FYATU
JF-Expert Member
- Dec 7, 2011
- 5,392
- 4,468
Iwe ni kwa wale wa kipato cha juu kati au cha chini...yaani kama Mke anatengeneza shilingi mia tano kwa siku na wewe Bw Mkubwa ni apeche alolo, ni ngumu sana kuwa na ndoa imara ya Mume na Mke wanaosikilizana na kuheshimiana.
Huenda kwa nje mtafanikiwa kutuonesha kana kwamba ndoa yenu ipo imara ila bado kuna mengi tu Mwanaume atakuwa anayakosa...Mwanaume bila uhuru wa 'kiume' ndani ya nyumba ni adhabu tosha.
Pale ambapo Mama ndiye anaweka chakula mezani, analipa kodi ya chumba, ananunua madaftari na kalamu za Watoto..... na wewe bwana mkubwa kila siku unarudi na koti begani huna hata pee mfukoni ni mtihani mkubwa hata kama utanyamaza kimya.
Mbaya zaidi kwa zile ndoa mabazo Jamaa alizifumania za mkupuo mahali, akafanikiwa kumsomesha Mtoto Mkali aliyetimia, mlaini kama sufi....na mkafanya harusi moja ya kifahari iliyoacha gumzo mjini.....miaka mitatu baadae ile milioni 50 ndio imekatika, shughuli haziend na Marafiki wamepukutika, my friend usitarajie mambo yatabaki kama yalivyozoeleka...ni either Mzee baba uwe mvumilivu wa visa vya Mke, au umkimbie umuache kama sio yeye kufanya hivyo.
Mimi siungi mkono hii tabia ya kikatili ya kukatisha uhai wa Mtu mwingine kama njia ya kulipiza kisasi, muachane kwa amani au muachane kwa amani mtaonana Mungu akipenda....maana kiukweli kuna mambo yanaweza yakakukwaza mpaka ukatamani tu liwalo na liwe.
Huenda kwa nje mtafanikiwa kutuonesha kana kwamba ndoa yenu ipo imara ila bado kuna mengi tu Mwanaume atakuwa anayakosa...Mwanaume bila uhuru wa 'kiume' ndani ya nyumba ni adhabu tosha.
Pale ambapo Mama ndiye anaweka chakula mezani, analipa kodi ya chumba, ananunua madaftari na kalamu za Watoto..... na wewe bwana mkubwa kila siku unarudi na koti begani huna hata pee mfukoni ni mtihani mkubwa hata kama utanyamaza kimya.
Mbaya zaidi kwa zile ndoa mabazo Jamaa alizifumania za mkupuo mahali, akafanikiwa kumsomesha Mtoto Mkali aliyetimia, mlaini kama sufi....na mkafanya harusi moja ya kifahari iliyoacha gumzo mjini.....miaka mitatu baadae ile milioni 50 ndio imekatika, shughuli haziend na Marafiki wamepukutika, my friend usitarajie mambo yatabaki kama yalivyozoeleka...ni either Mzee baba uwe mvumilivu wa visa vya Mke, au umkimbie umuache kama sio yeye kufanya hivyo.
Mimi siungi mkono hii tabia ya kikatili ya kukatisha uhai wa Mtu mwingine kama njia ya kulipiza kisasi, muachane kwa amani au muachane kwa amani mtaonana Mungu akipenda....maana kiukweli kuna mambo yanaweza yakakukwaza mpaka ukatamani tu liwalo na liwe.