila ilishaexpire baada ya kuukimbia mwenge 1984).

Niliomba kujiunga na CCM mapema mwaka huu lakini wakanipa masharti magumu gumu hivi ya kucompromise some of principles nikagoma tu. Ila sasa wataka au wasitake nitajiunga nao humo humo... kwani naamini ninatimiza masharti yote ya kuwa mwanachama.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom