Tukubali mfumo wa kuchapana viboko, utatusaidia mbeleni

Teamo

JF-Expert Member
Jan 9, 2009
12,272
1,034
SOURCE:SAUTI TA WATU TANZANIA DAIMA-salehe moohamed


MWANZONI mwa wiki hii, Rais Jakaya Kikwete, aliamua kumfukuza kazi Mkuu wa Wilaya ya Bukoba, Albert Mnali, kwa kosa la kuwachapa viboko walimu wa shule za msingi, ambao shule zao hazikufaulisha wanafunzi wengi kuingia shule za sekondari.

Binafsi sikukipenda kitendo alichokifanya mkuu huyo wa wilaya, kwa kuwa kiliwadhalilisha walimu lakini pia alitoa adhabu bila ya kuangalia mazingira magumu wanayofanyia kazi walimu hapa nchini.

Tuangalie upande wa pili wa shilingi, hivi ni kweli DC yule alifanya kitendo kile kwa kuwa anawachukia walimu au kwa kuwa aliudhika na matokeo mabovu ya wanafunzi ambao tunaamini ndio taifa la kesho na wanahitaji elimu bora ili waweze kukabiliana na changamoto za dunia kwa lengo la kuikwamua nchi kiuchumi.

Pamoja na kutokubalina na uamuzi aliouchukua DC huyo lakini nampongeza kwa kuwa mbunifu wa adhabu inayofaa kwa watu wasiotenda kazi kwa ufanisi unaotakiwa katika jamii, hasa wale ambao sekta zao zinaonekana kuwa na mazingira mazuri ya utendaji kazi.

Mfumo huu kama ukianza kutumika, watendaji wa halmashauri, mkoa na wizara nina hakika utakuwa mzuri kwa kuwa baadhi ya watendaji wamekuwa na tabia ya kufanya kazi kwa mazoea, tena kwa kuendekeza urasimu ili mradi yule ambaye anatakiwa kupata huduma asiweze kuipata kwa muda unaotakiwa na ikiwezekana atoe rushwa ili ahudumiwe.

Leo hii askari wa usalama wa barabarani kila kukicha wamekuwa wakishiriki katika vitendo vya rushwa kwa kuyaachia mabasi makubwa na daladala kuvunja sheria mbalimbali za barabarani, ambazo mwisho wake ni ajali na vifo vya watu wasio na hatia.

Hawa tukiwachapa viboko kwa uzembe wao hatutakuwa na tatizo na tena kama ikiwezekana wachapwe mbele ya vyombo vya habari ili kesho na wengine wenye nia ya kufanya makosa hayo wasiweze kuyafanya ili kukwepa kudhalilishwa na kuchukuliwa hatua za kinidhamu, ikiwemo kufukuzwa kazi.

Baada ya hapo tuhamie kwa watendaji wa wizara ambao muda mwingi hukaa na kubuni mbinu za kufuja rasilimali za taifa bila kujali wizi huo huathiri wananchi, hasa kwa kukosa huduma za kijamii kama vile maji, umeme, dawa zahanati na nyinginezo.

Hawa wamekuwa kikwazo kikubwa cha maendeleo ya taifa ambapo wakati mwingine wamekuwa wakiingia mikataba mbalimbali kwa lengo la kujipatia asilimia 10 ‘ten pacent’ ili hali wakijua kabisa wawekezaji hao hawana uwezo wa kuendesha mradi husika au mwekezaji husika ana lengo la kuinufaisha zaidi nchi anayotoka.

Ni aibu leo hii mwekezaji wa hoteli kuajiri mpaka mfagiaji kutoka nje ilhali Watanzania wapo wengi, wengine huagiza hata nyanya, vitunguu, kuku na bidhaa nyinginezo kutoka nchi za nje ilhali Iringa, Mbeya, Morogoro na mikoa mingine inazalisha kwa wingi bidhaa hizo mpaka nyingine zinaozea mashambani.

Viboko wanastahili watendaji hawa na wala si walimu ambao kuanzia malazi, chakula, mishahara na huduma za jamii huzipata kwa kiwango duni kulinganisha na wanasiasa ambao wamekuwa mstari wa mbele kuandaa na kutetea masilahi manono wawapo ndani na nje ya Bunge.

Wakati mwingine ili binadamu aweze kujifunza ni lazima yatokee makosa na atokee mtu wa kuyasahihisha makosa hayo, DC Mnali ametuonyesha njia, si vibaya na sisi kuangalia utaratibu huu ambao nina imani ipo siku tutaanza kuwachapa na viongozi wa ngazi za juu.

Nitafurahi zaidi pale rais atakapochapwa viboko hadharani kwa kosa la kutotimiza ahadi yake ya maisha bora kwa kila Mtanzania kama alivyoahidi katika kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2005.

Si kila mtu ni shuhuda wa hayo maisha yaliyoahidiwa kama yametimia? Leo hii maisha yamezidi kudorora na hata yule aliyekuwa na uwezo wa kununua fungu la dagaa hivi sasa hana tena uwezo wa kununua kutokana na kupanda kwa gharama za maisha.

Tukimaliza kumchapa viboko rais tuhamie kwa mawaziri wake ambao nao wamekuwa mzigo mkubwa kwa taifa kuliko hata kile wanachokizalisha, hasa kwa kushindwa kufanya mambo mbalimbali yenye tija kwa nchi na badala yake wamekuwa wakijilimbikizia mali kiasi ya kuonekana ni wafanyabiashara, badala ya watoa huduma kwa jamii.

Leo hii waziri amekuwa mfalme na mwananchi wamegeuzwa kuwa mtwana wakati mwananchi ndiye ambaye anapaswa kuhudumiwa (mfalme), huu ni udhaifu na kama tusipochapana viboko hatutaweza kubadilika.

Kwa nini tusiwachape watendaji wa baraza la mitihani la taifa ambao kwa miaka kadhaa hivi sasa wamekuwa wakidaiwa kuvujisha mitihani pamoja na kuuza baadhi ya vyeti kwa watu wasiohitimu elimu husika au kupata alama ndogo katika mitihani yao ya mwisho.

Mbona hatuwachapi viboko wahadhiri wa vyuo vyetu ambao hutoa shahada kwa wahitimu wa vyuo baada ya kupewa rushwa ya ngono au fedha, hawa si ndio hatari kwa maendeleo ya taifa kuliko hata ugonjwa wa ukimwi?

Hawa wanastahili viboko, tena vya mkia wa taa, athari ya kuwa na wataalamu wenye elimu bandia ni kubwa zaidi katika sekta ya uchumi, afya elimu na nyinginezo kuliko hata huku kumfukuza DC aliyejaribu kuweka historia katika jamii kwa kuwacharaza viboko walimu ambao kwake aliona kutofika kazini mapema ni moja ya sababu zilizowakwamisha wanafunzi kufaulu.
 
Kuchapa fimbo wanasema eti sii haki za binadamu!

Je uzembe, ubadhirifu, wizi ufisadi na uhujumu wa uchumi unaleta vifo kwa watoto wadogo tena wengi..hizi ndo haki za binadamu??

Sasa hawa wezi wa EPA na Bot wakichapwa fimbo hadharani..je ni kinyume cha haki za binadmu?

Duties and obligations kwanza...then ndo human rights
 
Last edited:
SOURCE:SAUTI TA WATU TANZANIA DAIMA-salehe moohamed


MWANZONI mwa wiki hii, Rais Jakaya Kikwete, aliamua kumfukuza kazi Mkuu wa Wilaya ya Bukoba, Albert Mnali, kwa kosa la kuwachapa viboko walimu wa shule za msingi, ambao shule zao hazikufaulisha wanafunzi wengi kuingia shule za sekondari.

Binafsi sikukipenda kitendo alichokifanya mkuu huyo wa wilaya, kwa kuwa kiliwadhalilisha walimu lakini pia alitoa adhabu bila ya kuangalia mazingira magumu wanayofanyia kazi walimu hapa nchini.

Tuangalie upande wa pili wa shilingi, hivi ni kweli DC yule alifanya kitendo kile kwa kuwa anawachukia walimu au kwa kuwa aliudhika na matokeo mabovu ya wanafunzi ambao tunaamini ndio taifa la kesho na wanahitaji elimu bora ili waweze kukabiliana na changamoto za dunia kwa lengo la kuikwamua nchi kiuchumi.

Pamoja na kutokubalina na uamuzi aliouchukua DC huyo lakini nampongeza kwa kuwa mbunifu wa adhabu inayofaa kwa watu wasiotenda kazi kwa ufanisi unaotakiwa katika jamii, hasa wale ambao sekta zao zinaonekana kuwa na mazingira mazuri ya utendaji kazi.

Mfumo huu kama ukianza kutumika, watendaji wa halmashauri, mkoa na wizara nina hakika utakuwa mzuri kwa kuwa baadhi ya watendaji wamekuwa na tabia ya kufanya kazi kwa mazoea, tena kwa kuendekeza urasimu ili mradi yule ambaye anatakiwa kupata huduma asiweze kuipata kwa muda unaotakiwa na ikiwezekana atoe rushwa ili ahudumiwe.

Leo hii askari wa usalama wa barabarani kila kukicha wamekuwa wakishiriki katika vitendo vya rushwa kwa kuyaachia mabasi makubwa na daladala kuvunja sheria mbalimbali za barabarani, ambazo mwisho wake ni ajali na vifo vya watu wasio na hatia.

Hawa tukiwachapa viboko kwa uzembe wao hatutakuwa na tatizo na tena kama ikiwezekana wachapwe mbele ya vyombo vya habari ili kesho na wengine wenye nia ya kufanya makosa hayo wasiweze kuyafanya ili kukwepa kudhalilishwa na kuchukuliwa hatua za kinidhamu, ikiwemo kufukuzwa kazi.

Baada ya hapo tuhamie kwa watendaji wa wizara ambao muda mwingi hukaa na kubuni mbinu za kufuja rasilimali za taifa bila kujali wizi huo huathiri wananchi, hasa kwa kukosa huduma za kijamii kama vile maji, umeme, dawa zahanati na nyinginezo.

Hawa wamekuwa kikwazo kikubwa cha maendeleo ya taifa ambapo wakati mwingine wamekuwa wakiingia mikataba mbalimbali kwa lengo la kujipatia asilimia 10 ‘ten pacent’ ili hali wakijua kabisa wawekezaji hao hawana uwezo wa kuendesha mradi husika au mwekezaji husika ana lengo la kuinufaisha zaidi nchi anayotoka.

Ni aibu leo hii mwekezaji wa hoteli kuajiri mpaka mfagiaji kutoka nje ilhali Watanzania wapo wengi, wengine huagiza hata nyanya, vitunguu, kuku na bidhaa nyinginezo kutoka nchi za nje ilhali Iringa, Mbeya, Morogoro na mikoa mingine inazalisha kwa wingi bidhaa hizo mpaka nyingine zinaozea mashambani.

Viboko wanastahili watendaji hawa na wala si walimu ambao kuanzia malazi, chakula, mishahara na huduma za jamii huzipata kwa kiwango duni kulinganisha na wanasiasa ambao wamekuwa mstari wa mbele kuandaa na kutetea masilahi manono wawapo ndani na nje ya Bunge.

Wakati mwingine ili binadamu aweze kujifunza ni lazima yatokee makosa na atokee mtu wa kuyasahihisha makosa hayo, DC Mnali ametuonyesha njia, si vibaya na sisi kuangalia utaratibu huu ambao nina imani ipo siku tutaanza kuwachapa na viongozi wa ngazi za juu.

Nitafurahi zaidi pale rais atakapochapwa viboko hadharani kwa kosa la kutotimiza ahadi yake ya maisha bora kwa kila Mtanzania kama alivyoahidi katika kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2005.

Si kila mtu ni shuhuda wa hayo maisha yaliyoahidiwa kama yametimia? Leo hii maisha yamezidi kudorora na hata yule aliyekuwa na uwezo wa kununua fungu la dagaa hivi sasa hana tena uwezo wa kununua kutokana na kupanda kwa gharama za maisha.

Tukimaliza kumchapa viboko rais tuhamie kwa mawaziri wake ambao nao wamekuwa mzigo mkubwa kwa taifa kuliko hata kile wanachokizalisha, hasa kwa kushindwa kufanya mambo mbalimbali yenye tija kwa nchi na badala yake wamekuwa wakijilimbikizia mali kiasi ya kuonekana ni wafanyabiashara, badala ya watoa huduma kwa jamii.

Leo hii waziri amekuwa mfalme na mwananchi wamegeuzwa kuwa mtwana wakati mwananchi ndiye ambaye anapaswa kuhudumiwa (mfalme), huu ni udhaifu na kama tusipochapana viboko hatutaweza kubadilika.

Kwa nini tusiwachape watendaji wa baraza la mitihani la taifa ambao kwa miaka kadhaa hivi sasa wamekuwa wakidaiwa kuvujisha mitihani pamoja na kuuza baadhi ya vyeti kwa watu wasiohitimu elimu husika au kupata alama ndogo katika mitihani yao ya mwisho.

Mbona hatuwachapi viboko wahadhiri wa vyuo vyetu ambao hutoa shahada kwa wahitimu wa vyuo baada ya kupewa rushwa ya ngono au fedha, hawa si ndio hatari kwa maendeleo ya taifa kuliko hata ugonjwa wa ukimwi?

Hawa wanastahili viboko, tena vya mkia wa taa, athari ya kuwa na wataalamu wenye elimu bandia ni kubwa zaidi katika sekta ya uchumi, afya elimu na nyinginezo kuliko hata huku kumfukuza DC aliyejaribu kuweka historia katika jamii kwa kuwacharaza viboko walimu ambao kwake aliona kutofika kazini mapema ni moja ya sababu zilizowakwamisha wanafunzi kufaulu.




Issue hapa ni aina ya adhabu iliyotekelezwa kwa walimu hao ambayo haikustahili kwa mujibu wa sheria. sasa ukisema huo ndio uwe utaratibu wa kuwaadabisha watu huko ni kukosa busara ktk utoaji uamuzi. Kuna adhabu mbalimbali ikiwemo kusimamishwa kazi,kufukuzwa n.k na zote hizo zina utaratibu wake kabla ya kufanyiwa kazi,ukiona mtu anatetea viboko ujue kishafika mwisho wa kutafakari ni lazima kuwepo na Rule of Law. Haki za bina damu ni lazima ziheshimiwe uwezi kusema tu mtu amekuwa mzembe basi achapwe viboko bila kujali litakalotokea baada ya kuchapwa hivyo kwa hiyo kesho wewe utasema tena adhabu nyingine iwe kubakwa kwa mwanamke atakayechelewa kazi na mwanaume hivyo hivyo kama ilivyowai kutokea Pakistan kosa alilofanya kaka mtu adhabu akapewa dada yake ya kubakwa. Tatizo sisi ni mfumo mzima wa uongozi ndio unatumaliza kwani walimu wakilipwa maslahi yao hakuna atakayechelewa au kutofika kazini bila sababu, hiyo pia ni pamoja maeneo mengine ya kazi kama hakuna uwajibikaji wa kiuongozi watu watachwelewa tu kazini,kwa hiyo kuchapwa viboko kama unamchapa mwanao ni udharirishaji hatutaki kurudi nyuma enzi ya ukoloni ambapo babu zetu walikuwa wakidharirishwa kwa viboko au ndio uafrika wenyewe huo?. Tuacheni ujinga,suala hili haliitaji elimu ya chuo kukuu kulielewa.
 
Issue hapa ni aina ya adhabu iliyotekelezwa kwa walimu hao ambayo haikustahili kwa mujibu wa sheria. sasa ukisema huo ndio uwe utaratibu wa kuwaadabisha watu huko ni kukosa busara ktk utoaji uamuzi. Kuna adhabu mbalimbali ikiwemo kusimamishwa kazi,kufukuzwa n.k na zote hizo zina utaratibu wake kabla ya kufanyiwa kazi,ukiona mtu anatetea viboko ujue kishafika mwisho wa kutafakari ni lazima kuwepo na Rule of Law. Haki za bina damu ni lazima ziheshimiwe uwezi kusema tu mtu amekuwa mzembe basi achapwe viboko bila kujali litakalotokea baada ya kuchapwa hivyo kwa hiyo kesho wewe utasema tena adhabu nyingine iwe kubakwa kwa mwanamke atakayechelewa kazi na mwanaume hivyo hivyo kama ilivyowai kutokea Pakistan kosa alilofanya kaka mtu adhabu akapewa dada yake ya kubakwa. Tatizo sisi ni mfumo mzima wa uongozi ndio unatumaliza kwani walimu wakilipwa maslahi yao hakuna atakayechelewa au kutofika kazini bila sababu, hiyo pia ni pamoja maeneo mengine ya kazi kama hakuna uwajibikaji wa kiuongozi watu watachwelewa tu kazini,kwa hiyo kuchapwa viboko kama unamchapa mwanao ni udharirishaji hatutaki kurudi nyuma enzi ya ukoloni ambapo babu zetu walikuwa wakidharirishwa kwa viboko au ndio uafrika wenyewe huo?. Tuacheni ujinga,suala hili haliitaji elimu ya chuo kukuu kulielewa.


mwanaluguma,

Unayoongea ni sahihi..mimi nachopinga ni watu kuwa wazembe na kujificha ktk kigezo cha Human Rights! Rights huendana na duties and Obligations!

Ktk nchi nyingi zilizoendelea utaona Authoritarian states..na sera nzuri na vision na uzalendo wa hali ya juu.. huleta maendeleo ..tena haraka zaidi!

Sii lazima viboko..we need a system of Law kama China au Singapore...kuweka kwanza nidhamu ya kazi..ili watu wazalishe..na wazoee kufanya kazi!

Hii kwa kama miaka 10-15... then watu wakishakuwa wanawajibika na kuiogopa serikali..na sheria tulizo nazo..then...ndo tufikirie Human rights!

Nadhani unanielewa!

Ni sheria hizi hizi zinawafanya wakubwa wakiiba wanapeta..na wezi wa kuku wanafungwa!

Sasa watu wanaoshababisha hasara kubwa kama ya 200 Biliions BoT au EPA wakicharazwa viboko..tena hadharani..tena mbele ya wake zao...sii sawa tu..iwe fundisho kwa wengine??

We need to make a reality check kama kweli Utawala wetu na sheria za sasa zinatupeleka kisahihi?

Mimi naona kuna walakini!
 
Huu mfumo utakuwa mzuri sana, kwani Tanzania ni nini ambacho hatuna cha kutufanya tuendelee kuwa omba omba na kuchekelea misaada kutoka nje ni nini hasa kama siyo UZEMBE.Juzi rais wa China kaja Tanzania, watu wanakenua tu meno kwa misaada aliyotoa, kwani china imefikaje hapo ilipo, kosa moja moja tu la uzembe, wao syo fimbo, ni kifo moja kwa moja, sasa hapa kwetu fimbo tu,CCW wanasema ametokwa na damu siku tatu, non-sense.Bila kujituma sisi wenywewe hata kwa kuchapana bakora hata tupewe misaada kiasi gani hatuwezi kufika popote ndugu zanguni.Mimi binafisi naomba hili jambo lipewe uzito wake na hata ikibidi lipitishwe na bungeni iwe sheria, then tupime baada ya miaka mitano tutakuwa wapi.
 
mwanaluguma,

Unayoongea ni sahihi..mimi nachopinga ni watu kuwa wazembe na kujificha ktk kigezo cha Human Rights! Rights huendana na duties and Obligations!

Ktk nchi nyingi zilizoendelea utaona Authoritarian states..na sera nzuri na vision na uzalendo wa hali ya juu.. huleta maendeleo ..tena haraka zaidi!

Sii lazima viboko..we need a system of Law kama China au Singapore...kuweka kwanza nidhamu ya kazi..ili watu wazalishe..na wazoee kufanya kazi!

Hii kwa kama miaka 10-15... then watu wakishakuwa wanawajibika na kuiogopa serikali..na sheria tulizo nazo..then...ndo tufikirie Human rights!

Nadhani unanielewa!

Ni sheria hizi hizi zinawafanya wakubwa wakiiba wanapeta..na wezi wa kuku wanafungwa!

Sasa watu wanaoshababisha hasara kubwa kama ya 200 Biliions BoT au EPA wakicharazwa viboko..tena hadharani..tena mbele ya wake zao...sii sawa tu..iwe fundisho kwa wengine??

We need to make a reality check kama kweli Utawala wetu na sheria za sasa zinatupeleka kisahihi?

Mimi naona kuna walakini!



Kama unaamini katika Rule of law basi basi utakubaliana nami kuwa utungaji wa sheria unaenda pamoja na uzingatiaji haki za binadamu. Ukweli ni kuwa adhabu ya viboko Tanzania tunayo yaani ''Corporal Punishment'' lakini kuna makosa ambayo adhabu hiyo imeruhusiwa kutumika hiyoni pamoja na umri wa mtu kama utasoma ile sheria ya utekelezaji adhabu ya viboko ya 1949. Lakini huko kote si muhimu sana, muhimu ni kitendo cha kutekelezwa adhabu inayostahili kutolewa na mahakama kwa utaratibu batiri eti kwa kisingizio cha uzembe wa walimu. Duties and obligations unazosema zinaanzia kwa kiongozi,kwa hiyo ata mnali angepaswa kuzingatia hilo yeye kama kiongozi hakupaswa kutoa adhabu ile bila kuheshimu utaratibu wa utumishi wa umma. Mambo ya jazba hayana nafasi tena, huu si wakati wa mob justice kwamba mwizi kaiba basi kila mtu anampiga mawe. Hakuna anayependa walimu wasifundishe darasani kwa sababu ya uzembe,lakini mpaka kuumfikia mwalimu mzembe umeanzia wapi? maana yake hata mnali pia alistahili kuchapwa viboko "so to speak".
 
Naona Mnali anazidi kupata umaarufu kwa kitendo chake cha "kishujaa"......mgawanyiko ni mkubwa sana hata watu hawajui wanasimama wapi kwenye suala hilo kimsimamo...kazi kwelii mm namshauri JK amchukue jamaa awe msaidizi mtendaji wa waziri wa Serikali za mitaa maana kule ndio kuna uozo kuliko akawakimbize sana wale jamaa...wakurugenzi na madiwani wao....
 
Kuchapa viboko ni u-primitive tu. Mbona viboko vinatumika sana mashuleni wakati wa kufundisha hisabati au English na bado watu mambumbumbu :confused:
 
Jamani lets be serious...
Hivi Mheshimiwa Mnali amewahi kuwachukulia hatua zozote za kinidhamu waalimu wazembe katika wilaya yake kabla ya tukio hili? Kama amewahi kuchukua hatua zozote na aseme wazi wazi kwamba ameshahangaika sana kuwakanya waalimu wale kuhusu uzembe lakini wakawa hawashikiki...
Na hili ndio tatizo letu kubwa sasa hivi, sheria na taratibu zipo, vyombo vya kisheria na kinidhamu vipo lakini hatutaki kwenda njia hiyo na kukimbilia kufanya mambo kwa jazba...walimu wazembe wachapwe viboko, wauaji maalbino nao wauwawe papo hapo...nk
 
Jamani lets be serious...
Hivi Mheshimiwa Mnali amewahi kuwachukulia hatua zozote za kinidhamu waalimu wazembe katika wilaya yake kabla ya tukio hili? Kama amewahi kuchukua hatua zozote na aseme wazi wazi kwamba ameshahangaika sana kuwakanya waalimu wale kuhusu uzembe lakini wakawa hawashikiki...
Na hili ndio tatizo letu kubwa sasa hivi, sheria na taratibu zipo, vyombo vya kisheria na kinidhamu vipo lakini hatutaki kwenda njia hiyo na kukimbilia kufanya mambo kwa jazba...walimu wazembe wachapwe viboko, wauaji maalbino nao wauwawe papo hapo...nk
Kwa maoni yangu si walimu pekee walio wazembe na kama kuna haja ya kuchapa viboko wazembe, asilimia 8o ya wafanyakazi wa Tanzania wanastahili viboko. Kama nasema uongo tembelea ofisi za serikali na utaona kila aina ya madudu si kuchelewa tu bali hata utendaji kazi mbaya. Hakuna huduma za kulidhisha.
Hawa wote nao wanastahili viboko
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom